Ezekiel 24 (BOKCV)

1 Katika mwaka wa tisa, mwezi wa kumi, siku ya kumi, neno la BWANA likanijia kusema: 2 “Mwanadamu, weka kumbukumbu ya tarehe hii, tarehe hii hasa, kwa kuwa mfalme wa Babeli ameuzingira mji wa Yerusalemu kwa jeshi siku hii ya leo. 3 Iambie nyumba hii ya kuasi fumbo, na uwaambie, ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo:“ ‘Teleka sufuria jikoni; itelekena umimine maji ndani yake, 4 Weka vipande vya nyama ndani yake,vipande vyote vizuri,vya paja na vya bega.Ijaze hiyo sufuria kwa mifupa hii mizuri; 5 chagua yule aliye bora wa kundi la kondoo.Panga kuni chini ya sufuria kwa ajili ya mifupa;chochea mpaka ichemkena uitokose hiyo mifupa ndani yake. 6 “ ‘Kwa kuwa hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo:“ ‘Ole wa mji umwagao damu,ole wa sufuria ambayo sasaina ukoko ndani yake,ambayo ukoko wake hautoki.Kipakue kipande baada ya kipande,bila kuvipigia kura. 7 “ ‘Kwa kuwa damu aliyoimwaga ipo katikati yake:huyo mwanamke aliimwagajuu ya mwamba ulio wazi;hakuimwaga kwenye ardhi,ambako vumbi lingeifunika. 8 Kuchochea ghadhabu na kulipiza kisasi,nimemwaga damu yakejuu ya mwamba ulio wazi,ili isifunikwe. 9 “ ‘Kwa hiyo, hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo:“ ‘Ole wa mji umwagao damu!Mimi nami nitalundikia kuni nyingi. 10 Kwa hiyo lundika kunina uwashe moto.Pika hiyo nyama vizuri,changanya viungo ndani yake,na uiache mifupa iungue kwenye moto. 11 Kisha teleka sufuria tupu kwenye makaampaka iwe na moto sana na shaba yake ingʼae,ili uchafu wake upate kuyeyukana ukoko wake upate kuungua na kuondoka. 12 Imezuia juhudi zote,ukoko wake mwingi haujaondoka,hata ikiwa ni kwa moto. 13 “ ‘Sasa uchafu wako ni uasherati wako. Kwa sababu nilijaribu kukutakasa lakini haikuwezekana kutakaswa kutoka kwenye huo uchafu wako, hutatakasika tena mpaka ghadhabu yangu dhidi yako iwe imepungua. 14 “ ‘Mimi BWANA nimesema, wakati umewadia wa mimi kutenda. Mimi sitazuia, mimi sitaona huruma wala sitapunguza hasira yangu, Utahukumiwa sawasawa na mwenendo na matendo yako, asema BWANA Mwenyezi.’ ” 15 Neno la BWANA likanijia kusema: 16 “Mwanadamu, kwa pigo moja nakaribia kukuondolea kile kilicho furaha ya macho yako. Lakini usiomboleze au kulia wala kudondosha machozi yoyote. 17 Lia kwa uchungu kimya kimya usimwombolezee mtu aliyekufa. Jifunge kilemba chako na uvae viatu vyako miguuni mwako, usifunike sehemu ya chini ya uso wako, wala usile vyakula vya kawaida vya wakati wa matanga.” 18 Hivyo nikanena na watu asubuhi na jioni mke wangu akafa. Asubuhi yake nilifanya kama nilivyoamriwa. 19 Ndipo watu wakaniuliza, “Je, jambo hili unalofanya linamaanisha nini kwetu?” 20 Kwa hiyo nikawaambia, “Neno la BWANA lilinijia kusema: 21 ‘Sema na nyumba ya Israeli. Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Ninakaribia kupatia unajisi mahali pangu patakatifu, ngome ambayo ndani yake mnaona fahari, furaha ya macho yenu, kitu mnachokipenda. Wana wenu na binti zenu mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga. 22 Nanyi mtafanya kama nilivyofanya. Hamtafunika sehemu ya chini ya nyuso zenu wala hamtakula vyakula vya kawaida vya waombolezaji. 23 Mtajifunga vilemba vichwani mwenu na kuvaa viatu vyenu miguuni mwenu. Hamtaomboleza au kulia, lakini mtadhoofika kwa sababu ya dhambi zenu na kulia kwa uchungu kila mtu na mwenzake. 24 Ezekieli atakuwa ishara kwenu, mtafanya kama yeye alivyofanya. Wakati jambo hili litakapotokea, mtajua kuwa Mimi ndimi BWANA Mwenyezi.’ 25 “Nawe, mwanadamu, siku ile nitakapoondoa ngome yao iliyo furaha yao na utukufu wao, kitu cha kupendeza macho yao, kile kilicho shauku ya mioyo yao, wana wao na binti zao vilevile, 26 siku hiyo atakayetoroka atakuja kuwapasha habari. 27 Katika siku ile kinywa chako kitamfumbukia yeye aliyenusurika, nawe utaongea wala hutanyamaza tena. Hivyo wewe utakuwa ishara kwao, nao watajua kuwa Mimi ndimi BWANA.”

In Other Versions

Ezekiel 24 in the ANGEFD

Ezekiel 24 in the ANTPNG2D

Ezekiel 24 in the AS21

Ezekiel 24 in the BAGH

Ezekiel 24 in the BBPNG

Ezekiel 24 in the BBT1E

Ezekiel 24 in the BDS

Ezekiel 24 in the BEV

Ezekiel 24 in the BHAD

Ezekiel 24 in the BIB

Ezekiel 24 in the BLPT

Ezekiel 24 in the BNT

Ezekiel 24 in the BNTABOOT

Ezekiel 24 in the BNTLV

Ezekiel 24 in the BOATCB

Ezekiel 24 in the BOATCB2

Ezekiel 24 in the BOBCV

Ezekiel 24 in the BOCNT

Ezekiel 24 in the BOECS

Ezekiel 24 in the BOGWICC

Ezekiel 24 in the BOHCB

Ezekiel 24 in the BOHCV

Ezekiel 24 in the BOHLNT

Ezekiel 24 in the BOHNTLTAL

Ezekiel 24 in the BOICB

Ezekiel 24 in the BOILNTAP

Ezekiel 24 in the BOITCV

Ezekiel 24 in the BOKCV2

Ezekiel 24 in the BOKHWOG

Ezekiel 24 in the BOKSSV

Ezekiel 24 in the BOLCB

Ezekiel 24 in the BOLCB2

Ezekiel 24 in the BOMCV

Ezekiel 24 in the BONAV

Ezekiel 24 in the BONCB

Ezekiel 24 in the BONLT

Ezekiel 24 in the BONUT2

Ezekiel 24 in the BOPLNT

Ezekiel 24 in the BOSCB

Ezekiel 24 in the BOSNC

Ezekiel 24 in the BOTLNT

Ezekiel 24 in the BOVCB

Ezekiel 24 in the BOYCB

Ezekiel 24 in the BPBB

Ezekiel 24 in the BPH

Ezekiel 24 in the BSB

Ezekiel 24 in the CCB

Ezekiel 24 in the CUV

Ezekiel 24 in the CUVS

Ezekiel 24 in the DBT

Ezekiel 24 in the DGDNT

Ezekiel 24 in the DHNT

Ezekiel 24 in the DNT

Ezekiel 24 in the ELBE

Ezekiel 24 in the EMTV

Ezekiel 24 in the ESV

Ezekiel 24 in the FBV

Ezekiel 24 in the FEB

Ezekiel 24 in the GGMNT

Ezekiel 24 in the GNT

Ezekiel 24 in the HARY

Ezekiel 24 in the HNT

Ezekiel 24 in the IRVA

Ezekiel 24 in the IRVB

Ezekiel 24 in the IRVG

Ezekiel 24 in the IRVH

Ezekiel 24 in the IRVK

Ezekiel 24 in the IRVM

Ezekiel 24 in the IRVM2

Ezekiel 24 in the IRVO

Ezekiel 24 in the IRVP

Ezekiel 24 in the IRVT

Ezekiel 24 in the IRVT2

Ezekiel 24 in the IRVU

Ezekiel 24 in the ISVN

Ezekiel 24 in the JSNT

Ezekiel 24 in the KAPI

Ezekiel 24 in the KBT1ETNIK

Ezekiel 24 in the KBV

Ezekiel 24 in the KJV

Ezekiel 24 in the KNFD

Ezekiel 24 in the LBA

Ezekiel 24 in the LBLA

Ezekiel 24 in the LNT

Ezekiel 24 in the LSV

Ezekiel 24 in the MAAL

Ezekiel 24 in the MBV

Ezekiel 24 in the MBV2

Ezekiel 24 in the MHNT

Ezekiel 24 in the MKNFD

Ezekiel 24 in the MNG

Ezekiel 24 in the MNT

Ezekiel 24 in the MNT2

Ezekiel 24 in the MRS1T

Ezekiel 24 in the NAA

Ezekiel 24 in the NASB

Ezekiel 24 in the NBLA

Ezekiel 24 in the NBS

Ezekiel 24 in the NBVTP

Ezekiel 24 in the NET2

Ezekiel 24 in the NIV11

Ezekiel 24 in the NNT

Ezekiel 24 in the NNT2

Ezekiel 24 in the NNT3

Ezekiel 24 in the PDDPT

Ezekiel 24 in the PFNT

Ezekiel 24 in the RMNT

Ezekiel 24 in the SBIAS

Ezekiel 24 in the SBIBS

Ezekiel 24 in the SBIBS2

Ezekiel 24 in the SBICS

Ezekiel 24 in the SBIDS

Ezekiel 24 in the SBIGS

Ezekiel 24 in the SBIHS

Ezekiel 24 in the SBIIS

Ezekiel 24 in the SBIIS2

Ezekiel 24 in the SBIIS3

Ezekiel 24 in the SBIKS

Ezekiel 24 in the SBIKS2

Ezekiel 24 in the SBIMS

Ezekiel 24 in the SBIOS

Ezekiel 24 in the SBIPS

Ezekiel 24 in the SBISS

Ezekiel 24 in the SBITS

Ezekiel 24 in the SBITS2

Ezekiel 24 in the SBITS3

Ezekiel 24 in the SBITS4

Ezekiel 24 in the SBIUS

Ezekiel 24 in the SBIVS

Ezekiel 24 in the SBT

Ezekiel 24 in the SBT1E

Ezekiel 24 in the SCHL

Ezekiel 24 in the SNT

Ezekiel 24 in the SUSU

Ezekiel 24 in the SUSU2

Ezekiel 24 in the SYNO

Ezekiel 24 in the TBIAOTANT

Ezekiel 24 in the TBT1E

Ezekiel 24 in the TBT1E2

Ezekiel 24 in the TFTIP

Ezekiel 24 in the TFTU

Ezekiel 24 in the TGNTATF3T

Ezekiel 24 in the THAI

Ezekiel 24 in the TNFD

Ezekiel 24 in the TNT

Ezekiel 24 in the TNTIK

Ezekiel 24 in the TNTIL

Ezekiel 24 in the TNTIN

Ezekiel 24 in the TNTIP

Ezekiel 24 in the TNTIZ

Ezekiel 24 in the TOMA

Ezekiel 24 in the TTENT

Ezekiel 24 in the UBG

Ezekiel 24 in the UGV

Ezekiel 24 in the UGV2

Ezekiel 24 in the UGV3

Ezekiel 24 in the VBL

Ezekiel 24 in the VDCC

Ezekiel 24 in the YALU

Ezekiel 24 in the YAPE

Ezekiel 24 in the YBVTP

Ezekiel 24 in the ZBP