Ezekiel 29 (BOKCV)

1 Katika mwaka wa kumi, mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili, neno la BWANA likanijia kusema: 2 “Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya Farao mfalme wa Misri na utabiri dhidi yake na dhidi ya Misri yote. 3 Nena, nawe useme: ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo:“ ‘Mimi ni kinyume nawe, Farao, mfalme wa Misri,joka kubwa ulalaye katikati ya vijito vyako.Unasema, “Mto Naili ni wangu mwenyewe;niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.” 4 Lakini nitatia ndoana katika mataya yakonami nitawafanya samaki wa vijito vyakowashikamane na magamba yako.Nitakutoa katikati ya vijito vyako,pamoja na samaki wotewalioshikamana na magamba yako. 5 Nitakutupa jangwani,wewe pamoja na samaki wote wa vijito vyako.Utaanguka uwanjani,nawe hutakusanywa au kuchukuliwa.Nitakutoa uwe chakulakwa wanyama wa nchina ndege wa angani. 6 Ndipo wale wote waishio Misri watakapojua kuwa Mimi ndimi BWANA.“ ‘Umekuwa fimbo ya tete kwa nyumba ya Israeli. 7 Walipokushika kwa mikono yao, ulivunjika na kuchana mabega yao; walipokuegemea, ulivunjika na migongo yao ikateguka. 8 “ ‘Kwa hiyo hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Nitaleta upanga juu yako na kuua watu wako na wanyama wao. 9 Misri itakuwa ukiwa na isiyolimwa wala kukaliwa na watu. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi BWANA.“ ‘Kwa sababu ulisema, “Mto Naili ni wangu; mimi niliufanya,” 10 kwa hiyo mimi ni kinyume nawe na kinyume na vijito vyako, nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa magofu na ukiwa isiyolimwa wala kukaliwa na watu kuanzia Migdoli hadi Aswani, hata kufikia mpakani wa Ethiopia. 11 Hakuna unyayo wa mtu au mnyama utakaopita ndani yake, wala hakuna yeyote atakayeishi humo kwa muda wa miaka arobaini. 12 Nitaifanya nchi ya Misri ukiwa, miongoni mwa nchi zilizo ukiwa, nayo miji yake itabaki ukiwa miaka arobaini miongoni mwa miji iliyo magofu. Nami nitawatawanya Wamisri miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi nyingine. 13 “ ‘Lakini hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Mwishoni mwa hiyo miaka arobaini, nitawakusanya Wamisri kutoka mataifa walikotawanywa. 14 Nitawarudisha hao Wamisri kutoka kwenye kutekwa kwao na kuwaweka katika Pathrosi, nchi ya baba zao. Huko watakuwa na ufalme usiokuwa na nguvu. 15 Utakuwa ufalme dhaifu kuliko zote na kamwe Misri haitajikweza tena juu ya mataifa mengine. Nitaufanya ufalme wake dhaifu sana kiasi kwamba kamwe hautatawala tena juu ya mataifa mengine. 16 Misri haitakuwa tena tumaini la watu wa Israeli bali itakuwa kumbukumbu ya dhambi yao kwa kuigeukia kuomba msaada. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi BWANA Mwenyezi.’ ” 17 Katika mwaka wa ishirini na saba, mwezi wa kwanza, siku ya kwanza, neno la BWANA likanijia, kusema: 18 “Mwanadamu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliongoza jeshi lake kufanya kazi ngumu dhidi ya Tiro; kila kichwa kilipata upaa na kila bega likachunika. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo yoyote kutokana na muda wote aliongoza hiyo vita dhidi ya Tiro. 19 Kwa hiyo hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Nitaitia Misri mikononi mwa Nebukadneza mfalme wa Babeli, naye atachukua utajiri wa Misri. Atateka mateka na kuchukua nyara mali za Misri kama ujira kwa ajili ya jeshi lake. 20 Nimempa mfalme wa Babeli nchi ya Misri kuwa ujira kwa juhudi zake kwa sababu yeye na jeshi lake walifanya kwa ajili yangu, asema BWANA Mwenyezi. 21 “Katika siku hiyo nitaifanya nyumba ya Israeli iwe na nguvu nami nitakifungua kinywa chako miongoni mwao. Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi BWANA.”

In Other Versions

Ezekiel 29 in the ANGEFD

Ezekiel 29 in the ANTPNG2D

Ezekiel 29 in the AS21

Ezekiel 29 in the BAGH

Ezekiel 29 in the BBPNG

Ezekiel 29 in the BBT1E

Ezekiel 29 in the BDS

Ezekiel 29 in the BEV

Ezekiel 29 in the BHAD

Ezekiel 29 in the BIB

Ezekiel 29 in the BLPT

Ezekiel 29 in the BNT

Ezekiel 29 in the BNTABOOT

Ezekiel 29 in the BNTLV

Ezekiel 29 in the BOATCB

Ezekiel 29 in the BOATCB2

Ezekiel 29 in the BOBCV

Ezekiel 29 in the BOCNT

Ezekiel 29 in the BOECS

Ezekiel 29 in the BOGWICC

Ezekiel 29 in the BOHCB

Ezekiel 29 in the BOHCV

Ezekiel 29 in the BOHLNT

Ezekiel 29 in the BOHNTLTAL

Ezekiel 29 in the BOICB

Ezekiel 29 in the BOILNTAP

Ezekiel 29 in the BOITCV

Ezekiel 29 in the BOKCV2

Ezekiel 29 in the BOKHWOG

Ezekiel 29 in the BOKSSV

Ezekiel 29 in the BOLCB

Ezekiel 29 in the BOLCB2

Ezekiel 29 in the BOMCV

Ezekiel 29 in the BONAV

Ezekiel 29 in the BONCB

Ezekiel 29 in the BONLT

Ezekiel 29 in the BONUT2

Ezekiel 29 in the BOPLNT

Ezekiel 29 in the BOSCB

Ezekiel 29 in the BOSNC

Ezekiel 29 in the BOTLNT

Ezekiel 29 in the BOVCB

Ezekiel 29 in the BOYCB

Ezekiel 29 in the BPBB

Ezekiel 29 in the BPH

Ezekiel 29 in the BSB

Ezekiel 29 in the CCB

Ezekiel 29 in the CUV

Ezekiel 29 in the CUVS

Ezekiel 29 in the DBT

Ezekiel 29 in the DGDNT

Ezekiel 29 in the DHNT

Ezekiel 29 in the DNT

Ezekiel 29 in the ELBE

Ezekiel 29 in the EMTV

Ezekiel 29 in the ESV

Ezekiel 29 in the FBV

Ezekiel 29 in the FEB

Ezekiel 29 in the GGMNT

Ezekiel 29 in the GNT

Ezekiel 29 in the HARY

Ezekiel 29 in the HNT

Ezekiel 29 in the IRVA

Ezekiel 29 in the IRVB

Ezekiel 29 in the IRVG

Ezekiel 29 in the IRVH

Ezekiel 29 in the IRVK

Ezekiel 29 in the IRVM

Ezekiel 29 in the IRVM2

Ezekiel 29 in the IRVO

Ezekiel 29 in the IRVP

Ezekiel 29 in the IRVT

Ezekiel 29 in the IRVT2

Ezekiel 29 in the IRVU

Ezekiel 29 in the ISVN

Ezekiel 29 in the JSNT

Ezekiel 29 in the KAPI

Ezekiel 29 in the KBT1ETNIK

Ezekiel 29 in the KBV

Ezekiel 29 in the KJV

Ezekiel 29 in the KNFD

Ezekiel 29 in the LBA

Ezekiel 29 in the LBLA

Ezekiel 29 in the LNT

Ezekiel 29 in the LSV

Ezekiel 29 in the MAAL

Ezekiel 29 in the MBV

Ezekiel 29 in the MBV2

Ezekiel 29 in the MHNT

Ezekiel 29 in the MKNFD

Ezekiel 29 in the MNG

Ezekiel 29 in the MNT

Ezekiel 29 in the MNT2

Ezekiel 29 in the MRS1T

Ezekiel 29 in the NAA

Ezekiel 29 in the NASB

Ezekiel 29 in the NBLA

Ezekiel 29 in the NBS

Ezekiel 29 in the NBVTP

Ezekiel 29 in the NET2

Ezekiel 29 in the NIV11

Ezekiel 29 in the NNT

Ezekiel 29 in the NNT2

Ezekiel 29 in the NNT3

Ezekiel 29 in the PDDPT

Ezekiel 29 in the PFNT

Ezekiel 29 in the RMNT

Ezekiel 29 in the SBIAS

Ezekiel 29 in the SBIBS

Ezekiel 29 in the SBIBS2

Ezekiel 29 in the SBICS

Ezekiel 29 in the SBIDS

Ezekiel 29 in the SBIGS

Ezekiel 29 in the SBIHS

Ezekiel 29 in the SBIIS

Ezekiel 29 in the SBIIS2

Ezekiel 29 in the SBIIS3

Ezekiel 29 in the SBIKS

Ezekiel 29 in the SBIKS2

Ezekiel 29 in the SBIMS

Ezekiel 29 in the SBIOS

Ezekiel 29 in the SBIPS

Ezekiel 29 in the SBISS

Ezekiel 29 in the SBITS

Ezekiel 29 in the SBITS2

Ezekiel 29 in the SBITS3

Ezekiel 29 in the SBITS4

Ezekiel 29 in the SBIUS

Ezekiel 29 in the SBIVS

Ezekiel 29 in the SBT

Ezekiel 29 in the SBT1E

Ezekiel 29 in the SCHL

Ezekiel 29 in the SNT

Ezekiel 29 in the SUSU

Ezekiel 29 in the SUSU2

Ezekiel 29 in the SYNO

Ezekiel 29 in the TBIAOTANT

Ezekiel 29 in the TBT1E

Ezekiel 29 in the TBT1E2

Ezekiel 29 in the TFTIP

Ezekiel 29 in the TFTU

Ezekiel 29 in the TGNTATF3T

Ezekiel 29 in the THAI

Ezekiel 29 in the TNFD

Ezekiel 29 in the TNT

Ezekiel 29 in the TNTIK

Ezekiel 29 in the TNTIL

Ezekiel 29 in the TNTIN

Ezekiel 29 in the TNTIP

Ezekiel 29 in the TNTIZ

Ezekiel 29 in the TOMA

Ezekiel 29 in the TTENT

Ezekiel 29 in the UBG

Ezekiel 29 in the UGV

Ezekiel 29 in the UGV2

Ezekiel 29 in the UGV3

Ezekiel 29 in the VBL

Ezekiel 29 in the VDCC

Ezekiel 29 in the YALU

Ezekiel 29 in the YAPE

Ezekiel 29 in the YBVTP

Ezekiel 29 in the ZBP