Deuteronomy 18 (BOKCV)

1 Makuhani ambao ni Walawi, yaani kabila lote la Lawi, hawatakuwa na mgawo wala urithi pamoja na Israeli. Wataishi kwa sadaka zitolewazo kwa ajili ya BWANA za kuteketezwa kwa moto, kwa maana huo ndio urithi wao. 2 Hawatakuwa na urithi miongoni mwa ndugu zao; BWANA ndiye urithi wao, kama alivyowaahidi. 3 Hili ndilo fungu la makuhani kutoka kwa watu watakaotoa dhabihu ya fahali au kondoo: mguu wa mbele, mataya na matumbo. 4 Mtawapa malimbuko ya nafaka zenu, divai mpya, mafuta na sufu ya kwanza kutoka manyoya ya kondoo zenu, 5 kwa kuwa BWANA Mungu wenu amewachagua pamoja na wazao wao kutoka makabila yenu kusimama na kuhudumu katika jina la BWANA siku zote. 6 Ikiwa Mlawi atahama kutoka mmojawapo ya miji yenu popote katika Israeli ambapo anaishi, akaja kwa moyo wote mahali ambapo BWANA atapachagua, 7 anaweza akahudumu katika jina la BWANA Mungu wake kama Walawi wenzake wote wanaohudumu hapo mbele za BWANA. 8 Atashiriki sawa katika mafao yao, hata kama amepokea fedha kutoka mauzo ya mali ya jamaa yake. 9 Wakati mtakapoingia katika nchi ambayo BWANA Mungu wenu anawapa, msijifunze kuiga njia za machukizo za mataifa ya huko. 10 Asionekane mtu yeyote miongoni mwenu ampitishaye mwanawe au binti yake katika moto, atakayefanya uaguzi, ulozi, anayetabiri nyakati, anayejishughulisha na uchawi, 11 wala arogaye kwa kupiga mafundo, wala mwaguzi au anayeabudu mizimu, wala awaombaye wafu. 12 Mtu yeyote afanyaye mambo haya ni chukizo kwa BWANA, tena ni kwa sababu ya matendo haya ya kuchukiza wayafanyayo ndiyo maana BWANA Mungu wenu atayafukuza mataifa hayo mbele yenu. 13 Kamwe msilaumiwe mbele za BWANA Mungu wenu. 14 Mataifa mtakayowafukuza husikiliza wale wafanyao ulozi na uaguzi. Lakini kwenu ninyi, BWANA Mungu wenu hajawaruhusu kufanya hivyo. 15 BWANA Mungu wenu atawainulia nabii kama mimi kutoka miongoni mwa ndugu zenu wenyewe. Msikilizeni yeye. 16 Kwa kuwa hivi ndivyo mlivyomwomba BWANA Mungu wenu kule Horebu siku ile ya kusanyiko, wakati mliposema, “Na tusiisikie sauti ya BWANA Mungu wetu, wala kuuona moto huu mkubwa tena, ama sivyo tutakufa.” 17 BWANA akaniambia: “Wanachosema ni vyema. 18 Nitawainulia nabii kama wewe kutoka miongoni mwa ndugu zao; nitaweka maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia kila kitu nitakachomwamuru. 19 Kama mtu yeyote hatasikiliza maneno yangu ambayo huyo nabii atayasema kwa Jina langu, mimi mwenyewe nitamwajibisha. 20 Lakini nabii ambaye atathubutu kusema kwa Jina langu kitu chochote ambacho sikumwamuru akiseme, au nabii ambaye husema kwa jina la miungu mingine ni lazima auawe.” 21 Mnaweza kuulizana wenyewe, “Tutawezaje kujua wakati ujumbe haukusemwa na BWANA?” 22 Ikiwa kile nabii anachotangaza kwa jina la BWANA hakikutokea au kutimia, huo ni ujumbe ambao BWANA hakusema. Nabii huyo amesema kwa ujuaji. Msimwogope huyo.

In Other Versions

Deuteronomy 18 in the ANGEFD

Deuteronomy 18 in the ANTPNG2D

Deuteronomy 18 in the AS21

Deuteronomy 18 in the BAGH

Deuteronomy 18 in the BBPNG

Deuteronomy 18 in the BBT1E

Deuteronomy 18 in the BDS

Deuteronomy 18 in the BEV

Deuteronomy 18 in the BHAD

Deuteronomy 18 in the BIB

Deuteronomy 18 in the BLPT

Deuteronomy 18 in the BNT

Deuteronomy 18 in the BNTABOOT

Deuteronomy 18 in the BNTLV

Deuteronomy 18 in the BOATCB

Deuteronomy 18 in the BOATCB2

Deuteronomy 18 in the BOBCV

Deuteronomy 18 in the BOCNT

Deuteronomy 18 in the BOECS

Deuteronomy 18 in the BOGWICC

Deuteronomy 18 in the BOHCB

Deuteronomy 18 in the BOHCV

Deuteronomy 18 in the BOHLNT

Deuteronomy 18 in the BOHNTLTAL

Deuteronomy 18 in the BOICB

Deuteronomy 18 in the BOILNTAP

Deuteronomy 18 in the BOITCV

Deuteronomy 18 in the BOKCV2

Deuteronomy 18 in the BOKHWOG

Deuteronomy 18 in the BOKSSV

Deuteronomy 18 in the BOLCB

Deuteronomy 18 in the BOLCB2

Deuteronomy 18 in the BOMCV

Deuteronomy 18 in the BONAV

Deuteronomy 18 in the BONCB

Deuteronomy 18 in the BONLT

Deuteronomy 18 in the BONUT2

Deuteronomy 18 in the BOPLNT

Deuteronomy 18 in the BOSCB

Deuteronomy 18 in the BOSNC

Deuteronomy 18 in the BOTLNT

Deuteronomy 18 in the BOVCB

Deuteronomy 18 in the BOYCB

Deuteronomy 18 in the BPBB

Deuteronomy 18 in the BPH

Deuteronomy 18 in the BSB

Deuteronomy 18 in the CCB

Deuteronomy 18 in the CUV

Deuteronomy 18 in the CUVS

Deuteronomy 18 in the DBT

Deuteronomy 18 in the DGDNT

Deuteronomy 18 in the DHNT

Deuteronomy 18 in the DNT

Deuteronomy 18 in the ELBE

Deuteronomy 18 in the EMTV

Deuteronomy 18 in the ESV

Deuteronomy 18 in the FBV

Deuteronomy 18 in the FEB

Deuteronomy 18 in the GGMNT

Deuteronomy 18 in the GNT

Deuteronomy 18 in the HARY

Deuteronomy 18 in the HNT

Deuteronomy 18 in the IRVA

Deuteronomy 18 in the IRVB

Deuteronomy 18 in the IRVG

Deuteronomy 18 in the IRVH

Deuteronomy 18 in the IRVK

Deuteronomy 18 in the IRVM

Deuteronomy 18 in the IRVM2

Deuteronomy 18 in the IRVO

Deuteronomy 18 in the IRVP

Deuteronomy 18 in the IRVT

Deuteronomy 18 in the IRVT2

Deuteronomy 18 in the IRVU

Deuteronomy 18 in the ISVN

Deuteronomy 18 in the JSNT

Deuteronomy 18 in the KAPI

Deuteronomy 18 in the KBT1ETNIK

Deuteronomy 18 in the KBV

Deuteronomy 18 in the KJV

Deuteronomy 18 in the KNFD

Deuteronomy 18 in the LBA

Deuteronomy 18 in the LBLA

Deuteronomy 18 in the LNT

Deuteronomy 18 in the LSV

Deuteronomy 18 in the MAAL

Deuteronomy 18 in the MBV

Deuteronomy 18 in the MBV2

Deuteronomy 18 in the MHNT

Deuteronomy 18 in the MKNFD

Deuteronomy 18 in the MNG

Deuteronomy 18 in the MNT

Deuteronomy 18 in the MNT2

Deuteronomy 18 in the MRS1T

Deuteronomy 18 in the NAA

Deuteronomy 18 in the NASB

Deuteronomy 18 in the NBLA

Deuteronomy 18 in the NBS

Deuteronomy 18 in the NBVTP

Deuteronomy 18 in the NET2

Deuteronomy 18 in the NIV11

Deuteronomy 18 in the NNT

Deuteronomy 18 in the NNT2

Deuteronomy 18 in the NNT3

Deuteronomy 18 in the PDDPT

Deuteronomy 18 in the PFNT

Deuteronomy 18 in the RMNT

Deuteronomy 18 in the SBIAS

Deuteronomy 18 in the SBIBS

Deuteronomy 18 in the SBIBS2

Deuteronomy 18 in the SBICS

Deuteronomy 18 in the SBIDS

Deuteronomy 18 in the SBIGS

Deuteronomy 18 in the SBIHS

Deuteronomy 18 in the SBIIS

Deuteronomy 18 in the SBIIS2

Deuteronomy 18 in the SBIIS3

Deuteronomy 18 in the SBIKS

Deuteronomy 18 in the SBIKS2

Deuteronomy 18 in the SBIMS

Deuteronomy 18 in the SBIOS

Deuteronomy 18 in the SBIPS

Deuteronomy 18 in the SBISS

Deuteronomy 18 in the SBITS

Deuteronomy 18 in the SBITS2

Deuteronomy 18 in the SBITS3

Deuteronomy 18 in the SBITS4

Deuteronomy 18 in the SBIUS

Deuteronomy 18 in the SBIVS

Deuteronomy 18 in the SBT

Deuteronomy 18 in the SBT1E

Deuteronomy 18 in the SCHL

Deuteronomy 18 in the SNT

Deuteronomy 18 in the SUSU

Deuteronomy 18 in the SUSU2

Deuteronomy 18 in the SYNO

Deuteronomy 18 in the TBIAOTANT

Deuteronomy 18 in the TBT1E

Deuteronomy 18 in the TBT1E2

Deuteronomy 18 in the TFTIP

Deuteronomy 18 in the TFTU

Deuteronomy 18 in the TGNTATF3T

Deuteronomy 18 in the THAI

Deuteronomy 18 in the TNFD

Deuteronomy 18 in the TNT

Deuteronomy 18 in the TNTIK

Deuteronomy 18 in the TNTIL

Deuteronomy 18 in the TNTIN

Deuteronomy 18 in the TNTIP

Deuteronomy 18 in the TNTIZ

Deuteronomy 18 in the TOMA

Deuteronomy 18 in the TTENT

Deuteronomy 18 in the UBG

Deuteronomy 18 in the UGV

Deuteronomy 18 in the UGV2

Deuteronomy 18 in the UGV3

Deuteronomy 18 in the VBL

Deuteronomy 18 in the VDCC

Deuteronomy 18 in the YALU

Deuteronomy 18 in the YAPE

Deuteronomy 18 in the YBVTP

Deuteronomy 18 in the ZBP