Jeremiah 11 (BOKCV)

1 Hili ndilo neno lililomjia Yeremia kutoka kwa BWANA: 2 “Sikia maneno ya agano hili, nawe uwaambie watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu. 3 Waambie kwamba hili ndilo asemalo BWANA, Mungu wa Israeli: ‘Amelaaniwa mtu ambaye hatayatii maneno ya agano hili, 4 maneno niliyowaamuru baba zenu nilipowatoa katika nchi ya Misri, kutoka tanuru la kuyeyushia vyuma.’ Nilisema, ‘Nitiini mimi na mfanye kila kitu ninachowaamuru, nanyi mtakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu. 5 Kisha nitatimiza kiapo nilichowaapia baba zenu, kuwapa nchi itiririkayo maziwa na asali,’ nchi ambayo mnaimiliki leo.”Nikajibu, “Amen, BWANA.” 6 BWANA akaniambia, “Tangaza maneno haya yote katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu: ‘Sikilizeni maneno ya agano hili na kuyafuata. 7 Tangu wakati ule niliwapandisha baba zenu kutoka Misri mpaka leo, niliwaonya tena na tena, nikisema “Nitiini mimi.” 8 Lakini hawakusikiliza wala kujali. Badala yake, walifuata ukaidi wa mioyo yao miovu. Hivyo nikaleta juu yao laana zote za agano nililokuwa nimewaamuru wao kulifuata, lakini wao hawakulishika.’ ” 9 Kisha BWANA akaniambia, “Kuna shauri baya linaloendelea miongoni mwa watu wa Yuda na wale wanaoishi Yerusalemu. 10 Wamerudia dhambi za baba zao, waliokataa kusikiliza maneno yangu. Wameifuata miungu mingine kuitumikia. Nyumba zote mbili za Israeli na Yuda zimelivunja agano nililofanya na baba zao. 11 Kwa hivyo, hili ndilo asemalo BWANA: ‘Nitaleta juu yao maafa ambayo hawawezi kuyakimbia. Hata kama wakinililia, sitawasikiliza. 12 Miji ya Yuda na watu wa Yerusalemu watakwenda kuililia miungu ambayo wameifukizia uvumba, lakini haitawasaidia kamwe wakati maafa yatakapowapiga. 13 Mnayo miungu mingi kama miji mliyo nayo, ee Yuda, nazo madhabahu mlizozijenga za kufukizia uvumba huyo mungu wa aibu Baali ni nyingi kama barabara za Yerusalemu.’ 14 “Wewe usiwaombee watu hawa wala kufanya maombezi yoyote au kunisihi kwa ajili yao, kwa sababu sitawasikiliza watakaponiita wakati wa taabu yao. 15 “Mpenzi wangu anafanya nini hekaluni mwangu,anapofanya mashauri yake maovu na wengi?Je, nyama iliyowekwa wakfu yawezakuondolea mbali adhabu yako?Unapojiingiza katika ubaya wako,ndipo unashangilia.” 16 BWANA alikuita mti wa mzeituni uliostawiulio na matunda mazuri kwa sura.Lakini kwa ngurumo ya mawimbi makuuatautia moto,nayo matawi yake yatavunjika. 17 BWANA Mwenye Nguvu Zote, aliyekupanda, ametamka maafa kwa ajili yako, kwa sababu nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda mmefanya maovu na kunikasirisha kwa kumfukizia Baali uvumba. 18 Kwa sababu BWANA alinifunulia hila zao mbaya, nilizifahamu, kwa kuwa wakati ule alinionyesha yale waliyokuwa wanayafanya. 19 Nilikuwa kama mwana-kondoo mpole aliyeongozwa machinjoni; mimi sikutambua kwamba walikuwa wamefanya shauri baya dhidi yangu, wakisema,“Sisi na tuuangamize mti na matunda yake;nasi tumkatilie mbali kutoka nchi ya walio hai,ili jina lake lisikumbukwe tena.” 20 Lakini, Ee BWANA Mwenye Nguvu Zote, wewe uhukumuye kwa haki,nawe uchunguzaye moyo na akili,wacha nione ukiwalipiza wao kisasi,kwa maana kwako nimeweka shauri langu. 21 “Kwa hiyo hili ndilo BWANA asemalo kuhusu watu wa Anathothi wale wanaotafuta uhai wako wakisema, ‘Usitoe unabii kwa jina la BWANA, la sivyo utakufa kwa mikono yetu’: 22 kwa hiyo hili ndilo BWANA Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nitawaadhibu. Vijana wao waume watakufa kwa upanga, wana wao na binti zao kwa njaa. 23 Hawatasaziwa hata mabaki kwao, kwa sababu nitaleta maafa kwa watu wa Anathothi katika mwaka wa adhabu yao.’ ”

In Other Versions

Jeremiah 11 in the ANGEFD

Jeremiah 11 in the ANTPNG2D

Jeremiah 11 in the AS21

Jeremiah 11 in the BAGH

Jeremiah 11 in the BBPNG

Jeremiah 11 in the BBT1E

Jeremiah 11 in the BDS

Jeremiah 11 in the BEV

Jeremiah 11 in the BHAD

Jeremiah 11 in the BIB

Jeremiah 11 in the BLPT

Jeremiah 11 in the BNT

Jeremiah 11 in the BNTABOOT

Jeremiah 11 in the BNTLV

Jeremiah 11 in the BOATCB

Jeremiah 11 in the BOATCB2

Jeremiah 11 in the BOBCV

Jeremiah 11 in the BOCNT

Jeremiah 11 in the BOECS

Jeremiah 11 in the BOGWICC

Jeremiah 11 in the BOHCB

Jeremiah 11 in the BOHCV

Jeremiah 11 in the BOHLNT

Jeremiah 11 in the BOHNTLTAL

Jeremiah 11 in the BOICB

Jeremiah 11 in the BOILNTAP

Jeremiah 11 in the BOITCV

Jeremiah 11 in the BOKCV2

Jeremiah 11 in the BOKHWOG

Jeremiah 11 in the BOKSSV

Jeremiah 11 in the BOLCB

Jeremiah 11 in the BOLCB2

Jeremiah 11 in the BOMCV

Jeremiah 11 in the BONAV

Jeremiah 11 in the BONCB

Jeremiah 11 in the BONLT

Jeremiah 11 in the BONUT2

Jeremiah 11 in the BOPLNT

Jeremiah 11 in the BOSCB

Jeremiah 11 in the BOSNC

Jeremiah 11 in the BOTLNT

Jeremiah 11 in the BOVCB

Jeremiah 11 in the BOYCB

Jeremiah 11 in the BPBB

Jeremiah 11 in the BPH

Jeremiah 11 in the BSB

Jeremiah 11 in the CCB

Jeremiah 11 in the CUV

Jeremiah 11 in the CUVS

Jeremiah 11 in the DBT

Jeremiah 11 in the DGDNT

Jeremiah 11 in the DHNT

Jeremiah 11 in the DNT

Jeremiah 11 in the ELBE

Jeremiah 11 in the EMTV

Jeremiah 11 in the ESV

Jeremiah 11 in the FBV

Jeremiah 11 in the FEB

Jeremiah 11 in the GGMNT

Jeremiah 11 in the GNT

Jeremiah 11 in the HARY

Jeremiah 11 in the HNT

Jeremiah 11 in the IRVA

Jeremiah 11 in the IRVB

Jeremiah 11 in the IRVG

Jeremiah 11 in the IRVH

Jeremiah 11 in the IRVK

Jeremiah 11 in the IRVM

Jeremiah 11 in the IRVM2

Jeremiah 11 in the IRVO

Jeremiah 11 in the IRVP

Jeremiah 11 in the IRVT

Jeremiah 11 in the IRVT2

Jeremiah 11 in the IRVU

Jeremiah 11 in the ISVN

Jeremiah 11 in the JSNT

Jeremiah 11 in the KAPI

Jeremiah 11 in the KBT1ETNIK

Jeremiah 11 in the KBV

Jeremiah 11 in the KJV

Jeremiah 11 in the KNFD

Jeremiah 11 in the LBA

Jeremiah 11 in the LBLA

Jeremiah 11 in the LNT

Jeremiah 11 in the LSV

Jeremiah 11 in the MAAL

Jeremiah 11 in the MBV

Jeremiah 11 in the MBV2

Jeremiah 11 in the MHNT

Jeremiah 11 in the MKNFD

Jeremiah 11 in the MNG

Jeremiah 11 in the MNT

Jeremiah 11 in the MNT2

Jeremiah 11 in the MRS1T

Jeremiah 11 in the NAA

Jeremiah 11 in the NASB

Jeremiah 11 in the NBLA

Jeremiah 11 in the NBS

Jeremiah 11 in the NBVTP

Jeremiah 11 in the NET2

Jeremiah 11 in the NIV11

Jeremiah 11 in the NNT

Jeremiah 11 in the NNT2

Jeremiah 11 in the NNT3

Jeremiah 11 in the PDDPT

Jeremiah 11 in the PFNT

Jeremiah 11 in the RMNT

Jeremiah 11 in the SBIAS

Jeremiah 11 in the SBIBS

Jeremiah 11 in the SBIBS2

Jeremiah 11 in the SBICS

Jeremiah 11 in the SBIDS

Jeremiah 11 in the SBIGS

Jeremiah 11 in the SBIHS

Jeremiah 11 in the SBIIS

Jeremiah 11 in the SBIIS2

Jeremiah 11 in the SBIIS3

Jeremiah 11 in the SBIKS

Jeremiah 11 in the SBIKS2

Jeremiah 11 in the SBIMS

Jeremiah 11 in the SBIOS

Jeremiah 11 in the SBIPS

Jeremiah 11 in the SBISS

Jeremiah 11 in the SBITS

Jeremiah 11 in the SBITS2

Jeremiah 11 in the SBITS3

Jeremiah 11 in the SBITS4

Jeremiah 11 in the SBIUS

Jeremiah 11 in the SBIVS

Jeremiah 11 in the SBT

Jeremiah 11 in the SBT1E

Jeremiah 11 in the SCHL

Jeremiah 11 in the SNT

Jeremiah 11 in the SUSU

Jeremiah 11 in the SUSU2

Jeremiah 11 in the SYNO

Jeremiah 11 in the TBIAOTANT

Jeremiah 11 in the TBT1E

Jeremiah 11 in the TBT1E2

Jeremiah 11 in the TFTIP

Jeremiah 11 in the TFTU

Jeremiah 11 in the TGNTATF3T

Jeremiah 11 in the THAI

Jeremiah 11 in the TNFD

Jeremiah 11 in the TNT

Jeremiah 11 in the TNTIK

Jeremiah 11 in the TNTIL

Jeremiah 11 in the TNTIN

Jeremiah 11 in the TNTIP

Jeremiah 11 in the TNTIZ

Jeremiah 11 in the TOMA

Jeremiah 11 in the TTENT

Jeremiah 11 in the UBG

Jeremiah 11 in the UGV

Jeremiah 11 in the UGV2

Jeremiah 11 in the UGV3

Jeremiah 11 in the VBL

Jeremiah 11 in the VDCC

Jeremiah 11 in the YALU

Jeremiah 11 in the YAPE

Jeremiah 11 in the YBVTP

Jeremiah 11 in the ZBP