Ezekiel 6 (BOKCV)
1 Neno la BWANA likanijia kusema, 2 “Mwanadamu, elekeza uso wako kukabili milima ya Israeli, utabiri dhidi yake 3 na useme: ‘Ee milima ya Israeli, sikia neno la BWANA Mwenyezi. Hili ndilo BWANA Mwenyezi aliambiayo milima na vilima, magenge na mabonde: Ninakaribia kuleta upanga dhidi yenu, nami nitapaharibu mahali penu pote pa juu pa kuabudia miungu. 4 Madhabahu yenu yatabomolewa na madhabahu yenu ya kufukizia uvumba yatavunjavunjwa, nami nitawachinja watu wenu mbele ya sanamu zenu. 5 Nitazilaza maiti za Waisraeli mbele ya sanamu zao, nami nitatawanya mifupa yenu kuzunguka madhabahu yenu. 6 Popote mnapoishi, miji hiyo itafanywa ukiwa na mahali pa juu pa kuabudia miungu patabomolewa, ili madhabahu yenu ifanywe ukiwa na kuharibiwa, sanamu zenu zitavunjavunjwa na kuharibiwa, madhabahu yenu ya kufukizia uvumba yatabomolewa na kila mlichokifanya kitakatiliwa mbali. 7 Watu wenu watachinjwa katikati yenu, nanyi mtatambua Mimi ndimi BWANA. 8 “ ‘Lakini nitawabakiza hai baadhi yenu, kwa kuwa baadhi yenu watanusurika kuuawa watakapokuwa wametawanyika katika nchi na mataifa. 9 Ndipo katika mataifa ambamo watakuwa wamechukuliwa mateka, wale ambao watanusurika watanikumbuka, jinsi ambavyo nimehuzunishwa na mioyo yao ya uzinzi, ambayo imegeukia mbali nami na macho yao ambayo yametamani sanamu zao. Watajichukia wenyewe kwa ajili ya uovu walioutenda na kwa ajili ya desturi zao za kuchukiza. 10 Nao watajua kuwa Mimi ndimi BWANA, sikuwaonya bure kuwa nitaleta maafa hayo yote juu yao. 11 “ ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Piga makofi, kanyaga chini kwa mguu na upige kelele, “Ole!” kwa sababu ya maovu yote na machukizo yote yanayofanywa na nyumba ya Israeli, kwa kuwa wataanguka kwa upanga, njaa na tauni. 12 Yeye aliye mbali sana atakufa kwa tauni, naye aliye karibu atauawa kwa upanga, naye yule atakayenusurika na kubaki atakufa kwa njaa. Hivyo ndivyo nitakavyotimiza ghadhabu yangu dhidi yao. 13 Nao watajua kwamba Mimi ndimi BWANA, wakati maiti za watu wao zitakapokuwa zimelala katikati ya sanamu zao kuzunguka madhabahu yao, juu ya kila kilima kilichoinuka na juu ya vilele vyote vya milima, chini ya kila mti uliotanda na kila mwaloni wenye majani, yaani, sehemu walizofukizia uvumba kwa sanamu zao zote. 14 Nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yao na kuifanya nchi yao ukiwa, kuanzia jangwani hadi Dibla, kila mahali wanapoishi. Ndipo watakapojua ya kwamba Mimi ndimi BWANA.’ ”
In Other Versions
Ezekiel 6 in the ANGEFD
Ezekiel 6 in the ANTPNG2D
Ezekiel 6 in the AS21
Ezekiel 6 in the BAGH
Ezekiel 6 in the BBPNG
Ezekiel 6 in the BBT1E
Ezekiel 6 in the BDS
Ezekiel 6 in the BEV
Ezekiel 6 in the BHAD
Ezekiel 6 in the BIB
Ezekiel 6 in the BLPT
Ezekiel 6 in the BNT
Ezekiel 6 in the BNTABOOT
Ezekiel 6 in the BNTLV
Ezekiel 6 in the BOATCB
Ezekiel 6 in the BOATCB2
Ezekiel 6 in the BOBCV
Ezekiel 6 in the BOCNT
Ezekiel 6 in the BOECS
Ezekiel 6 in the BOGWICC
Ezekiel 6 in the BOHCB
Ezekiel 6 in the BOHCV
Ezekiel 6 in the BOHLNT
Ezekiel 6 in the BOHNTLTAL
Ezekiel 6 in the BOICB
Ezekiel 6 in the BOILNTAP
Ezekiel 6 in the BOITCV
Ezekiel 6 in the BOKCV2
Ezekiel 6 in the BOKHWOG
Ezekiel 6 in the BOKSSV
Ezekiel 6 in the BOLCB
Ezekiel 6 in the BOLCB2
Ezekiel 6 in the BOMCV
Ezekiel 6 in the BONAV
Ezekiel 6 in the BONCB
Ezekiel 6 in the BONLT
Ezekiel 6 in the BONUT2
Ezekiel 6 in the BOPLNT
Ezekiel 6 in the BOSCB
Ezekiel 6 in the BOSNC
Ezekiel 6 in the BOTLNT
Ezekiel 6 in the BOVCB
Ezekiel 6 in the BOYCB
Ezekiel 6 in the BPBB
Ezekiel 6 in the BPH
Ezekiel 6 in the BSB
Ezekiel 6 in the CCB
Ezekiel 6 in the CUV
Ezekiel 6 in the CUVS
Ezekiel 6 in the DBT
Ezekiel 6 in the DGDNT
Ezekiel 6 in the DHNT
Ezekiel 6 in the DNT
Ezekiel 6 in the ELBE
Ezekiel 6 in the EMTV
Ezekiel 6 in the ESV
Ezekiel 6 in the FBV
Ezekiel 6 in the FEB
Ezekiel 6 in the GGMNT
Ezekiel 6 in the GNT
Ezekiel 6 in the HARY
Ezekiel 6 in the HNT
Ezekiel 6 in the IRVA
Ezekiel 6 in the IRVB
Ezekiel 6 in the IRVG
Ezekiel 6 in the IRVH
Ezekiel 6 in the IRVK
Ezekiel 6 in the IRVM
Ezekiel 6 in the IRVM2
Ezekiel 6 in the IRVO
Ezekiel 6 in the IRVP
Ezekiel 6 in the IRVT
Ezekiel 6 in the IRVT2
Ezekiel 6 in the IRVU
Ezekiel 6 in the ISVN
Ezekiel 6 in the JSNT
Ezekiel 6 in the KAPI
Ezekiel 6 in the KBT1ETNIK
Ezekiel 6 in the KBV
Ezekiel 6 in the KJV
Ezekiel 6 in the KNFD
Ezekiel 6 in the LBA
Ezekiel 6 in the LBLA
Ezekiel 6 in the LNT
Ezekiel 6 in the LSV
Ezekiel 6 in the MAAL
Ezekiel 6 in the MBV
Ezekiel 6 in the MBV2
Ezekiel 6 in the MHNT
Ezekiel 6 in the MKNFD
Ezekiel 6 in the MNG
Ezekiel 6 in the MNT
Ezekiel 6 in the MNT2
Ezekiel 6 in the MRS1T
Ezekiel 6 in the NAA
Ezekiel 6 in the NASB
Ezekiel 6 in the NBLA
Ezekiel 6 in the NBS
Ezekiel 6 in the NBVTP
Ezekiel 6 in the NET2
Ezekiel 6 in the NIV11
Ezekiel 6 in the NNT
Ezekiel 6 in the NNT2
Ezekiel 6 in the NNT3
Ezekiel 6 in the PDDPT
Ezekiel 6 in the PFNT
Ezekiel 6 in the RMNT
Ezekiel 6 in the SBIAS
Ezekiel 6 in the SBIBS
Ezekiel 6 in the SBIBS2
Ezekiel 6 in the SBICS
Ezekiel 6 in the SBIDS
Ezekiel 6 in the SBIGS
Ezekiel 6 in the SBIHS
Ezekiel 6 in the SBIIS
Ezekiel 6 in the SBIIS2
Ezekiel 6 in the SBIIS3
Ezekiel 6 in the SBIKS
Ezekiel 6 in the SBIKS2
Ezekiel 6 in the SBIMS
Ezekiel 6 in the SBIOS
Ezekiel 6 in the SBIPS
Ezekiel 6 in the SBISS
Ezekiel 6 in the SBITS
Ezekiel 6 in the SBITS2
Ezekiel 6 in the SBITS3
Ezekiel 6 in the SBITS4
Ezekiel 6 in the SBIUS
Ezekiel 6 in the SBIVS
Ezekiel 6 in the SBT
Ezekiel 6 in the SBT1E
Ezekiel 6 in the SCHL
Ezekiel 6 in the SNT
Ezekiel 6 in the SUSU
Ezekiel 6 in the SUSU2
Ezekiel 6 in the SYNO
Ezekiel 6 in the TBIAOTANT
Ezekiel 6 in the TBT1E
Ezekiel 6 in the TBT1E2
Ezekiel 6 in the TFTIP
Ezekiel 6 in the TFTU
Ezekiel 6 in the TGNTATF3T
Ezekiel 6 in the THAI
Ezekiel 6 in the TNFD
Ezekiel 6 in the TNT
Ezekiel 6 in the TNTIK
Ezekiel 6 in the TNTIL
Ezekiel 6 in the TNTIN
Ezekiel 6 in the TNTIP
Ezekiel 6 in the TNTIZ
Ezekiel 6 in the TOMA
Ezekiel 6 in the TTENT
Ezekiel 6 in the UBG
Ezekiel 6 in the UGV
Ezekiel 6 in the UGV2
Ezekiel 6 in the UGV3
Ezekiel 6 in the VBL
Ezekiel 6 in the VDCC
Ezekiel 6 in the YALU
Ezekiel 6 in the YAPE
Ezekiel 6 in the YBVTP
Ezekiel 6 in the ZBP