Genesis 48 (BOKCV)

1 Baada ya muda Yosefu akaambiwa kwamba, “Baba yako ni mgonjwa.” Kwa hiyo akawachukua wanawe wawili Manase na Efraimu, pamoja naye. 2 Yakobo alipoambiwa, “Mwanao Yosefu amekujia kukuona,” Israeli akakusanya nguvu zake, akaketi kitandani. 3 Yakobo akamwambia Yosefu, “Mungu Mwenyezi alinitokea huko Luzu katika nchi ya Kanaani, huko akanibariki, 4 naye akaniambia, ‘Nitakufanya ustawi na kuongezeka hesabu yako, nitakufanya kuwa jamii ya mataifa, nami nitakupa nchi hii uimiliki milele wewe na wazao wako baada yako.’ 5 “Sasa basi, wanao wawili waliozaliwa kwako huku Misri kabla sijaja hapa kwako watahesabiwa kuwa ni wangu; Efraimu na Manase watakuwa wangu, kama vile Reubeni na Simeoni walivyo wangu. 6 Lakini watoto utakaowazaa baada yao watakuwa wako. Katika nchi watakayoirithi, watatambuliwa kwa jina la ndugu zao. 7 Nilipokuwa ninarudi kutoka Padani, katika huzuni yangu Raheli alifariki katika nchi ya Kanaani tulipokuwa tungali tukisafiri, tukiwa karibu kufika Efrathi. Kwa hiyo nilimzika huko, kando ya njia iendayo Efrathi” (yaani Bethlehemu). 8 Wakati Israeli alipowaona wana wa Yosefu, akauliza, “Hawa ni nani?” 9 Yosefu akamjibu baba yake, “Hawa ni wana ambao Mungu amenipa nikiwa huku.”Ndipo Israeli akasema, “Walete kwangu ili niwabariki.” 10 Basi macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee, naye aliona kwa shida. Kwa hiyo Yosefu akawaleta wanawe karibu na baba yake, Israeli akawabusu na akawakumbatia. 11 Israeli akamwambia Yosefu, “Kamwe sikutazamia kuuona uso wako tena, lakini sasa Mungu ameniruhusu kuwaona watoto wako pia.” 12 Ndipo Yosefu akawaondoa wanawe magotini mwa Israeli naye akasujudu hadi nchi. 13 Yosefu akachukua wale wana wawili, Efraimu kwenye mkono wake wa kuume akimwelekeza kwenye mkono wa kushoto wa Israeli, na Manase katika mkono wake wa kushoto akimwelekeza kwenye mkono wa kuume wa Israeli, akawaleta karibu na babu yao. 14 Lakini Israeli akaupeleka mkono wake wa kuume, akauweka juu ya kichwa cha Efraimu, ingawa alikuwa ndiye mdogo, na mkono wake wa kushoto akaukatisha, akauweka juu ya kichwa cha Manase, ingawa Manase alikuwa ndiye mzaliwa wa kwanza. 15 Ndipo akambariki Yosefu akisema,“Mungu ambaye baba zanguAbrahamu na Isaki walimtii,Mungu ambaye amekuwa mchungajiwa maisha yangu yote mpaka leo hii, 16 Malaika ambaye aliniokoa kutoka madhara yote,yeye na awabariki vijana hawa.Na waitwe kwa jina languna kwa majina ya baba zangu Abrahamu na Isaki,wao na waongezeke kwa wingikatika dunia.” 17 Yosefu alipoona baba yake akiweka mkono wa kuume juu ya kichwa cha Efraimu, hakupendezwa, kwa hiyo akauchukua mkono wa baba yake kutoka kichwa cha Efraimu na kuuweka juu ya kichwa cha Manase. 18 Yosefu akamwambia, “Hapana, baba yangu, huyu ndiye mzaliwa wa kwanza; uweke mkono wako wa kuume juu ya kichwa chake.” 19 Lakini baba yake akakataa, akasema, “Ninajua, mwanangu, ninajua. Yeye pia atakuwa taifa, naye pia atakuwa mkuu. Hata hivyo, ndugu yake mdogo atakuwa mkuu kuliko yeye, nao wazao wake watakuwa kundi la mataifa.” 20 Akawabarikia siku ile na kusema,“Kwa jina lenu Israeli watatamka baraka hii:‘Mungu na awafanye kama Efraimu na Manase.’ ”Kwa hiyo akamtanguliza Efraimu mbele ya Manase. 21 Ndipo Israeli akamwambia Yosefu, “Mimi ninakaribia kufa, lakini Mungu atakuwa pamoja nanyi, na atawarudisha katika nchi ya baba zenu. 22 Kwako wewe, kama aliye juu ya ndugu zako, ninakupa sehemu moja zaidi ya ndugu zako, lile eneo nililoteka kwa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.”

In Other Versions

Genesis 48 in the ANGEFD

Genesis 48 in the ANTPNG2D

Genesis 48 in the AS21

Genesis 48 in the BAGH

Genesis 48 in the BBPNG

Genesis 48 in the BBT1E

Genesis 48 in the BDS

Genesis 48 in the BEV

Genesis 48 in the BHAD

Genesis 48 in the BIB

Genesis 48 in the BLPT

Genesis 48 in the BNT

Genesis 48 in the BNTABOOT

Genesis 48 in the BNTLV

Genesis 48 in the BOATCB

Genesis 48 in the BOATCB2

Genesis 48 in the BOBCV

Genesis 48 in the BOCNT

Genesis 48 in the BOECS

Genesis 48 in the BOGWICC

Genesis 48 in the BOHCB

Genesis 48 in the BOHCV

Genesis 48 in the BOHLNT

Genesis 48 in the BOHNTLTAL

Genesis 48 in the BOICB

Genesis 48 in the BOILNTAP

Genesis 48 in the BOITCV

Genesis 48 in the BOKCV2

Genesis 48 in the BOKHWOG

Genesis 48 in the BOKSSV

Genesis 48 in the BOLCB

Genesis 48 in the BOLCB2

Genesis 48 in the BOMCV

Genesis 48 in the BONAV

Genesis 48 in the BONCB

Genesis 48 in the BONLT

Genesis 48 in the BONUT2

Genesis 48 in the BOPLNT

Genesis 48 in the BOSCB

Genesis 48 in the BOSNC

Genesis 48 in the BOTLNT

Genesis 48 in the BOVCB

Genesis 48 in the BOYCB

Genesis 48 in the BPBB

Genesis 48 in the BPH

Genesis 48 in the BSB

Genesis 48 in the CCB

Genesis 48 in the CUV

Genesis 48 in the CUVS

Genesis 48 in the DBT

Genesis 48 in the DGDNT

Genesis 48 in the DHNT

Genesis 48 in the DNT

Genesis 48 in the ELBE

Genesis 48 in the EMTV

Genesis 48 in the ESV

Genesis 48 in the FBV

Genesis 48 in the FEB

Genesis 48 in the GGMNT

Genesis 48 in the GNT

Genesis 48 in the HARY

Genesis 48 in the HNT

Genesis 48 in the IRVA

Genesis 48 in the IRVB

Genesis 48 in the IRVG

Genesis 48 in the IRVH

Genesis 48 in the IRVK

Genesis 48 in the IRVM

Genesis 48 in the IRVM2

Genesis 48 in the IRVO

Genesis 48 in the IRVP

Genesis 48 in the IRVT

Genesis 48 in the IRVT2

Genesis 48 in the IRVU

Genesis 48 in the ISVN

Genesis 48 in the JSNT

Genesis 48 in the KAPI

Genesis 48 in the KBT1ETNIK

Genesis 48 in the KBV

Genesis 48 in the KJV

Genesis 48 in the KNFD

Genesis 48 in the LBA

Genesis 48 in the LBLA

Genesis 48 in the LNT

Genesis 48 in the LSV

Genesis 48 in the MAAL

Genesis 48 in the MBV

Genesis 48 in the MBV2

Genesis 48 in the MHNT

Genesis 48 in the MKNFD

Genesis 48 in the MNG

Genesis 48 in the MNT

Genesis 48 in the MNT2

Genesis 48 in the MRS1T

Genesis 48 in the NAA

Genesis 48 in the NASB

Genesis 48 in the NBLA

Genesis 48 in the NBS

Genesis 48 in the NBVTP

Genesis 48 in the NET2

Genesis 48 in the NIV11

Genesis 48 in the NNT

Genesis 48 in the NNT2

Genesis 48 in the NNT3

Genesis 48 in the PDDPT

Genesis 48 in the PFNT

Genesis 48 in the RMNT

Genesis 48 in the SBIAS

Genesis 48 in the SBIBS

Genesis 48 in the SBIBS2

Genesis 48 in the SBICS

Genesis 48 in the SBIDS

Genesis 48 in the SBIGS

Genesis 48 in the SBIHS

Genesis 48 in the SBIIS

Genesis 48 in the SBIIS2

Genesis 48 in the SBIIS3

Genesis 48 in the SBIKS

Genesis 48 in the SBIKS2

Genesis 48 in the SBIMS

Genesis 48 in the SBIOS

Genesis 48 in the SBIPS

Genesis 48 in the SBISS

Genesis 48 in the SBITS

Genesis 48 in the SBITS2

Genesis 48 in the SBITS3

Genesis 48 in the SBITS4

Genesis 48 in the SBIUS

Genesis 48 in the SBIVS

Genesis 48 in the SBT

Genesis 48 in the SBT1E

Genesis 48 in the SCHL

Genesis 48 in the SNT

Genesis 48 in the SUSU

Genesis 48 in the SUSU2

Genesis 48 in the SYNO

Genesis 48 in the TBIAOTANT

Genesis 48 in the TBT1E

Genesis 48 in the TBT1E2

Genesis 48 in the TFTIP

Genesis 48 in the TFTU

Genesis 48 in the TGNTATF3T

Genesis 48 in the THAI

Genesis 48 in the TNFD

Genesis 48 in the TNT

Genesis 48 in the TNTIK

Genesis 48 in the TNTIL

Genesis 48 in the TNTIN

Genesis 48 in the TNTIP

Genesis 48 in the TNTIZ

Genesis 48 in the TOMA

Genesis 48 in the TTENT

Genesis 48 in the UBG

Genesis 48 in the UGV

Genesis 48 in the UGV2

Genesis 48 in the UGV3

Genesis 48 in the VBL

Genesis 48 in the VDCC

Genesis 48 in the YALU

Genesis 48 in the YAPE

Genesis 48 in the YBVTP

Genesis 48 in the ZBP