John 15 (BOKCV)

1 “Mimi ndimi mzabibu wa kweli na Baba yangu ndiye mkulima. 2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, Baba yangu hulikata, nalo kila tawi lizaalo, hulisafisha ili lipate kuzaa matunda zaidi. 3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililonena nanyi. 4 Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda lisipokaa ndani ya mzabibu, vivyo hivyo ninyi msipokaa ndani yangu hamwezi kuzaa matunda. 5 “Mimi ni mzabibu, ninyi ni matawi. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa sana, maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya jambo lolote. 6 Mtu yeyote asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka. Matawi kama hayo hukusanywa na kutupwa motoni, yakateketea. 7 Ninyi mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni lolote mtakalo, nanyi mtatendewa. 8 Kwa hiyo Baba yangu hutukuzwa, kwa vile mzaavyo matunda mengi, nanyi mtakuwa wanafunzi wangu. 9 “Kama vile Baba alivyonipenda mimi, hivyo ndivyo mimi nilivyowapenda ninyi. Basi kaeni katika pendo langu. 10 Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake. 11 Nimewaambia mambo haya ili furaha yangu iwe ndani yenu na furaha yenu iwe kamili. 12 Amri yangu ndiyo hii: Mpendane kama mimi nilivyowapenda ninyi. 13 Hakuna mtu mwenye upendo mkuu kuliko huu, mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake. 14 Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru. 15 Siwaiti ninyi watumishi tena, kwa sababu watumishi hawajui bwana wao analofanya, bali nimewaita ninyi rafiki, kwa maana nimewajulisha mambo yote niliyoyasikia kutoka kwa Baba yangu. 16 Si ninyi mlionichagua, bali mimi ndiye niliyewachagua ninyi na kuwaweka mwende mkazae matunda, na matunda yenu yapate kudumu. Ili nalo lolote mtakalomwomba Baba katika Jina langu, awape ninyi. 17 Amri yangu ndiyo hii: Mpendane. 18 “Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba ulinichukia mimi kabla yenu. 19 Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungeliwapenda kama vile unavyowapenda walio wake. Kwa sababu ninyi si wa ulimwengu, lakini mimi nimewachagua kutoka ulimwengu, hii ndiyo sababu ulimwengu unawachukia. 20 Kumbukeni lile neno nililowaambia, ‘Hakuna mtumishi aliye mkuu kuliko bwana wake.’ Kama wamenitesa mimi, nanyi pia watawatesa. Kama wamelishika neno langu, watalishika na neno lenu pia. 21 Watawatendea ninyi haya yote kwa ajili ya Jina langu, kwa sababu hawamjui yeye aliyenituma. 22 Kama sikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa hawana udhuru kwa ajili ya dhambi zao. 23 Yeyote anayenichukia mimi, anamchukia pia na Baba yangu. 24 Kama sikuwa nimefanya miujiza ambayo haijapata kufanywa na mtu mwingine yeyote, wasingalikuwa na hatia ya dhambi. Lakini sasa wameiona miujiza hii na bado wakatuchukia mimi na Baba yangu. 25 Lakini hii ni kutimiza lile neno lililoandikwa kwenye Sheria kwamba, ‘Walinichukia pasipo sababu.’ 26 “Lakini atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, yaani, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi. 27 Ninyi nanyi itawapasa kushuhudia kwa sababu mmekuwa pamoja nami tangu mwanzo.

In Other Versions

John 15 in the ANGEFD

John 15 in the ANTPNG2D

John 15 in the AS21

John 15 in the BAGH

John 15 in the BBPNG

John 15 in the BBT1E

John 15 in the BDS

John 15 in the BEV

John 15 in the BHAD

John 15 in the BIB

John 15 in the BLPT

John 15 in the BNT

John 15 in the BNTABOOT

John 15 in the BNTLV

John 15 in the BOATCB

John 15 in the BOATCB2

John 15 in the BOBCV

John 15 in the BOCNT

John 15 in the BOECS

John 15 in the BOGWICC

John 15 in the BOHCB

John 15 in the BOHCV

John 15 in the BOHLNT

John 15 in the BOHNTLTAL

John 15 in the BOICB

John 15 in the BOILNTAP

John 15 in the BOITCV

John 15 in the BOKCV2

John 15 in the BOKHWOG

John 15 in the BOKSSV

John 15 in the BOLCB

John 15 in the BOLCB2

John 15 in the BOMCV

John 15 in the BONAV

John 15 in the BONCB

John 15 in the BONLT

John 15 in the BONUT2

John 15 in the BOPLNT

John 15 in the BOSCB

John 15 in the BOSNC

John 15 in the BOTLNT

John 15 in the BOVCB

John 15 in the BOYCB

John 15 in the BPBB

John 15 in the BPH

John 15 in the BSB

John 15 in the CCB

John 15 in the CUV

John 15 in the CUVS

John 15 in the DBT

John 15 in the DGDNT

John 15 in the DHNT

John 15 in the DNT

John 15 in the ELBE

John 15 in the EMTV

John 15 in the ESV

John 15 in the FBV

John 15 in the FEB

John 15 in the GGMNT

John 15 in the GNT

John 15 in the HARY

John 15 in the HNT

John 15 in the IRVA

John 15 in the IRVB

John 15 in the IRVG

John 15 in the IRVH

John 15 in the IRVK

John 15 in the IRVM

John 15 in the IRVM2

John 15 in the IRVO

John 15 in the IRVP

John 15 in the IRVT

John 15 in the IRVT2

John 15 in the IRVU

John 15 in the ISVN

John 15 in the JSNT

John 15 in the KAPI

John 15 in the KBT1ETNIK

John 15 in the KBV

John 15 in the KJV

John 15 in the KNFD

John 15 in the LBA

John 15 in the LBLA

John 15 in the LNT

John 15 in the LSV

John 15 in the MAAL

John 15 in the MBV

John 15 in the MBV2

John 15 in the MHNT

John 15 in the MKNFD

John 15 in the MNG

John 15 in the MNT

John 15 in the MNT2

John 15 in the MRS1T

John 15 in the NAA

John 15 in the NASB

John 15 in the NBLA

John 15 in the NBS

John 15 in the NBVTP

John 15 in the NET2

John 15 in the NIV11

John 15 in the NNT

John 15 in the NNT2

John 15 in the NNT3

John 15 in the PDDPT

John 15 in the PFNT

John 15 in the RMNT

John 15 in the SBIAS

John 15 in the SBIBS

John 15 in the SBIBS2

John 15 in the SBICS

John 15 in the SBIDS

John 15 in the SBIGS

John 15 in the SBIHS

John 15 in the SBIIS

John 15 in the SBIIS2

John 15 in the SBIIS3

John 15 in the SBIKS

John 15 in the SBIKS2

John 15 in the SBIMS

John 15 in the SBIOS

John 15 in the SBIPS

John 15 in the SBISS

John 15 in the SBITS

John 15 in the SBITS2

John 15 in the SBITS3

John 15 in the SBITS4

John 15 in the SBIUS

John 15 in the SBIVS

John 15 in the SBT

John 15 in the SBT1E

John 15 in the SCHL

John 15 in the SNT

John 15 in the SUSU

John 15 in the SUSU2

John 15 in the SYNO

John 15 in the TBIAOTANT

John 15 in the TBT1E

John 15 in the TBT1E2

John 15 in the TFTIP

John 15 in the TFTU

John 15 in the TGNTATF3T

John 15 in the THAI

John 15 in the TNFD

John 15 in the TNT

John 15 in the TNTIK

John 15 in the TNTIL

John 15 in the TNTIN

John 15 in the TNTIP

John 15 in the TNTIZ

John 15 in the TOMA

John 15 in the TTENT

John 15 in the UBG

John 15 in the UGV

John 15 in the UGV2

John 15 in the UGV3

John 15 in the VBL

John 15 in the VDCC

John 15 in the YALU

John 15 in the YAPE

John 15 in the YBVTP

John 15 in the ZBP