Zechariah 14 (BOKCV)

1 Siku ya BWANA inakuja ambayo nyara zilizotekwa kwenu zitagawanywa miongoni mwenu. 2 Nitayakusanya mataifa yote huko Yerusalemu kupigana dhidi yake, mji utatekwa, nyumba zitavamiwa na kuporwa na wanawake watanajisiwa. Nusu ya mji watakwenda uhamishoni, lakini watakaobaki hawataondolewa kutoka mjini. 3 Kisha BWANA atatoka na kupigana dhidi ya watu wa yale mataifa, kama apiganavyo siku ya vita. 4 Siku hiyo miguu yake itasimama juu ya Mlima wa Mizeituni, mashariki mwa Yerusalemu, nao Mlima wa Mizeituni utagawanyika mara mbili kuanzia mashariki hadi magharibi, ukifanya bonde kubwa, nusu ya mlima ukisogea kuelekea kaskazini na nusu kuelekea kusini. 5 Nanyi mtakimbia kupitia katika bonde hilo la mlima wangu kwa kuwa litaenea hadi Aseli. Mtakimbia kama mlivyokimbia tetemeko la ardhi katika siku za Uzia mfalme wa Yuda. Kisha BWANA Mungu wangu atakuja na watakatifu wote pamoja naye. 6 Siku hiyo hakutakuwepo nuru, baridi wala theluji. 7 Itakuwa siku ya kipekee, isiyo na mchana wala usiku, siku ijulikanayo na BWANA. Jioni inapofika nuru itakuwepo. 8 Siku hiyo, maji yaliyo hai yatatiririka kutoka Yerusalemu, nusu kwenda kwenye bahari ya mashariki, na nusu kwenda kwenye bahari ya magharibi wakati wa kiangazi na wakati wa masika. 9 BWANA atakuwa mfalme juu ya dunia yote. Katika siku hiyo atakuwepo BWANA mmoja na jina lake litakuwa jina pekee. 10 Nchi yote kuanzia Geba, kaskazini mwa Yuda, hadi Rimoni, kusini mwa Yerusalemu, itakuwa kama Araba. Lakini Yerusalemu utainuliwa juu na kubaki mahali pake, toka Lango la Benyamini hadi mahali pa Lango la Kwanza, mpaka kwenye Lango la Pembeni na kutoka Mnara wa Hananeli hadi kwenye mashinikizo ya divai ya mfalme. 11 Utakaliwa na watu, kamwe hautaharibiwa tena, Yerusalemu utakaa salama. 12 Hii ndiyo tauni ambayo BWANA atapiga nayo mataifa yote ambayo yalipigana dhidi ya Yerusalemu: Nyama ya miili yao itaoza wangali wamesimama kwa miguu yao, macho yao yataoza kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza vinywani mwao. 13 Katika siku hiyo BWANA atawatia wanaume hofu kuu. Kila mwanaume atakamata mkono wa mwenzake nao watashambuliana. 14 Yuda pia atapigana katika Yerusalemu. Utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka Yerusalemu utakusanywa, wingi wa dhahabu, fedha na nguo. 15 Tauni ya aina iyo hiyo itapiga farasi na nyumbu, ngamia na punda, nao wanyama wote walioko kwenye kambi za adui. 16 Kisha walionusurika katika mataifa yote ambayo yaliushambulia Yerusalemu watakuwa wakipanda Yerusalemu kila mwaka kumwabudu Mfalme, BWANA Mwenye Nguvu Zote na kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 17 Ikiwa taifa lolote la dunia hawatakwenda Yerusalemu kumwabudu Mfalme, BWANA Mwenye Nguvu Zote, mvua haitanyesha kwao. 18 Ikiwa watu wa Misri nao hawatakwenda kushiriki, hawatapata mvua. BWANA ataleta juu yao tauni ile ambayo itawapiga mataifa yale ambayo hayatakwenda kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 19 Hii itakuwa adhabu ya Misri na adhabu ya mataifa yote yale ambayo hayatakwenda Yerusalemu kuadhimisha Sikukuu ya Vibanda. 20 Katika siku hiyo, kengele zilizofungwa kwenye farasi zitaandikwa maneno haya: TAKATIFU KWA BWANA, navyo vyungu vya kupikia katika nyumba ya BWANA vitakuwa kama bakuli takatifu mbele ya madhabahu. 21 Kila chungu kilichoko Yerusalemu na Yuda kitakuwa kitakatifu kwa BWANA Mwenye Nguvu Zote na wote wanaokuja kutoa dhabihu watachukua baadhi ya vyungu hivyo na kupikia. Katika siku hiyo hatakuwepo tena mfanyabiashara katika nyumba ya BWANA Mwenye Nguvu Zote.

In Other Versions

Zechariah 14 in the ANGEFD

Zechariah 14 in the ANTPNG2D

Zechariah 14 in the AS21

Zechariah 14 in the BAGH

Zechariah 14 in the BBPNG

Zechariah 14 in the BBT1E

Zechariah 14 in the BDS

Zechariah 14 in the BEV

Zechariah 14 in the BHAD

Zechariah 14 in the BIB

Zechariah 14 in the BLPT

Zechariah 14 in the BNT

Zechariah 14 in the BNTABOOT

Zechariah 14 in the BNTLV

Zechariah 14 in the BOATCB

Zechariah 14 in the BOATCB2

Zechariah 14 in the BOBCV

Zechariah 14 in the BOCNT

Zechariah 14 in the BOECS

Zechariah 14 in the BOGWICC

Zechariah 14 in the BOHCB

Zechariah 14 in the BOHCV

Zechariah 14 in the BOHLNT

Zechariah 14 in the BOHNTLTAL

Zechariah 14 in the BOICB

Zechariah 14 in the BOILNTAP

Zechariah 14 in the BOITCV

Zechariah 14 in the BOKCV2

Zechariah 14 in the BOKHWOG

Zechariah 14 in the BOKSSV

Zechariah 14 in the BOLCB

Zechariah 14 in the BOLCB2

Zechariah 14 in the BOMCV

Zechariah 14 in the BONAV

Zechariah 14 in the BONCB

Zechariah 14 in the BONLT

Zechariah 14 in the BONUT2

Zechariah 14 in the BOPLNT

Zechariah 14 in the BOSCB

Zechariah 14 in the BOSNC

Zechariah 14 in the BOTLNT

Zechariah 14 in the BOVCB

Zechariah 14 in the BOYCB

Zechariah 14 in the BPBB

Zechariah 14 in the BPH

Zechariah 14 in the BSB

Zechariah 14 in the CCB

Zechariah 14 in the CUV

Zechariah 14 in the CUVS

Zechariah 14 in the DBT

Zechariah 14 in the DGDNT

Zechariah 14 in the DHNT

Zechariah 14 in the DNT

Zechariah 14 in the ELBE

Zechariah 14 in the EMTV

Zechariah 14 in the ESV

Zechariah 14 in the FBV

Zechariah 14 in the FEB

Zechariah 14 in the GGMNT

Zechariah 14 in the GNT

Zechariah 14 in the HARY

Zechariah 14 in the HNT

Zechariah 14 in the IRVA

Zechariah 14 in the IRVB

Zechariah 14 in the IRVG

Zechariah 14 in the IRVH

Zechariah 14 in the IRVK

Zechariah 14 in the IRVM

Zechariah 14 in the IRVM2

Zechariah 14 in the IRVO

Zechariah 14 in the IRVP

Zechariah 14 in the IRVT

Zechariah 14 in the IRVT2

Zechariah 14 in the IRVU

Zechariah 14 in the ISVN

Zechariah 14 in the JSNT

Zechariah 14 in the KAPI

Zechariah 14 in the KBT1ETNIK

Zechariah 14 in the KBV

Zechariah 14 in the KJV

Zechariah 14 in the KNFD

Zechariah 14 in the LBA

Zechariah 14 in the LBLA

Zechariah 14 in the LNT

Zechariah 14 in the LSV

Zechariah 14 in the MAAL

Zechariah 14 in the MBV

Zechariah 14 in the MBV2

Zechariah 14 in the MHNT

Zechariah 14 in the MKNFD

Zechariah 14 in the MNG

Zechariah 14 in the MNT

Zechariah 14 in the MNT2

Zechariah 14 in the MRS1T

Zechariah 14 in the NAA

Zechariah 14 in the NASB

Zechariah 14 in the NBLA

Zechariah 14 in the NBS

Zechariah 14 in the NBVTP

Zechariah 14 in the NET2

Zechariah 14 in the NIV11

Zechariah 14 in the NNT

Zechariah 14 in the NNT2

Zechariah 14 in the NNT3

Zechariah 14 in the PDDPT

Zechariah 14 in the PFNT

Zechariah 14 in the RMNT

Zechariah 14 in the SBIAS

Zechariah 14 in the SBIBS

Zechariah 14 in the SBIBS2

Zechariah 14 in the SBICS

Zechariah 14 in the SBIDS

Zechariah 14 in the SBIGS

Zechariah 14 in the SBIHS

Zechariah 14 in the SBIIS

Zechariah 14 in the SBIIS2

Zechariah 14 in the SBIIS3

Zechariah 14 in the SBIKS

Zechariah 14 in the SBIKS2

Zechariah 14 in the SBIMS

Zechariah 14 in the SBIOS

Zechariah 14 in the SBIPS

Zechariah 14 in the SBISS

Zechariah 14 in the SBITS

Zechariah 14 in the SBITS2

Zechariah 14 in the SBITS3

Zechariah 14 in the SBITS4

Zechariah 14 in the SBIUS

Zechariah 14 in the SBIVS

Zechariah 14 in the SBT

Zechariah 14 in the SBT1E

Zechariah 14 in the SCHL

Zechariah 14 in the SNT

Zechariah 14 in the SUSU

Zechariah 14 in the SUSU2

Zechariah 14 in the SYNO

Zechariah 14 in the TBIAOTANT

Zechariah 14 in the TBT1E

Zechariah 14 in the TBT1E2

Zechariah 14 in the TFTIP

Zechariah 14 in the TFTU

Zechariah 14 in the TGNTATF3T

Zechariah 14 in the THAI

Zechariah 14 in the TNFD

Zechariah 14 in the TNT

Zechariah 14 in the TNTIK

Zechariah 14 in the TNTIL

Zechariah 14 in the TNTIN

Zechariah 14 in the TNTIP

Zechariah 14 in the TNTIZ

Zechariah 14 in the TOMA

Zechariah 14 in the TTENT

Zechariah 14 in the UBG

Zechariah 14 in the UGV

Zechariah 14 in the UGV2

Zechariah 14 in the UGV3

Zechariah 14 in the VBL

Zechariah 14 in the VDCC

Zechariah 14 in the YALU

Zechariah 14 in the YAPE

Zechariah 14 in the YBVTP

Zechariah 14 in the ZBP