1 Samuel 6 (BOKCV)

1 Sanduku la BWANA lilipokuwa limekaa katika nchi ya Wafilisti kwa miezi saba, 2 Wafilisti waliwaita makuhani wa Dagoni na waaguzi, na kuwaambia, “Tutafanya nini na hili Sanduku la BWANA? Tuambieni jinsi tutakavyolirudisha mahali pake.” 3 Wakajibu, “Kama mtalirudisha Sanduku la Mungu wa Israeli, msilirudishe mikono mitupu bali kwa vyovyote mpelekeeni sadaka ya hatia. Kisha mtaponywa, nanyi mtafahamu kwa nini mkono wake haujaondolewa kwenu.” 4 Wafilisti wakawauliza, “Ni sadaka gani ya hatia tutakayompelekea?”Wakajibu, “Majipu matano ya dhahabu na panya wa dhahabu watano, kulingana na idadi ya watawala wa Wafilisti, kwa sababu tauni iyo hiyo imewaua ninyi na watawala wenu. 5 Tengenezeni mifano ya majipu na ya panya wale wanaoharibu nchi yenu, nanyi mheshimuni Mungu wa Israeli. Labda ataondoa mkono wake kutoka kwenu na kwa miungu yenu na nchi yenu. 6 Kwa nini ninyi mnafanya mioyo yenu migumu kama Wamisri na Farao walivyofanya? Je, alipowatendea kwa ukali, hawakuwaachia Waisraeli wakaenda zao? 7 “Sasa basi, wekeni gari jipya la kukokotwa pamoja na ngʼombe wawili ambao wamezaa lakini ambao kamwe hawajafungwa nira. Fungieni hao ngʼombe hilo gari, lakini ondoeni ndama wao na mwaweke zizini. 8 Chukueni hilo Sanduku la BWANA na mliweke juu ya gari la kukokotwa, na ndani ya kasha kando yake wekeni hivyo vitu vya dhahabu mnavyompelekea BWANA kama sadaka ya hatia. Lipelekeni, 9 lakini liangalieni kwa makini. Iwapo litakwenda katika nchi yake lenyewe, kuelekea Beth-Shemeshi, basi tutajua kwamba BWANA ndiye alileta haya maafa makubwa juu yetu. Lakini kama halikwenda, basi tutajua kwamba haukuwa mkono wa BWANA uliotupiga na kwamba iliyotokea kwetu ni ajali.” 10 Basi wakafanya hivyo. Wakachukua ngʼombe wawili wa aina hiyo, wakawafungia hilo gari la kukokotwa, nao ndama wao wakawekwa zizini. 11 Wakaliweka Sanduku la BWANA juu ya hilo gari la kukokotwa pamoja na lile kasha lenye ile mifano ya panya wa dhahabu na ya majipu ya dhahabu. 12 Kisha hao ngʼombe wakaenda moja kwa moja kuelekea Beth-Shemeshi, wakishuka bila kugeuka kuume au kushoto, huku wakilia njia yote. Watawala wa Wafilisti waliwafuata hao ngʼombe hadi mpakani mwa Beth-Shemeshi. 13 Wakati huu watu wa Beth-Shemeshi walikuwa wakivuna ngano yao huko bondeni, walipoinua macho yao na kuona lile Sanduku, wakafurahi kuliona. 14 Lile gari la kukokotwa lilikuja mpaka kwenye shamba la Yoshua wa Beth-Shemeshi, nalo likasimama kando ya mwamba mkubwa. Watu wakapasua mbao za lile gari la kukokotwa na kutoa dhabihu wale ngʼombe kama sadaka ya kuteketezwa kwa BWANA. 15 Walawi walilishusha Sanduku la BWANA, pamoja na lile kasha lililokuwa na vile vitu vya dhahabu na kuviweka juu ya ule mwamba mkubwa. Siku ile watu wa Beth-Shemeshi wakatoa sadaka za kuteketezwa na dhabihu kwa BWANA. 16 Wale watawala watano wa Wafilisti waliona haya yote, nao wakarudi siku ile ile mpaka Ekroni. 17 Haya ndiyo yale majipu ya dhahabu Wafilisti waliyotuma kama sadaka ya hatia kwa BWANA, moja kwa ajili ya Ashdodi, moja kwa Gaza, moja kwa Ashkeloni, moja kwa Gathi, na moja kwa Ekroni. 18 Nayo hesabu ya wale panya wa dhahabu ilikuwa kulingana na idadi ya miji ya Wafilisti ya watawala watano wa Wafilisti: miji yao iliyozungukwa na maboma, pamoja na vijiji vya miji hiyo. Ule mwamba mkubwa, ambao juu yake waliliweka lile Sanduku la BWANA, ni ushahidi hadi leo katika shamba la Yoshua wa Beth-Shemeshi. 19 Lakini Mungu aliwapiga baadhi ya watu wa Beth-Shemeshi, akiwaua watu sabini miongoni mwao kwa sababu walichungulia ndani ya Sanduku la BWANA. Watu wakaomboleza kwa sababu ya pigo zito kutoka kwa BWANA, 20 nao watu wa Beth-Shemeshi wakauliza, “Ni nani awezaye kusimama mbele za BWANA, huyu Mungu aliye mtakatifu? Sanduku litapanda kwenda kwa nani kutoka hapa?” 21 Kisha wakatuma wajumbe kwa watu wa Kiriath-Yearimu, wakisema, “Wafilisti wamerudisha Sanduku la BWANA. Shukeni na mlipandishe huko kwenu.”

In Other Versions

1 Samuel 6 in the ANGEFD

1 Samuel 6 in the ANTPNG2D

1 Samuel 6 in the AS21

1 Samuel 6 in the BAGH

1 Samuel 6 in the BBPNG

1 Samuel 6 in the BBT1E

1 Samuel 6 in the BDS

1 Samuel 6 in the BEV

1 Samuel 6 in the BHAD

1 Samuel 6 in the BIB

1 Samuel 6 in the BLPT

1 Samuel 6 in the BNT

1 Samuel 6 in the BNTABOOT

1 Samuel 6 in the BNTLV

1 Samuel 6 in the BOATCB

1 Samuel 6 in the BOATCB2

1 Samuel 6 in the BOBCV

1 Samuel 6 in the BOCNT

1 Samuel 6 in the BOECS

1 Samuel 6 in the BOGWICC

1 Samuel 6 in the BOHCB

1 Samuel 6 in the BOHCV

1 Samuel 6 in the BOHLNT

1 Samuel 6 in the BOHNTLTAL

1 Samuel 6 in the BOICB

1 Samuel 6 in the BOILNTAP

1 Samuel 6 in the BOITCV

1 Samuel 6 in the BOKCV2

1 Samuel 6 in the BOKHWOG

1 Samuel 6 in the BOKSSV

1 Samuel 6 in the BOLCB

1 Samuel 6 in the BOLCB2

1 Samuel 6 in the BOMCV

1 Samuel 6 in the BONAV

1 Samuel 6 in the BONCB

1 Samuel 6 in the BONLT

1 Samuel 6 in the BONUT2

1 Samuel 6 in the BOPLNT

1 Samuel 6 in the BOSCB

1 Samuel 6 in the BOSNC

1 Samuel 6 in the BOTLNT

1 Samuel 6 in the BOVCB

1 Samuel 6 in the BOYCB

1 Samuel 6 in the BPBB

1 Samuel 6 in the BPH

1 Samuel 6 in the BSB

1 Samuel 6 in the CCB

1 Samuel 6 in the CUV

1 Samuel 6 in the CUVS

1 Samuel 6 in the DBT

1 Samuel 6 in the DGDNT

1 Samuel 6 in the DHNT

1 Samuel 6 in the DNT

1 Samuel 6 in the ELBE

1 Samuel 6 in the EMTV

1 Samuel 6 in the ESV

1 Samuel 6 in the FBV

1 Samuel 6 in the FEB

1 Samuel 6 in the GGMNT

1 Samuel 6 in the GNT

1 Samuel 6 in the HARY

1 Samuel 6 in the HNT

1 Samuel 6 in the IRVA

1 Samuel 6 in the IRVB

1 Samuel 6 in the IRVG

1 Samuel 6 in the IRVH

1 Samuel 6 in the IRVK

1 Samuel 6 in the IRVM

1 Samuel 6 in the IRVM2

1 Samuel 6 in the IRVO

1 Samuel 6 in the IRVP

1 Samuel 6 in the IRVT

1 Samuel 6 in the IRVT2

1 Samuel 6 in the IRVU

1 Samuel 6 in the ISVN

1 Samuel 6 in the JSNT

1 Samuel 6 in the KAPI

1 Samuel 6 in the KBT1ETNIK

1 Samuel 6 in the KBV

1 Samuel 6 in the KJV

1 Samuel 6 in the KNFD

1 Samuel 6 in the LBA

1 Samuel 6 in the LBLA

1 Samuel 6 in the LNT

1 Samuel 6 in the LSV

1 Samuel 6 in the MAAL

1 Samuel 6 in the MBV

1 Samuel 6 in the MBV2

1 Samuel 6 in the MHNT

1 Samuel 6 in the MKNFD

1 Samuel 6 in the MNG

1 Samuel 6 in the MNT

1 Samuel 6 in the MNT2

1 Samuel 6 in the MRS1T

1 Samuel 6 in the NAA

1 Samuel 6 in the NASB

1 Samuel 6 in the NBLA

1 Samuel 6 in the NBS

1 Samuel 6 in the NBVTP

1 Samuel 6 in the NET2

1 Samuel 6 in the NIV11

1 Samuel 6 in the NNT

1 Samuel 6 in the NNT2

1 Samuel 6 in the NNT3

1 Samuel 6 in the PDDPT

1 Samuel 6 in the PFNT

1 Samuel 6 in the RMNT

1 Samuel 6 in the SBIAS

1 Samuel 6 in the SBIBS

1 Samuel 6 in the SBIBS2

1 Samuel 6 in the SBICS

1 Samuel 6 in the SBIDS

1 Samuel 6 in the SBIGS

1 Samuel 6 in the SBIHS

1 Samuel 6 in the SBIIS

1 Samuel 6 in the SBIIS2

1 Samuel 6 in the SBIIS3

1 Samuel 6 in the SBIKS

1 Samuel 6 in the SBIKS2

1 Samuel 6 in the SBIMS

1 Samuel 6 in the SBIOS

1 Samuel 6 in the SBIPS

1 Samuel 6 in the SBISS

1 Samuel 6 in the SBITS

1 Samuel 6 in the SBITS2

1 Samuel 6 in the SBITS3

1 Samuel 6 in the SBITS4

1 Samuel 6 in the SBIUS

1 Samuel 6 in the SBIVS

1 Samuel 6 in the SBT

1 Samuel 6 in the SBT1E

1 Samuel 6 in the SCHL

1 Samuel 6 in the SNT

1 Samuel 6 in the SUSU

1 Samuel 6 in the SUSU2

1 Samuel 6 in the SYNO

1 Samuel 6 in the TBIAOTANT

1 Samuel 6 in the TBT1E

1 Samuel 6 in the TBT1E2

1 Samuel 6 in the TFTIP

1 Samuel 6 in the TFTU

1 Samuel 6 in the TGNTATF3T

1 Samuel 6 in the THAI

1 Samuel 6 in the TNFD

1 Samuel 6 in the TNT

1 Samuel 6 in the TNTIK

1 Samuel 6 in the TNTIL

1 Samuel 6 in the TNTIN

1 Samuel 6 in the TNTIP

1 Samuel 6 in the TNTIZ

1 Samuel 6 in the TOMA

1 Samuel 6 in the TTENT

1 Samuel 6 in the UBG

1 Samuel 6 in the UGV

1 Samuel 6 in the UGV2

1 Samuel 6 in the UGV3

1 Samuel 6 in the VBL

1 Samuel 6 in the VDCC

1 Samuel 6 in the YALU

1 Samuel 6 in the YAPE

1 Samuel 6 in the YBVTP

1 Samuel 6 in the ZBP