Judges 15 (BOKCV)

1 Baada ya kitambo kidogo, wakati wa mavuno ya ngano, Samsoni akachukua mwana-mbuzi, kwenda kumzuru mkewe. Akasema, “Nataka kuingia chumbani kwa mke wangu.” Lakini baba yake huyo mwanamke hakumruhusu kuingia. 2 Huyo baba mkwe wake akamwambia, “Nilikuwa na hakika kwamba ulimkataa, hivyo mimi nikampa rafiki yako. Je, mdogo wake wa kike si mzuri zaidi kuliko yeye? Mchukue huyo badala yake.” 3 Samsoni akawaambia, “Wakati huu, nitakapowadhuru Wafilisti, sitakuwa na lawama.” 4 Hivyo Samsoni akatoka akawakamata mbweha 300 na kuwafunga wawili wawili kwa mikia yao kila mmoja kwa mwingine. Kisha akafungia mwenge wa moto, kwenye mikia ya kila jozi moja ya mbweha aliyokuwa ameifunga, 5 akawasha ile mienge na kuwaachia wale mbweha katika mashamba ya Wafilisti ya nafaka zilizosimamishwa katika matita. Akateketeza matita ya nafaka zilizosimama, pamoja na mashamba ya mizabibu na viunga vya mizeituni. 6 Ndipo Wafilisti wakauliza, “Ni nani aliyetenda jambo hili?” Wakaambiwa, “Ni Samsoni, yule mkwewe Mtimna, kwa sababu alimchukua mkewe akampa mwenzake.”Hivyo Wafilisti wakapanda wakamteketeza kwa moto yeye huyo mwanamke pamoja na baba yake. 7 Samsoni akawaambia, “Kwa kuwa mmetenda hivyo, hakika sitatulia mpaka niwe nimelipiza kisasi juu yenu.” 8 Akawashambulia kwa ukali kwa mapigo makuu na kuwaua watu wengi sana. Kisha akateremka na kukaa katika ufa kwenye mwamba wa Etamu. 9 Wafilisti wakapanda na kupiga kambi huko Yuda na kuenea huko Lehi. 10 Watu wa Yuda wakawauliza, “Kwa nini mmekuja kupigana nasi?”Wakawajibu, “Tumekuja ili kumkamata Samsoni na kumtenda kama alivyotutendea.” 11 Ndipo watu 3,000 toka Yuda walipoteremka na kwenda kwenye ufa wa mwamba huko Etamu, na kumwambia Samsoni, “Je, hujatambua kuwa Wafilisti wanatutawala? Ni nini hiki ulichotutendea?”Akawajibu, “Mimi nimewatendea tu kile walichonitendea.” 12 Wakamwambia, “Tumekuja kukufunga na kukutia mikononi mwa Wafilisti.”Samsoni akawaambia, “Niapieni kuwa hamtaniua ninyi wenyewe.” 13 Wakamjibu, “Sisi hatutakuua, bali tutakufunga tu na kukutia mikononi mwao.” Basi wakamfunga kwa kamba mbili mpya. Wakamchukua toka huko kwenye ufa katika mwamba. 14 Alipokaribia Lehi, Wafilisti wakamjia wakipiga kelele. Roho wa BWANA akamjia juu yake kwa nguvu. Kamba zilizomfunga mikono yake zikawa kama kitani iliyochomwa kwa moto, na vifungo vyake vikaanguka chini toka mikononi mwake. 15 Ndipo akaona mfupa mpya wa taya la punda, akanyoosha mkono, akauchukua na kuua nao Wafilisti wapatao 1,000. 16 Ndipo Samsoni akasema,“Kwa taya la pundamalundo juu ya malundo.Kwa taya la pundanimeua watu 1,000.” 17 Alipomaliza kusema, akautupa ule mfupa wa taya; na mahali pale pakaitwa Ramath-Lehi. 18 Kwa kuwa alikuwa amesikia kiu sana, akamlilia BWANA akisema, “Umempa mtumishi wako ushindi huu mkuu. Je, sasa nife kwa kiu na kuangukia mikononi mwa hawa watu wasiotahiriwa?” 19 BWANA akafunua shimo huko Lehi, pakatoka maji. Samsoni alipoyanywa, nguvu zikamrudia na kuhuika. Hivyo chemchemi ile ikaitwa En-Hakore, nayo iko mpaka leo huko Lehi. 20 Samsoni akawa mwamuzi wa Waisraeli katika siku za Wafilisti kwa muda wa miaka ishirini.

In Other Versions

Judges 15 in the ANGEFD

Judges 15 in the ANTPNG2D

Judges 15 in the AS21

Judges 15 in the BAGH

Judges 15 in the BBPNG

Judges 15 in the BBT1E

Judges 15 in the BDS

Judges 15 in the BEV

Judges 15 in the BHAD

Judges 15 in the BIB

Judges 15 in the BLPT

Judges 15 in the BNT

Judges 15 in the BNTABOOT

Judges 15 in the BNTLV

Judges 15 in the BOATCB

Judges 15 in the BOATCB2

Judges 15 in the BOBCV

Judges 15 in the BOCNT

Judges 15 in the BOECS

Judges 15 in the BOGWICC

Judges 15 in the BOHCB

Judges 15 in the BOHCV

Judges 15 in the BOHLNT

Judges 15 in the BOHNTLTAL

Judges 15 in the BOICB

Judges 15 in the BOILNTAP

Judges 15 in the BOITCV

Judges 15 in the BOKCV2

Judges 15 in the BOKHWOG

Judges 15 in the BOKSSV

Judges 15 in the BOLCB

Judges 15 in the BOLCB2

Judges 15 in the BOMCV

Judges 15 in the BONAV

Judges 15 in the BONCB

Judges 15 in the BONLT

Judges 15 in the BONUT2

Judges 15 in the BOPLNT

Judges 15 in the BOSCB

Judges 15 in the BOSNC

Judges 15 in the BOTLNT

Judges 15 in the BOVCB

Judges 15 in the BOYCB

Judges 15 in the BPBB

Judges 15 in the BPH

Judges 15 in the BSB

Judges 15 in the CCB

Judges 15 in the CUV

Judges 15 in the CUVS

Judges 15 in the DBT

Judges 15 in the DGDNT

Judges 15 in the DHNT

Judges 15 in the DNT

Judges 15 in the ELBE

Judges 15 in the EMTV

Judges 15 in the ESV

Judges 15 in the FBV

Judges 15 in the FEB

Judges 15 in the GGMNT

Judges 15 in the GNT

Judges 15 in the HARY

Judges 15 in the HNT

Judges 15 in the IRVA

Judges 15 in the IRVB

Judges 15 in the IRVG

Judges 15 in the IRVH

Judges 15 in the IRVK

Judges 15 in the IRVM

Judges 15 in the IRVM2

Judges 15 in the IRVO

Judges 15 in the IRVP

Judges 15 in the IRVT

Judges 15 in the IRVT2

Judges 15 in the IRVU

Judges 15 in the ISVN

Judges 15 in the JSNT

Judges 15 in the KAPI

Judges 15 in the KBT1ETNIK

Judges 15 in the KBV

Judges 15 in the KJV

Judges 15 in the KNFD

Judges 15 in the LBA

Judges 15 in the LBLA

Judges 15 in the LNT

Judges 15 in the LSV

Judges 15 in the MAAL

Judges 15 in the MBV

Judges 15 in the MBV2

Judges 15 in the MHNT

Judges 15 in the MKNFD

Judges 15 in the MNG

Judges 15 in the MNT

Judges 15 in the MNT2

Judges 15 in the MRS1T

Judges 15 in the NAA

Judges 15 in the NASB

Judges 15 in the NBLA

Judges 15 in the NBS

Judges 15 in the NBVTP

Judges 15 in the NET2

Judges 15 in the NIV11

Judges 15 in the NNT

Judges 15 in the NNT2

Judges 15 in the NNT3

Judges 15 in the PDDPT

Judges 15 in the PFNT

Judges 15 in the RMNT

Judges 15 in the SBIAS

Judges 15 in the SBIBS

Judges 15 in the SBIBS2

Judges 15 in the SBICS

Judges 15 in the SBIDS

Judges 15 in the SBIGS

Judges 15 in the SBIHS

Judges 15 in the SBIIS

Judges 15 in the SBIIS2

Judges 15 in the SBIIS3

Judges 15 in the SBIKS

Judges 15 in the SBIKS2

Judges 15 in the SBIMS

Judges 15 in the SBIOS

Judges 15 in the SBIPS

Judges 15 in the SBISS

Judges 15 in the SBITS

Judges 15 in the SBITS2

Judges 15 in the SBITS3

Judges 15 in the SBITS4

Judges 15 in the SBIUS

Judges 15 in the SBIVS

Judges 15 in the SBT

Judges 15 in the SBT1E

Judges 15 in the SCHL

Judges 15 in the SNT

Judges 15 in the SUSU

Judges 15 in the SUSU2

Judges 15 in the SYNO

Judges 15 in the TBIAOTANT

Judges 15 in the TBT1E

Judges 15 in the TBT1E2

Judges 15 in the TFTIP

Judges 15 in the TFTU

Judges 15 in the TGNTATF3T

Judges 15 in the THAI

Judges 15 in the TNFD

Judges 15 in the TNT

Judges 15 in the TNTIK

Judges 15 in the TNTIL

Judges 15 in the TNTIN

Judges 15 in the TNTIP

Judges 15 in the TNTIZ

Judges 15 in the TOMA

Judges 15 in the TTENT

Judges 15 in the UBG

Judges 15 in the UGV

Judges 15 in the UGV2

Judges 15 in the UGV3

Judges 15 in the VBL

Judges 15 in the VDCC

Judges 15 in the YALU

Judges 15 in the YAPE

Judges 15 in the YBVTP

Judges 15 in the ZBP