Matthew 16 (BOKCV)

1 Mafarisayo na Masadukayo wakamjia Yesu na kumjaribu kwa kumwomba awaonyeshe ishara kutoka mbinguni. 2 Yesu akawajibu, “Ifikapo jioni, mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa kuwa anga ni nyekundu.’ 3 Nanyi wakati wa asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule kuonekana kwa anga, lakini hamwezi kupambanua dalili za nyakati. 4 Kizazi kiovu na cha uzinzi kinatafuta ishara, lakini hakitapewa ishara yoyote isipokuwa ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda zake. 5 Wanafunzi wake walipofika ngʼambo ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua mikate. 6 Yesu akawaambia, “Jihadharini. Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya Masadukayo.” 7 Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema, “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.” 8 Yesu, akifahamu majadiliano yao, akauliza, “Enyi wa imani haba! Mbona mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa na mikate? 9 Je, bado hamwelewi? Je, hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu 5,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya? 10 Au ile mikate saba iliyolisha watu 4,000 na idadi ya vikapu vingapi vya mabaki mlivyokusanya? 11 Inakuwaje mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya Mafarisayo na Masadukayo.” 12 Ndipo wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo. 13 Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu husema kwamba mimi Mwana wa Adamu ni nani?” 14 Wakamjibu, “Baadhi husema ni Yohana Mbatizaji; wengine husema ni Eliya; na bado wengine husema ni Yeremia au mmojawapo wa manabii.” 15 Akawauliza, “Je, ninyi mnasema mimi ni nani?” 16 Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.” 17 Naye Yesu akamwambia, “Heri wewe, Simoni Bar-Yona, kwa maana hili halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na Baba yangu aliye mbinguni. 18 Nami nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata malango ya Kuzimu hayataweza kulishinda. 19 Nitakupa funguo za Ufalme wa mbinguni, na lolote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, nalo lolote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.” 20 Kisha akawakataza wanafunzi wake wasimwambie mtu yeyote kwamba yeye ndiye Kristo. 21 Tangu wakati huo, Yesu alianza kuwaeleza wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda Yerusalemu na kupata mateso mengi mikononi mwa wazee, viongozi wa makuhani, na walimu wa sheria, na kwamba itampasa auawe lakini siku ya tatu kufufuliwa. 22 Petro akamchukua kando, akaanza kumkemea akisema, “Haiwezekani, Bwana! Jambo hili kamwe halitakupata!” 23 Lakini Yesu akageuka na kumwambia Petro, “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.” 24 Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Mtu yeyote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane mwenyewe, auchukue msalaba wake, anifuate. 25 Kwa maana yeyote anayetaka kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini yeyote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili yangu atayapata. 26 Kwa maana, je, itamfaidi nini mtu kuupata ulimwengu wote, lakini akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 27 Kwa maana Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake, naye ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 28 Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa Adamu akija katika Ufalme wake.”

In Other Versions

Matthew 16 in the ANGEFD

Matthew 16 in the ANTPNG2D

Matthew 16 in the AS21

Matthew 16 in the BAGH

Matthew 16 in the BBPNG

Matthew 16 in the BBT1E

Matthew 16 in the BDS

Matthew 16 in the BEV

Matthew 16 in the BHAD

Matthew 16 in the BIB

Matthew 16 in the BLPT

Matthew 16 in the BNT

Matthew 16 in the BNTABOOT

Matthew 16 in the BNTLV

Matthew 16 in the BOATCB

Matthew 16 in the BOATCB2

Matthew 16 in the BOBCV

Matthew 16 in the BOCNT

Matthew 16 in the BOECS

Matthew 16 in the BOGWICC

Matthew 16 in the BOHCB

Matthew 16 in the BOHCV

Matthew 16 in the BOHLNT

Matthew 16 in the BOHNTLTAL

Matthew 16 in the BOICB

Matthew 16 in the BOILNTAP

Matthew 16 in the BOITCV

Matthew 16 in the BOKCV2

Matthew 16 in the BOKHWOG

Matthew 16 in the BOKSSV

Matthew 16 in the BOLCB

Matthew 16 in the BOLCB2

Matthew 16 in the BOMCV

Matthew 16 in the BONAV

Matthew 16 in the BONCB

Matthew 16 in the BONLT

Matthew 16 in the BONUT2

Matthew 16 in the BOPLNT

Matthew 16 in the BOSCB

Matthew 16 in the BOSNC

Matthew 16 in the BOTLNT

Matthew 16 in the BOVCB

Matthew 16 in the BOYCB

Matthew 16 in the BPBB

Matthew 16 in the BPH

Matthew 16 in the BSB

Matthew 16 in the CCB

Matthew 16 in the CUV

Matthew 16 in the CUVS

Matthew 16 in the DBT

Matthew 16 in the DGDNT

Matthew 16 in the DHNT

Matthew 16 in the DNT

Matthew 16 in the ELBE

Matthew 16 in the EMTV

Matthew 16 in the ESV

Matthew 16 in the FBV

Matthew 16 in the FEB

Matthew 16 in the GGMNT

Matthew 16 in the GNT

Matthew 16 in the HARY

Matthew 16 in the HNT

Matthew 16 in the IRVA

Matthew 16 in the IRVB

Matthew 16 in the IRVG

Matthew 16 in the IRVH

Matthew 16 in the IRVK

Matthew 16 in the IRVM

Matthew 16 in the IRVM2

Matthew 16 in the IRVO

Matthew 16 in the IRVP

Matthew 16 in the IRVT

Matthew 16 in the IRVT2

Matthew 16 in the IRVU

Matthew 16 in the ISVN

Matthew 16 in the JSNT

Matthew 16 in the KAPI

Matthew 16 in the KBT1ETNIK

Matthew 16 in the KBV

Matthew 16 in the KJV

Matthew 16 in the KNFD

Matthew 16 in the LBA

Matthew 16 in the LBLA

Matthew 16 in the LNT

Matthew 16 in the LSV

Matthew 16 in the MAAL

Matthew 16 in the MBV

Matthew 16 in the MBV2

Matthew 16 in the MHNT

Matthew 16 in the MKNFD

Matthew 16 in the MNG

Matthew 16 in the MNT

Matthew 16 in the MNT2

Matthew 16 in the MRS1T

Matthew 16 in the NAA

Matthew 16 in the NASB

Matthew 16 in the NBLA

Matthew 16 in the NBS

Matthew 16 in the NBVTP

Matthew 16 in the NET2

Matthew 16 in the NIV11

Matthew 16 in the NNT

Matthew 16 in the NNT2

Matthew 16 in the NNT3

Matthew 16 in the PDDPT

Matthew 16 in the PFNT

Matthew 16 in the RMNT

Matthew 16 in the SBIAS

Matthew 16 in the SBIBS

Matthew 16 in the SBIBS2

Matthew 16 in the SBICS

Matthew 16 in the SBIDS

Matthew 16 in the SBIGS

Matthew 16 in the SBIHS

Matthew 16 in the SBIIS

Matthew 16 in the SBIIS2

Matthew 16 in the SBIIS3

Matthew 16 in the SBIKS

Matthew 16 in the SBIKS2

Matthew 16 in the SBIMS

Matthew 16 in the SBIOS

Matthew 16 in the SBIPS

Matthew 16 in the SBISS

Matthew 16 in the SBITS

Matthew 16 in the SBITS2

Matthew 16 in the SBITS3

Matthew 16 in the SBITS4

Matthew 16 in the SBIUS

Matthew 16 in the SBIVS

Matthew 16 in the SBT

Matthew 16 in the SBT1E

Matthew 16 in the SCHL

Matthew 16 in the SNT

Matthew 16 in the SUSU

Matthew 16 in the SUSU2

Matthew 16 in the SYNO

Matthew 16 in the TBIAOTANT

Matthew 16 in the TBT1E

Matthew 16 in the TBT1E2

Matthew 16 in the TFTIP

Matthew 16 in the TFTU

Matthew 16 in the TGNTATF3T

Matthew 16 in the THAI

Matthew 16 in the TNFD

Matthew 16 in the TNT

Matthew 16 in the TNTIK

Matthew 16 in the TNTIL

Matthew 16 in the TNTIN

Matthew 16 in the TNTIP

Matthew 16 in the TNTIZ

Matthew 16 in the TOMA

Matthew 16 in the TTENT

Matthew 16 in the UBG

Matthew 16 in the UGV

Matthew 16 in the UGV2

Matthew 16 in the UGV3

Matthew 16 in the VBL

Matthew 16 in the VDCC

Matthew 16 in the YALU

Matthew 16 in the YAPE

Matthew 16 in the YBVTP

Matthew 16 in the ZBP