Amos 7 (BOKCV)

1 Hili ndilo alilonionyesha BWANA Mwenyezi katika maono: Alikuwa anaandaa makundi ya nzige baada ya kuvunwa fungu la mfalme na wakati ule tu mimea ya pili ilipokuwa ikichipua. 2 Wakati nzige walikuwa wamekula mimea yote ya nchi, nililia kwa sauti kuu, “BWANA Mwenyezi, samehe! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!” 3 Kwa hiyo BWANA akaghairi.Kisha BWANA akasema, “Hili halitatokea.” 4 Hili ndilo BWANA Mwenyezi alilonionyesha katika maono: BWANA Mwenyezi alikuwa akiita hukumu ya moto; nao ulikausha vilindi vikuu, ukateketeza nchi. 5 Ndipo nikalia, “BWANA Mwenyezi, nakusihi, zuia! Je, Yakobo atawezaje kuendelea kuishi? Yeye ni mdogo sana!” 6 Kwa hiyo BWANA akaghairi. BWANA Mwenyezi akasema, “Hili nalo halitatokea.” 7 Hili ndilo alilonionyesha katika maono: Bwana alikuwa amesimama karibu na ukuta ambao ulikuwa umejengwa kwa timazi, akiwa na uzi wa timazi mkononi mwake. 8 Naye BWANA akaniuliza, “Je, Amosi unaona nini?”Nikamjibu, “Uzi wa timazi.”Kisha Bwana akasema, “Tazama, ninaweka uzi wa timazi miongoni mwa watu wangu Israeli; sitawahurumia tena. 9 “Mahali pa Isaki pa juu pa kuabudia miungu pataangamizwa,na mahali patakatifu pa Israeli pa kuabudia pataharibiwa;kwa upanga wangu nitainukadhidi ya nyumba ya Yeroboamu.” 10 Kisha Amazia kuhani wa Betheli akatuma ujumbe kwa Yeroboamu mfalme wa Israeli, akisema: “Amosi analeta fitina juu yako katikati ya Israeli. Nchi haiwezi kuvumilia maneno yake yote. 11 Kwa kuwa hili ndilo Amosi analosema:“ ‘Yeroboamu atakufa kwa upanga,na kwa hakika Israeli watakwenda uhamishoni,mbali na nchi yao.’ ” 12 Kisha Amazia akamwambia Amosi, “Nenda zako, ewe mwonaji! Urudi katika nchi ya Yuda. Ujipatie riziki yako huko na kutoa unabii wako. 13 Usiendelee kutoa unabii katika Betheli, kwa sababu hapa ni mahali pa mfalme pa kuabudia na Hekalu la ufalme huu.” 14 Amosi akamjibu Amazia, “Mimi sikuwa nabii wala mwana wa nabii, lakini nilikuwa mchungaji wa kondoo na mtunza mikuyu. 15 Lakini BWANA akanitoa kutoka kuchunga kondoo na kuniambia, ‘Nenda, ukawatabirie watu wangu Israeli.’ 16 Sasa basi, sikieni neno la BWANA. Ninyi mnasema,“ ‘Usitabiri dhidi ya Israeli,na uache kuhubiri dhidi ya nyumba ya Isaki.’ 17 “Kwa hiyo hili ndilo asemalo BWANA:“ ‘Mke wako atakuwa kahaba mjini,nao wana wako na binti zako watauawa kwa upanga.Shamba lako litapimwa na kugawanywa,na wewe mwenyewe utafia katika nchi ya kipagani.Nayo Israeli kwa hakika itakwenda uhamishoni,mbali na nchi yao.’ ”

In Other Versions

Amos 7 in the ANGEFD

Amos 7 in the ANTPNG2D

Amos 7 in the AS21

Amos 7 in the BAGH

Amos 7 in the BBPNG

Amos 7 in the BBT1E

Amos 7 in the BDS

Amos 7 in the BEV

Amos 7 in the BHAD

Amos 7 in the BIB

Amos 7 in the BLPT

Amos 7 in the BNT

Amos 7 in the BNTABOOT

Amos 7 in the BNTLV

Amos 7 in the BOATCB

Amos 7 in the BOATCB2

Amos 7 in the BOBCV

Amos 7 in the BOCNT

Amos 7 in the BOECS

Amos 7 in the BOGWICC

Amos 7 in the BOHCB

Amos 7 in the BOHCV

Amos 7 in the BOHLNT

Amos 7 in the BOHNTLTAL

Amos 7 in the BOICB

Amos 7 in the BOILNTAP

Amos 7 in the BOITCV

Amos 7 in the BOKCV2

Amos 7 in the BOKHWOG

Amos 7 in the BOKSSV

Amos 7 in the BOLCB

Amos 7 in the BOLCB2

Amos 7 in the BOMCV

Amos 7 in the BONAV

Amos 7 in the BONCB

Amos 7 in the BONLT

Amos 7 in the BONUT2

Amos 7 in the BOPLNT

Amos 7 in the BOSCB

Amos 7 in the BOSNC

Amos 7 in the BOTLNT

Amos 7 in the BOVCB

Amos 7 in the BOYCB

Amos 7 in the BPBB

Amos 7 in the BPH

Amos 7 in the BSB

Amos 7 in the CCB

Amos 7 in the CUV

Amos 7 in the CUVS

Amos 7 in the DBT

Amos 7 in the DGDNT

Amos 7 in the DHNT

Amos 7 in the DNT

Amos 7 in the ELBE

Amos 7 in the EMTV

Amos 7 in the ESV

Amos 7 in the FBV

Amos 7 in the FEB

Amos 7 in the GGMNT

Amos 7 in the GNT

Amos 7 in the HARY

Amos 7 in the HNT

Amos 7 in the IRVA

Amos 7 in the IRVB

Amos 7 in the IRVG

Amos 7 in the IRVH

Amos 7 in the IRVK

Amos 7 in the IRVM

Amos 7 in the IRVM2

Amos 7 in the IRVO

Amos 7 in the IRVP

Amos 7 in the IRVT

Amos 7 in the IRVT2

Amos 7 in the IRVU

Amos 7 in the ISVN

Amos 7 in the JSNT

Amos 7 in the KAPI

Amos 7 in the KBT1ETNIK

Amos 7 in the KBV

Amos 7 in the KJV

Amos 7 in the KNFD

Amos 7 in the LBA

Amos 7 in the LBLA

Amos 7 in the LNT

Amos 7 in the LSV

Amos 7 in the MAAL

Amos 7 in the MBV

Amos 7 in the MBV2

Amos 7 in the MHNT

Amos 7 in the MKNFD

Amos 7 in the MNG

Amos 7 in the MNT

Amos 7 in the MNT2

Amos 7 in the MRS1T

Amos 7 in the NAA

Amos 7 in the NASB

Amos 7 in the NBLA

Amos 7 in the NBS

Amos 7 in the NBVTP

Amos 7 in the NET2

Amos 7 in the NIV11

Amos 7 in the NNT

Amos 7 in the NNT2

Amos 7 in the NNT3

Amos 7 in the PDDPT

Amos 7 in the PFNT

Amos 7 in the RMNT

Amos 7 in the SBIAS

Amos 7 in the SBIBS

Amos 7 in the SBIBS2

Amos 7 in the SBICS

Amos 7 in the SBIDS

Amos 7 in the SBIGS

Amos 7 in the SBIHS

Amos 7 in the SBIIS

Amos 7 in the SBIIS2

Amos 7 in the SBIIS3

Amos 7 in the SBIKS

Amos 7 in the SBIKS2

Amos 7 in the SBIMS

Amos 7 in the SBIOS

Amos 7 in the SBIPS

Amos 7 in the SBISS

Amos 7 in the SBITS

Amos 7 in the SBITS2

Amos 7 in the SBITS3

Amos 7 in the SBITS4

Amos 7 in the SBIUS

Amos 7 in the SBIVS

Amos 7 in the SBT

Amos 7 in the SBT1E

Amos 7 in the SCHL

Amos 7 in the SNT

Amos 7 in the SUSU

Amos 7 in the SUSU2

Amos 7 in the SYNO

Amos 7 in the TBIAOTANT

Amos 7 in the TBT1E

Amos 7 in the TBT1E2

Amos 7 in the TFTIP

Amos 7 in the TFTU

Amos 7 in the TGNTATF3T

Amos 7 in the THAI

Amos 7 in the TNFD

Amos 7 in the TNT

Amos 7 in the TNTIK

Amos 7 in the TNTIL

Amos 7 in the TNTIN

Amos 7 in the TNTIP

Amos 7 in the TNTIZ

Amos 7 in the TOMA

Amos 7 in the TTENT

Amos 7 in the UBG

Amos 7 in the UGV

Amos 7 in the UGV2

Amos 7 in the UGV3

Amos 7 in the VBL

Amos 7 in the VDCC

Amos 7 in the YALU

Amos 7 in the YAPE

Amos 7 in the YBVTP

Amos 7 in the ZBP