Revelation 14 (BOKCV)

1 Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao. 2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao. 3 Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani. 4 Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo. 5 Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote. 6 Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. 7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.” 8 Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.” 9 Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake, 10 yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo. 11 Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” 12 Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu. 13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.”“Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.” 14 Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake. 15 Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.” 16 Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa. 17 Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali. 18 Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.” 19 Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu. 20 Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.

In Other Versions

Revelation 14 in the ANGEFD

Revelation 14 in the ANTPNG2D

Revelation 14 in the AS21

Revelation 14 in the BAGH

Revelation 14 in the BBPNG

Revelation 14 in the BBT1E

Revelation 14 in the BDS

Revelation 14 in the BEV

Revelation 14 in the BHAD

Revelation 14 in the BIB

Revelation 14 in the BLPT

Revelation 14 in the BNT

Revelation 14 in the BNTABOOT

Revelation 14 in the BNTLV

Revelation 14 in the BOATCB

Revelation 14 in the BOATCB2

Revelation 14 in the BOBCV

Revelation 14 in the BOCNT

Revelation 14 in the BOECS

Revelation 14 in the BOGWICC

Revelation 14 in the BOHCB

Revelation 14 in the BOHCV

Revelation 14 in the BOHLNT

Revelation 14 in the BOHNTLTAL

Revelation 14 in the BOICB

Revelation 14 in the BOILNTAP

Revelation 14 in the BOITCV

Revelation 14 in the BOKCV2

Revelation 14 in the BOKHWOG

Revelation 14 in the BOKSSV

Revelation 14 in the BOLCB

Revelation 14 in the BOLCB2

Revelation 14 in the BOMCV

Revelation 14 in the BONAV

Revelation 14 in the BONCB

Revelation 14 in the BONLT

Revelation 14 in the BONUT2

Revelation 14 in the BOPLNT

Revelation 14 in the BOSCB

Revelation 14 in the BOSNC

Revelation 14 in the BOTLNT

Revelation 14 in the BOVCB

Revelation 14 in the BOYCB

Revelation 14 in the BPBB

Revelation 14 in the BPH

Revelation 14 in the BSB

Revelation 14 in the CCB

Revelation 14 in the CUV

Revelation 14 in the CUVS

Revelation 14 in the DBT

Revelation 14 in the DGDNT

Revelation 14 in the DHNT

Revelation 14 in the DNT

Revelation 14 in the ELBE

Revelation 14 in the EMTV

Revelation 14 in the ESV

Revelation 14 in the FBV

Revelation 14 in the FEB

Revelation 14 in the GGMNT

Revelation 14 in the GNT

Revelation 14 in the HARY

Revelation 14 in the HNT

Revelation 14 in the IRVA

Revelation 14 in the IRVB

Revelation 14 in the IRVG

Revelation 14 in the IRVH

Revelation 14 in the IRVK

Revelation 14 in the IRVM

Revelation 14 in the IRVM2

Revelation 14 in the IRVO

Revelation 14 in the IRVP

Revelation 14 in the IRVT

Revelation 14 in the IRVT2

Revelation 14 in the IRVU

Revelation 14 in the ISVN

Revelation 14 in the JSNT

Revelation 14 in the KAPI

Revelation 14 in the KBT1ETNIK

Revelation 14 in the KBV

Revelation 14 in the KJV

Revelation 14 in the KNFD

Revelation 14 in the LBA

Revelation 14 in the LBLA

Revelation 14 in the LNT

Revelation 14 in the LSV

Revelation 14 in the MAAL

Revelation 14 in the MBV

Revelation 14 in the MBV2

Revelation 14 in the MHNT

Revelation 14 in the MKNFD

Revelation 14 in the MNG

Revelation 14 in the MNT

Revelation 14 in the MNT2

Revelation 14 in the MRS1T

Revelation 14 in the NAA

Revelation 14 in the NASB

Revelation 14 in the NBLA

Revelation 14 in the NBS

Revelation 14 in the NBVTP

Revelation 14 in the NET2

Revelation 14 in the NIV11

Revelation 14 in the NNT

Revelation 14 in the NNT2

Revelation 14 in the NNT3

Revelation 14 in the PDDPT

Revelation 14 in the PFNT

Revelation 14 in the RMNT

Revelation 14 in the SBIAS

Revelation 14 in the SBIBS

Revelation 14 in the SBIBS2

Revelation 14 in the SBICS

Revelation 14 in the SBIDS

Revelation 14 in the SBIGS

Revelation 14 in the SBIHS

Revelation 14 in the SBIIS

Revelation 14 in the SBIIS2

Revelation 14 in the SBIIS3

Revelation 14 in the SBIKS

Revelation 14 in the SBIKS2

Revelation 14 in the SBIMS

Revelation 14 in the SBIOS

Revelation 14 in the SBIPS

Revelation 14 in the SBISS

Revelation 14 in the SBITS

Revelation 14 in the SBITS2

Revelation 14 in the SBITS3

Revelation 14 in the SBITS4

Revelation 14 in the SBIUS

Revelation 14 in the SBIVS

Revelation 14 in the SBT

Revelation 14 in the SBT1E

Revelation 14 in the SCHL

Revelation 14 in the SNT

Revelation 14 in the SUSU

Revelation 14 in the SUSU2

Revelation 14 in the SYNO

Revelation 14 in the TBIAOTANT

Revelation 14 in the TBT1E

Revelation 14 in the TBT1E2

Revelation 14 in the TFTIP

Revelation 14 in the TFTU

Revelation 14 in the TGNTATF3T

Revelation 14 in the THAI

Revelation 14 in the TNFD

Revelation 14 in the TNT

Revelation 14 in the TNTIK

Revelation 14 in the TNTIL

Revelation 14 in the TNTIN

Revelation 14 in the TNTIP

Revelation 14 in the TNTIZ

Revelation 14 in the TOMA

Revelation 14 in the TTENT

Revelation 14 in the UBG

Revelation 14 in the UGV

Revelation 14 in the UGV2

Revelation 14 in the UGV3

Revelation 14 in the VBL

Revelation 14 in the VDCC

Revelation 14 in the YALU

Revelation 14 in the YAPE

Revelation 14 in the YBVTP

Revelation 14 in the ZBP