Jeremiah 28 (BOKCV)

1 Katika mwezi wa tano wa mwaka ule ule, yaani mwaka wa nne, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia mfalme wa Yuda, nabii Hanania mwana wa Azuri, ambaye alitoka Gibeoni, akaniambia katika nyumba ya BWANA mbele ya makuhani na watu wote: 2 “Hili ndilo BWANA Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli. 3 Katika muda wa miaka miwili nitavirudisha mahali hapa vyombo vyote vya nyumba ya BWANA ambavyo Nebukadneza mfalme wa Babeli aliviondoa kutoka hapa na kuvipeleka Babeli. 4 Pia nitamrudisha mahali hapa Yekonia mwana wa Yehoyakimu mfalme wa Yuda, pamoja na wote waliohamishwa kutoka Yuda ambao walikwenda Babeli,’ asema BWANA, ‘kwa kuwa nitaivunja nira ya mfalme wa Babeli.’ ” 5 Ndipo nabii Yeremia akamjibu nabii Hanania mbele ya makuhani na watu wote waliokuwa wamesimama ndani ya nyumba ya BWANA. 6 Akasema, “Amen! BWANA na afanye hivyo! BWANA na ayatimize maneno uliyotoa unabii kwa kuvirudisha mahali hapa kutoka Babeli vyombo vya nyumba ya BWANA pamoja na wote waliohamishwa. 7 Hata hivyo, nisikilize nikuambie yale nitakayoyasema masikioni mwako na masikioni mwa watu hawa wote: 8 Tangu mwanzo, manabii waliokutangulia wewe na mimi walitabiri vita, maafa na tauni dhidi ya nchi nyingi na falme kubwa. 9 Lakini nabii atakayetabiri amani atatambuliwa kuwa kweli ametumwa na BWANA ikiwa unabii wake utatimia.” 10 Kisha nabii Hanania akaiondoa nira iliyokuwa shingoni mwa Yeremia na kuivunja, 11 naye akasema mbele ya watu wote, “Hili ndilo asemalo BWANA: ‘Vivi hivi ndivyo nitakavyoivunja nira ya Nebukadneza mfalme wa Babeli kutoka kwenye shingo za mataifa katika muda huu wa miaka miwili.’ ” Alipofanya hivi, nabii Yeremia akaondoka zake. 12 Kitambo kidogo baada ya nabii Hanania kuivunja nira kutoka shingo ya nabii Yeremia, neno la BWANA likamjia Yeremia: 13 “Nenda ukamwambie Hanania, ‘Hili ndilo asemalo BWANA: Umevunja nira ya mti, lakini badala yake utapata nira ya chuma. 14 Hili ndilo asemalo BWANA Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli: Nitaweka nira ya chuma kwenye shingo za mataifa haya yote ili kufanya yamtumikie Nebukadneza mfalme wa Babeli, nao watamtumikia. Nitampa kutawala hata wanyama wa mwituni.’ ” 15 Kisha nabii Yeremia akamwambia nabii Hanania, “Sikiliza Hanania! BWANA hajakutuma, lakini wewe umelishawishi taifa hili kuamini uongo. 16 Kwa hiyo, hili ndilo asemalo BWANA: ‘Hivi karibuni nitakuondoa kutoka juu ya uso wa dunia. Mwaka huu utakufa, kwa sababu umetangaza uasi dhidi ya BWANA.’ ” 17 Katika mwezi wa saba wa mwaka ule ule, nabii Hanania akafa.

In Other Versions

Jeremiah 28 in the ANGEFD

Jeremiah 28 in the ANTPNG2D

Jeremiah 28 in the AS21

Jeremiah 28 in the BAGH

Jeremiah 28 in the BBPNG

Jeremiah 28 in the BBT1E

Jeremiah 28 in the BDS

Jeremiah 28 in the BEV

Jeremiah 28 in the BHAD

Jeremiah 28 in the BIB

Jeremiah 28 in the BLPT

Jeremiah 28 in the BNT

Jeremiah 28 in the BNTABOOT

Jeremiah 28 in the BNTLV

Jeremiah 28 in the BOATCB

Jeremiah 28 in the BOATCB2

Jeremiah 28 in the BOBCV

Jeremiah 28 in the BOCNT

Jeremiah 28 in the BOECS

Jeremiah 28 in the BOGWICC

Jeremiah 28 in the BOHCB

Jeremiah 28 in the BOHCV

Jeremiah 28 in the BOHLNT

Jeremiah 28 in the BOHNTLTAL

Jeremiah 28 in the BOICB

Jeremiah 28 in the BOILNTAP

Jeremiah 28 in the BOITCV

Jeremiah 28 in the BOKCV2

Jeremiah 28 in the BOKHWOG

Jeremiah 28 in the BOKSSV

Jeremiah 28 in the BOLCB

Jeremiah 28 in the BOLCB2

Jeremiah 28 in the BOMCV

Jeremiah 28 in the BONAV

Jeremiah 28 in the BONCB

Jeremiah 28 in the BONLT

Jeremiah 28 in the BONUT2

Jeremiah 28 in the BOPLNT

Jeremiah 28 in the BOSCB

Jeremiah 28 in the BOSNC

Jeremiah 28 in the BOTLNT

Jeremiah 28 in the BOVCB

Jeremiah 28 in the BOYCB

Jeremiah 28 in the BPBB

Jeremiah 28 in the BPH

Jeremiah 28 in the BSB

Jeremiah 28 in the CCB

Jeremiah 28 in the CUV

Jeremiah 28 in the CUVS

Jeremiah 28 in the DBT

Jeremiah 28 in the DGDNT

Jeremiah 28 in the DHNT

Jeremiah 28 in the DNT

Jeremiah 28 in the ELBE

Jeremiah 28 in the EMTV

Jeremiah 28 in the ESV

Jeremiah 28 in the FBV

Jeremiah 28 in the FEB

Jeremiah 28 in the GGMNT

Jeremiah 28 in the GNT

Jeremiah 28 in the HARY

Jeremiah 28 in the HNT

Jeremiah 28 in the IRVA

Jeremiah 28 in the IRVB

Jeremiah 28 in the IRVG

Jeremiah 28 in the IRVH

Jeremiah 28 in the IRVK

Jeremiah 28 in the IRVM

Jeremiah 28 in the IRVM2

Jeremiah 28 in the IRVO

Jeremiah 28 in the IRVP

Jeremiah 28 in the IRVT

Jeremiah 28 in the IRVT2

Jeremiah 28 in the IRVU

Jeremiah 28 in the ISVN

Jeremiah 28 in the JSNT

Jeremiah 28 in the KAPI

Jeremiah 28 in the KBT1ETNIK

Jeremiah 28 in the KBV

Jeremiah 28 in the KJV

Jeremiah 28 in the KNFD

Jeremiah 28 in the LBA

Jeremiah 28 in the LBLA

Jeremiah 28 in the LNT

Jeremiah 28 in the LSV

Jeremiah 28 in the MAAL

Jeremiah 28 in the MBV

Jeremiah 28 in the MBV2

Jeremiah 28 in the MHNT

Jeremiah 28 in the MKNFD

Jeremiah 28 in the MNG

Jeremiah 28 in the MNT

Jeremiah 28 in the MNT2

Jeremiah 28 in the MRS1T

Jeremiah 28 in the NAA

Jeremiah 28 in the NASB

Jeremiah 28 in the NBLA

Jeremiah 28 in the NBS

Jeremiah 28 in the NBVTP

Jeremiah 28 in the NET2

Jeremiah 28 in the NIV11

Jeremiah 28 in the NNT

Jeremiah 28 in the NNT2

Jeremiah 28 in the NNT3

Jeremiah 28 in the PDDPT

Jeremiah 28 in the PFNT

Jeremiah 28 in the RMNT

Jeremiah 28 in the SBIAS

Jeremiah 28 in the SBIBS

Jeremiah 28 in the SBIBS2

Jeremiah 28 in the SBICS

Jeremiah 28 in the SBIDS

Jeremiah 28 in the SBIGS

Jeremiah 28 in the SBIHS

Jeremiah 28 in the SBIIS

Jeremiah 28 in the SBIIS2

Jeremiah 28 in the SBIIS3

Jeremiah 28 in the SBIKS

Jeremiah 28 in the SBIKS2

Jeremiah 28 in the SBIMS

Jeremiah 28 in the SBIOS

Jeremiah 28 in the SBIPS

Jeremiah 28 in the SBISS

Jeremiah 28 in the SBITS

Jeremiah 28 in the SBITS2

Jeremiah 28 in the SBITS3

Jeremiah 28 in the SBITS4

Jeremiah 28 in the SBIUS

Jeremiah 28 in the SBIVS

Jeremiah 28 in the SBT

Jeremiah 28 in the SBT1E

Jeremiah 28 in the SCHL

Jeremiah 28 in the SNT

Jeremiah 28 in the SUSU

Jeremiah 28 in the SUSU2

Jeremiah 28 in the SYNO

Jeremiah 28 in the TBIAOTANT

Jeremiah 28 in the TBT1E

Jeremiah 28 in the TBT1E2

Jeremiah 28 in the TFTIP

Jeremiah 28 in the TFTU

Jeremiah 28 in the TGNTATF3T

Jeremiah 28 in the THAI

Jeremiah 28 in the TNFD

Jeremiah 28 in the TNT

Jeremiah 28 in the TNTIK

Jeremiah 28 in the TNTIL

Jeremiah 28 in the TNTIN

Jeremiah 28 in the TNTIP

Jeremiah 28 in the TNTIZ

Jeremiah 28 in the TOMA

Jeremiah 28 in the TTENT

Jeremiah 28 in the UBG

Jeremiah 28 in the UGV

Jeremiah 28 in the UGV2

Jeremiah 28 in the UGV3

Jeremiah 28 in the VBL

Jeremiah 28 in the VDCC

Jeremiah 28 in the YALU

Jeremiah 28 in the YAPE

Jeremiah 28 in the YBVTP

Jeremiah 28 in the ZBP