Psalms 78 (BOKCV)

undefined Utenzi wa Asafu. 1 Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu,sikilizeni maneno ya kinywa changu. 2 Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo,nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale: 3 yale ambayo tuliyasikia na kuyajua,yale ambayo baba zetu walituambia. 4 Hatutayaficha kwa watoto wao;tutakiambia kizazi kijachomatendo yastahiliyo sifa ya BWANA,uweza wake, na maajabu aliyoyafanya. 5 Aliagiza amri kwa Yakobona akaweka sheria katika Israeli,ambazo aliwaamuru baba zetuwawafundishe watoto wao, 6 ili kizazi kijacho kizijue,pamoja na watoto ambao watazaliwa,nao pia wapate kuwaeleza watoto wao. 7 Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu,nao wasingesahau matendo yake,bali wangalizishika amri zake. 8 Ili wasifanane na baba zao,waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi,ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake,ambao roho zao hazikumwamini. 9 Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde,walikimbia siku ya vita. 10 Hawakulishika agano la Munguna walikataa kuishi kwa sheria yake. 11 Walisahau aliyokuwa ameyatenda,maajabu aliyokuwa amewaonyesha. 12 Alitenda miujiza machoni mwa baba zao,huko Soani, katika nchi ya Misri. 13 Aliigawanya bahari akawapitisha,alifanya maji yasimame imara kama ukuta. 14 Aliwaongoza kwa wingu mchanana kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha. 15 Alipasua miamba jangwanina akawapa maji tele kama bahari, 16 alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka,akayafanya maji yatiririke kama mito. 17 Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake,wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana. 18 Kwa makusudi walimjaribu Mungu,wakidai vyakula walivyovitamani. 19 Walinena dhidi ya Mungu, wakisema,“Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani? 20 Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu,vijito vikatiririka maji mengi.Lakini je, aweza kutupa chakula pia?Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?” 21 BWANA alipowasikia, alikasirika sana,moto wake ukawa dhidi ya Yakobo,na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli, 22 kwa kuwa hawakumwamini Mungu,wala kuutumainia ukombozi wake. 23 Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juuna kufungua milango ya mbingu, 24 akawanyeshea mana ili watu wale;aliwapa nafaka ya mbinguni. 25 Watu walikula mkate wa malaika,akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula. 26 Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbinguna kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake. 27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi,ndege warukao kama mchanga wa pwani. 28 Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao,kuzunguka mahema yao yote. 29 Walikula na kusaza,kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani. 30 Kabla hawajamaliza kula walichokitamani,hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao, 31 hasira ya Mungu ikawaka juu yao,akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao,akiwaangusha vijana wa Israeli. 32 Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi,licha ya maajabu yake, hawakuamini. 33 Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatilina miaka yao katika vitisho. 34 Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao,waliosalia walimtafuta,walimgeukia tena kwa shauku. 35 Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao,kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao. 36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao,wakisema uongo kwa ndimi zao, 37 mioyo yao haikuwa thabiti kwake,wala hawakuwa waaminifu katika agano lake. 38 Hata hivyo alikuwa na huruma,alisamehe maovu yaona hakuwaangamiza.Mara kwa mara alizuia hasira yake,wala hakuchochea ghadhabu yake yote. 39 Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu,upepo upitao ambao haurudi. 40 Mara ngapi walimwasi jangwanina kumhuzunisha nyikani! 41 Walimjaribu Mungu mara kwa mara,wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli. 42 Hawakukumbuka uwezo wake,siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi, 43 siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri,maajabu yake huko Soani. 44 Aligeuza mito yao kuwa damu,hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao. 45 Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala,na vyura wakawaharibu. 46 Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao,mazao yao kwa nzige. 47 Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawena mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji. 48 Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe,akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi. 49 Aliwafungulia hasira yake kali,ghadhabu yake, hasira na uadui,na kundi la malaika wa kuharibu. 50 Aliitengenezea njia hasira yake,hakuwaepusha na kifo,bali aliwaachia tauni. 51 Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu. 52 Lakini aliwatoa watu wake kama kundi,akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani. 53 Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa,bali bahari iliwameza adui zao. 54 Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu,hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa. 55 Aliyafukuza mataifa mbele yao,na kuwagawia nchi zao kama urithi,aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao. 56 Lakini wao walimjaribu Mungu,na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana,wala hawakuzishika sheria zake. 57 Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu,wakawa wasioweza kutegemewakama upinde wenye kasoro. 58 Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu,wakachochea wivu wake kwa sanamu zao. 59 Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana,akamkataa Israeli kabisa. 60 Akaiacha hema ya Shilo,hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu. 61 Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani,utukufu wake mikononi mwa adui. 62 Aliachia watu wake wauawe kwa upanga,akaukasirikia sana urithi wake. 63 Moto uliwaangamiza vijana wao,na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi, 64 makuhani wao waliuawa kwa upanga,wala wajane wao hawakuweza kulia. 65 Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini,kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo. 66 Aliwapiga na kuwashinda adui zake,akawatia katika aibu ya milele. 67 Ndipo alipozikataa hema za Yosefu,hakulichagua kabila la Efraimu, 68 lakini alilichagua kabila la Yuda,Mlima Sayuni, ambao aliupenda. 69 Alijenga patakatifu pake kama vilele,kama dunia ambayo aliimarisha milele. 70 Akamchagua Daudi mtumishi wakena kumtoa kwenye mazizi ya kondoo. 71 Kutoka kuchunga kondoo alimletakuwa mchungaji wa watu wake Yakobo,wa Israeli urithi wake. 72 Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo,kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

In Other Versions

Psalms 78 in the ANGEFD

Psalms 78 in the ANTPNG2D

Psalms 78 in the AS21

Psalms 78 in the BAGH

Psalms 78 in the BBPNG

Psalms 78 in the BBT1E

Psalms 78 in the BDS

Psalms 78 in the BEV

Psalms 78 in the BHAD

Psalms 78 in the BIB

Psalms 78 in the BLPT

Psalms 78 in the BNT

Psalms 78 in the BNTABOOT

Psalms 78 in the BNTLV

Psalms 78 in the BOATCB

Psalms 78 in the BOATCB2

Psalms 78 in the BOBCV

Psalms 78 in the BOCNT

Psalms 78 in the BOECS

Psalms 78 in the BOGWICC

Psalms 78 in the BOHCB

Psalms 78 in the BOHCV

Psalms 78 in the BOHLNT

Psalms 78 in the BOHNTLTAL

Psalms 78 in the BOICB

Psalms 78 in the BOILNTAP

Psalms 78 in the BOITCV

Psalms 78 in the BOKCV2

Psalms 78 in the BOKHWOG

Psalms 78 in the BOKSSV

Psalms 78 in the BOLCB

Psalms 78 in the BOLCB2

Psalms 78 in the BOMCV

Psalms 78 in the BONAV

Psalms 78 in the BONCB

Psalms 78 in the BONLT

Psalms 78 in the BONUT2

Psalms 78 in the BOPLNT

Psalms 78 in the BOSCB

Psalms 78 in the BOSNC

Psalms 78 in the BOTLNT

Psalms 78 in the BOVCB

Psalms 78 in the BOYCB

Psalms 78 in the BPBB

Psalms 78 in the BPH

Psalms 78 in the BSB

Psalms 78 in the CCB

Psalms 78 in the CUV

Psalms 78 in the CUVS

Psalms 78 in the DBT

Psalms 78 in the DGDNT

Psalms 78 in the DHNT

Psalms 78 in the DNT

Psalms 78 in the ELBE

Psalms 78 in the EMTV

Psalms 78 in the ESV

Psalms 78 in the FBV

Psalms 78 in the FEB

Psalms 78 in the GGMNT

Psalms 78 in the GNT

Psalms 78 in the HARY

Psalms 78 in the HNT

Psalms 78 in the IRVA

Psalms 78 in the IRVB

Psalms 78 in the IRVG

Psalms 78 in the IRVH

Psalms 78 in the IRVK

Psalms 78 in the IRVM

Psalms 78 in the IRVM2

Psalms 78 in the IRVO

Psalms 78 in the IRVP

Psalms 78 in the IRVT

Psalms 78 in the IRVT2

Psalms 78 in the IRVU

Psalms 78 in the ISVN

Psalms 78 in the JSNT

Psalms 78 in the KAPI

Psalms 78 in the KBT1ETNIK

Psalms 78 in the KBV

Psalms 78 in the KJV

Psalms 78 in the KNFD

Psalms 78 in the LBA

Psalms 78 in the LBLA

Psalms 78 in the LNT

Psalms 78 in the LSV

Psalms 78 in the MAAL

Psalms 78 in the MBV

Psalms 78 in the MBV2

Psalms 78 in the MHNT

Psalms 78 in the MKNFD

Psalms 78 in the MNG

Psalms 78 in the MNT

Psalms 78 in the MNT2

Psalms 78 in the MRS1T

Psalms 78 in the NAA

Psalms 78 in the NASB

Psalms 78 in the NBLA

Psalms 78 in the NBS

Psalms 78 in the NBVTP

Psalms 78 in the NET2

Psalms 78 in the NIV11

Psalms 78 in the NNT

Psalms 78 in the NNT2

Psalms 78 in the NNT3

Psalms 78 in the PDDPT

Psalms 78 in the PFNT

Psalms 78 in the RMNT

Psalms 78 in the SBIAS

Psalms 78 in the SBIBS

Psalms 78 in the SBIBS2

Psalms 78 in the SBICS

Psalms 78 in the SBIDS

Psalms 78 in the SBIGS

Psalms 78 in the SBIHS

Psalms 78 in the SBIIS

Psalms 78 in the SBIIS2

Psalms 78 in the SBIIS3

Psalms 78 in the SBIKS

Psalms 78 in the SBIKS2

Psalms 78 in the SBIMS

Psalms 78 in the SBIOS

Psalms 78 in the SBIPS

Psalms 78 in the SBISS

Psalms 78 in the SBITS

Psalms 78 in the SBITS2

Psalms 78 in the SBITS3

Psalms 78 in the SBITS4

Psalms 78 in the SBIUS

Psalms 78 in the SBIVS

Psalms 78 in the SBT

Psalms 78 in the SBT1E

Psalms 78 in the SCHL

Psalms 78 in the SNT

Psalms 78 in the SUSU

Psalms 78 in the SUSU2

Psalms 78 in the SYNO

Psalms 78 in the TBIAOTANT

Psalms 78 in the TBT1E

Psalms 78 in the TBT1E2

Psalms 78 in the TFTIP

Psalms 78 in the TFTU

Psalms 78 in the TGNTATF3T

Psalms 78 in the THAI

Psalms 78 in the TNFD

Psalms 78 in the TNT

Psalms 78 in the TNTIK

Psalms 78 in the TNTIL

Psalms 78 in the TNTIN

Psalms 78 in the TNTIP

Psalms 78 in the TNTIZ

Psalms 78 in the TOMA

Psalms 78 in the TTENT

Psalms 78 in the UBG

Psalms 78 in the UGV

Psalms 78 in the UGV2

Psalms 78 in the UGV3

Psalms 78 in the VBL

Psalms 78 in the VDCC

Psalms 78 in the YALU

Psalms 78 in the YAPE

Psalms 78 in the YBVTP

Psalms 78 in the ZBP