2 Corinthians 8 (BOKCV)

1 Basi sasa ndugu, nataka ninyi mjue kuhusu ile neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia. 2 Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha waliyokuwa nayo ilikuwa kubwa, ingawa walikuwa maskini kupindukia, kwa upande wao walifurika kwa wingi wa ukarimu. 3 Kwa maana nashuhudia kwamba wao walitoa kwa kadiri wawezavyo, hata na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe, 4 wakitusihi kwa bidii wapewe fursa ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watakatifu. 5 Wala hawakufanya tulivyotazamia, bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwa ajili yetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu. 6 Kwa hiyo tulimsihi Tito, kwa kuwa ndiye alianzisha jambo hili, akamilishe tendo hili la neema kwa upande wenu. 7 Lakini kama vile mlivyo mbele sana katika yote: Katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika uaminifu wote na katika upendo wenu kwetu sisi, vivyo hivyo tunataka pia mzidi katika neema hii ya kutoa. 8 Siwaamrishi, lakini nataka kujaribu unyofu wa upendo wenu kwa kuulinganisha na bidii ya wengine. 9 Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri. 10 Ushauri wangu kuhusu lile lililo bora kwenu juu ya jambo hili ni huu: Mwaka uliopita ninyi mlikuwa wa kwanza si tu kutoa lakini pia mlikuwa na shauku ya kufanya hivyo. 11 Sasa ikamilisheni kazi hii kwa shauku kama mlivyoanza, jitoleeni kulingana na uwezo wenu. 12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kulingana na kile mtu alicho nacho, wala si kwa kile ambacho hana. 13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka, bali pawe na uwiano. 14 Kwa wakati huu, wingi wa vitu mlivyo navyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao watakapokuwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu. 15 Ndipo patakuwa na usawa, kama ilivyoandikwa: “Aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.” 16 Ninamshukuru Mungu ambaye amemtia Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali. 17 Si kwamba Tito amekubali tu ombi letu, bali anakuja kwenu akiwa na shauku kuliko wakati mwingine, tena kwa hiari yake mwenyewe. 18 Nasi tunamtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili. 19 Zaidi ya hayo, alichaguliwa na makanisa ili asafiri pamoja nasi tulipokuwa tunapeleka matoleo ya ukarimu, kwa ajili ya utukufu wa Bwana mwenyewe, na ili kuonyesha hisani yetu kuwasaidia. 20 Tunataka kuepuka lawama yoyote kuhusu jinsi tunavyosimamia matoleo haya ya ukarimu. 21 Kwa kuwa tunakusudia kufanya kile kilicho haki si machoni mwa Bwana peke yake, bali pia machoni mwa watu wengine. 22 Pamoja nao, tunamtuma ndugu yetu ambaye mara kwa mara ametuthibitishia kwa njia nyingi kwamba ana shauku, naam, zaidi sana sasa kwa sababu analo tumaini kuu kwenu. 23 Kwa habari ya Tito, yeye ni mwenzangu na mtendakazi pamoja nami miongoni mwenu. Kwa habari za ndugu zetu, wao ni wawakilishi wa makanisa, na utukufu kwa Kristo. 24 Kwa hiyo waonyesheni wazi hawa ndugu uthibitisho wa upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, mbele ya makanisa, ili yapate kuona.

In Other Versions

2 Corinthians 8 in the ANGEFD

2 Corinthians 8 in the ANTPNG2D

2 Corinthians 8 in the AS21

2 Corinthians 8 in the BAGH

2 Corinthians 8 in the BBPNG

2 Corinthians 8 in the BBT1E

2 Corinthians 8 in the BDS

2 Corinthians 8 in the BEV

2 Corinthians 8 in the BHAD

2 Corinthians 8 in the BIB

2 Corinthians 8 in the BLPT

2 Corinthians 8 in the BNT

2 Corinthians 8 in the BNTABOOT

2 Corinthians 8 in the BNTLV

2 Corinthians 8 in the BOATCB

2 Corinthians 8 in the BOATCB2

2 Corinthians 8 in the BOBCV

2 Corinthians 8 in the BOCNT

2 Corinthians 8 in the BOECS

2 Corinthians 8 in the BOGWICC

2 Corinthians 8 in the BOHCB

2 Corinthians 8 in the BOHCV

2 Corinthians 8 in the BOHLNT

2 Corinthians 8 in the BOHNTLTAL

2 Corinthians 8 in the BOICB

2 Corinthians 8 in the BOILNTAP

2 Corinthians 8 in the BOITCV

2 Corinthians 8 in the BOKCV2

2 Corinthians 8 in the BOKHWOG

2 Corinthians 8 in the BOKSSV

2 Corinthians 8 in the BOLCB

2 Corinthians 8 in the BOLCB2

2 Corinthians 8 in the BOMCV

2 Corinthians 8 in the BONAV

2 Corinthians 8 in the BONCB

2 Corinthians 8 in the BONLT

2 Corinthians 8 in the BONUT2

2 Corinthians 8 in the BOPLNT

2 Corinthians 8 in the BOSCB

2 Corinthians 8 in the BOSNC

2 Corinthians 8 in the BOTLNT

2 Corinthians 8 in the BOVCB

2 Corinthians 8 in the BOYCB

2 Corinthians 8 in the BPBB

2 Corinthians 8 in the BPH

2 Corinthians 8 in the BSB

2 Corinthians 8 in the CCB

2 Corinthians 8 in the CUV

2 Corinthians 8 in the CUVS

2 Corinthians 8 in the DBT

2 Corinthians 8 in the DGDNT

2 Corinthians 8 in the DHNT

2 Corinthians 8 in the DNT

2 Corinthians 8 in the ELBE

2 Corinthians 8 in the EMTV

2 Corinthians 8 in the ESV

2 Corinthians 8 in the FBV

2 Corinthians 8 in the FEB

2 Corinthians 8 in the GGMNT

2 Corinthians 8 in the GNT

2 Corinthians 8 in the HARY

2 Corinthians 8 in the HNT

2 Corinthians 8 in the IRVA

2 Corinthians 8 in the IRVB

2 Corinthians 8 in the IRVG

2 Corinthians 8 in the IRVH

2 Corinthians 8 in the IRVK

2 Corinthians 8 in the IRVM

2 Corinthians 8 in the IRVM2

2 Corinthians 8 in the IRVO

2 Corinthians 8 in the IRVP

2 Corinthians 8 in the IRVT

2 Corinthians 8 in the IRVT2

2 Corinthians 8 in the IRVU

2 Corinthians 8 in the ISVN

2 Corinthians 8 in the JSNT

2 Corinthians 8 in the KAPI

2 Corinthians 8 in the KBT1ETNIK

2 Corinthians 8 in the KBV

2 Corinthians 8 in the KJV

2 Corinthians 8 in the KNFD

2 Corinthians 8 in the LBA

2 Corinthians 8 in the LBLA

2 Corinthians 8 in the LNT

2 Corinthians 8 in the LSV

2 Corinthians 8 in the MAAL

2 Corinthians 8 in the MBV

2 Corinthians 8 in the MBV2

2 Corinthians 8 in the MHNT

2 Corinthians 8 in the MKNFD

2 Corinthians 8 in the MNG

2 Corinthians 8 in the MNT

2 Corinthians 8 in the MNT2

2 Corinthians 8 in the MRS1T

2 Corinthians 8 in the NAA

2 Corinthians 8 in the NASB

2 Corinthians 8 in the NBLA

2 Corinthians 8 in the NBS

2 Corinthians 8 in the NBVTP

2 Corinthians 8 in the NET2

2 Corinthians 8 in the NIV11

2 Corinthians 8 in the NNT

2 Corinthians 8 in the NNT2

2 Corinthians 8 in the NNT3

2 Corinthians 8 in the PDDPT

2 Corinthians 8 in the PFNT

2 Corinthians 8 in the RMNT

2 Corinthians 8 in the SBIAS

2 Corinthians 8 in the SBIBS

2 Corinthians 8 in the SBIBS2

2 Corinthians 8 in the SBICS

2 Corinthians 8 in the SBIDS

2 Corinthians 8 in the SBIGS

2 Corinthians 8 in the SBIHS

2 Corinthians 8 in the SBIIS

2 Corinthians 8 in the SBIIS2

2 Corinthians 8 in the SBIIS3

2 Corinthians 8 in the SBIKS

2 Corinthians 8 in the SBIKS2

2 Corinthians 8 in the SBIMS

2 Corinthians 8 in the SBIOS

2 Corinthians 8 in the SBIPS

2 Corinthians 8 in the SBISS

2 Corinthians 8 in the SBITS

2 Corinthians 8 in the SBITS2

2 Corinthians 8 in the SBITS3

2 Corinthians 8 in the SBITS4

2 Corinthians 8 in the SBIUS

2 Corinthians 8 in the SBIVS

2 Corinthians 8 in the SBT

2 Corinthians 8 in the SBT1E

2 Corinthians 8 in the SCHL

2 Corinthians 8 in the SNT

2 Corinthians 8 in the SUSU

2 Corinthians 8 in the SUSU2

2 Corinthians 8 in the SYNO

2 Corinthians 8 in the TBIAOTANT

2 Corinthians 8 in the TBT1E

2 Corinthians 8 in the TBT1E2

2 Corinthians 8 in the TFTIP

2 Corinthians 8 in the TFTU

2 Corinthians 8 in the TGNTATF3T

2 Corinthians 8 in the THAI

2 Corinthians 8 in the TNFD

2 Corinthians 8 in the TNT

2 Corinthians 8 in the TNTIK

2 Corinthians 8 in the TNTIL

2 Corinthians 8 in the TNTIN

2 Corinthians 8 in the TNTIP

2 Corinthians 8 in the TNTIZ

2 Corinthians 8 in the TOMA

2 Corinthians 8 in the TTENT

2 Corinthians 8 in the UBG

2 Corinthians 8 in the UGV

2 Corinthians 8 in the UGV2

2 Corinthians 8 in the UGV3

2 Corinthians 8 in the VBL

2 Corinthians 8 in the VDCC

2 Corinthians 8 in the YALU

2 Corinthians 8 in the YAPE

2 Corinthians 8 in the YBVTP

2 Corinthians 8 in the ZBP