Deuteronomy 23 (BOKCV)

1 Asiingie mtu yeyote aliyehasiwa kwa kupondwa makende au kwa kukatwa uume wake katika kusanyiko la BWANA. 2 Mtu yeyote ambaye amezaliwa kwenye ndoa isiyo halali au wazao wake wasiingie kwenye kusanyiko la BWANA, hata mpaka kizazi cha kumi. 3 Hapatakuwa na Mwamoni au Mmoabu au yeyote wa wazao wao atakayeruhusiwa kuingia katika kusanyiko la BWANA, hata mpaka kizazi cha kumi. 4 Kwa kuwa hawakuja kuwalaki wakiwa na mkate na maji mlipokuwa njiani mlipotoka Misri, tena walimwajiri Balaamu mwana wa Beori kutoka Pethori iliyoko Aramu-Naharaimu ili kuwalaani ninyi. 5 Hata hivyo, BWANA Mungu wenu hakumsikiliza Balaamu bali aligeuza laana kuwa baraka kwenu kwa sababu BWANA Mungu wenu anawapenda. 6 Msitafute mapatano ya urafiki nao maisha yenu yote. 7 Usimchukie Mwedomu, kwa kuwa yeye ni ndugu yako. Usimchukie Mmisri, kwa sababu uliishi kama mgeni katika nchi yake. 8 Kizazi cha tatu cha watoto watakaozaliwa nao wanaweza kuingia katika kusanyiko la BWANA. 9 Unapokuwa umepiga kambi dhidi ya adui zako, jitenge na kitu chochote kisicho safi. 10 Ikiwa mtu amechafuka kwa sababu ya kutokwa na shahawa usiku, inampasa atoke nje ya kambi na kukaa huko. 11 Lakini jioni ikikaribia ataoga, na baada ya jua kuzama ataingia tena kambini. 12 Tengeni mahali nje ya kambi ambapo mnaweza kwenda kujisaidia. 13 Kama sehemu ya vifaa vyenu kuweni na kitu cha kulimia, nanyi mnapojisaidia, chimba shimo na kisha funika kile kikutokacho. 14 Kwa kuwa BWANA Mungu wenu hutembea katika kambi yenu ili kuwalinda na kuwaweka adui zenu mikononi mwenu. Kambi yenu ni lazima iwe takatifu, ili asione kitu chochote miongoni mwenu kilicho kichafu akageuka na kuwaacha. 15 Ikiwa mtumwa amekimbilia kwako, usimrudishe kwa bwana wake. 16 Mwache aishi miongoni mwenu mahali popote anapopapenda na katika mji wowote anaochagua. Usimwonee. 17 Asiwepo Mwisraeli mwanamke kahaba au mwanaume hanithi wa mahali pa kuabudia miungu. 18 Kamwe usilete mapato ya ukahaba ikiwa ni ya mwanamke au ni ya mwanaume katika nyumba ya BWANA Mungu wako kwa ajili ya nadhiri yoyote, kwa sababu BWANA Mungu wako anachukizwa na yote mawili. 19 Usimtoze ndugu yako riba, iwe ni fedha ama chakula ama kitu kingine chochote ambacho waweza kupata riba juu yake. 20 Unaweza kumtoza mgeni riba, lakini siyo nduguyo Mwisraeli, ili kwamba BWANA Mungu wako akubariki katika kila kitu unachoweka mkono katika nchi unayoingia kuimiliki. 21 Ukiweka nadhiri kwa BWANA Mungu wako, usichelewe kuitimiza, kwa kuwa BWANA Mungu wako atakudai, nawe utakuwa na hatia ya dhambi. 22 Lakini ukijizuia kuweka nadhiri, hutakuwa na hatia. 23 Chochote kitakachotamkwa kwa midomo yako ni lazima uhakikishe umekifanya, kwa sababu uliweka nadhiri yako kwa hiari mbele za BWANA Mungu wako kwa kinywa chako mwenyewe. 24 Kama ukiingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu kadiri utakavyo, lakini usiweke chochote kwenye kikapu chako. 25 Kama ukiingia katika shamba la nafaka la jirani yako, unaweza kukwanyua kwa mikono yako, lakini usikate kwa mundu nafaka iliyosimama.

In Other Versions

Deuteronomy 23 in the ANGEFD

Deuteronomy 23 in the ANTPNG2D

Deuteronomy 23 in the AS21

Deuteronomy 23 in the BAGH

Deuteronomy 23 in the BBPNG

Deuteronomy 23 in the BBT1E

Deuteronomy 23 in the BDS

Deuteronomy 23 in the BEV

Deuteronomy 23 in the BHAD

Deuteronomy 23 in the BIB

Deuteronomy 23 in the BLPT

Deuteronomy 23 in the BNT

Deuteronomy 23 in the BNTABOOT

Deuteronomy 23 in the BNTLV

Deuteronomy 23 in the BOATCB

Deuteronomy 23 in the BOATCB2

Deuteronomy 23 in the BOBCV

Deuteronomy 23 in the BOCNT

Deuteronomy 23 in the BOECS

Deuteronomy 23 in the BOGWICC

Deuteronomy 23 in the BOHCB

Deuteronomy 23 in the BOHCV

Deuteronomy 23 in the BOHLNT

Deuteronomy 23 in the BOHNTLTAL

Deuteronomy 23 in the BOICB

Deuteronomy 23 in the BOILNTAP

Deuteronomy 23 in the BOITCV

Deuteronomy 23 in the BOKCV2

Deuteronomy 23 in the BOKHWOG

Deuteronomy 23 in the BOKSSV

Deuteronomy 23 in the BOLCB

Deuteronomy 23 in the BOLCB2

Deuteronomy 23 in the BOMCV

Deuteronomy 23 in the BONAV

Deuteronomy 23 in the BONCB

Deuteronomy 23 in the BONLT

Deuteronomy 23 in the BONUT2

Deuteronomy 23 in the BOPLNT

Deuteronomy 23 in the BOSCB

Deuteronomy 23 in the BOSNC

Deuteronomy 23 in the BOTLNT

Deuteronomy 23 in the BOVCB

Deuteronomy 23 in the BOYCB

Deuteronomy 23 in the BPBB

Deuteronomy 23 in the BPH

Deuteronomy 23 in the BSB

Deuteronomy 23 in the CCB

Deuteronomy 23 in the CUV

Deuteronomy 23 in the CUVS

Deuteronomy 23 in the DBT

Deuteronomy 23 in the DGDNT

Deuteronomy 23 in the DHNT

Deuteronomy 23 in the DNT

Deuteronomy 23 in the ELBE

Deuteronomy 23 in the EMTV

Deuteronomy 23 in the ESV

Deuteronomy 23 in the FBV

Deuteronomy 23 in the FEB

Deuteronomy 23 in the GGMNT

Deuteronomy 23 in the GNT

Deuteronomy 23 in the HARY

Deuteronomy 23 in the HNT

Deuteronomy 23 in the IRVA

Deuteronomy 23 in the IRVB

Deuteronomy 23 in the IRVG

Deuteronomy 23 in the IRVH

Deuteronomy 23 in the IRVK

Deuteronomy 23 in the IRVM

Deuteronomy 23 in the IRVM2

Deuteronomy 23 in the IRVO

Deuteronomy 23 in the IRVP

Deuteronomy 23 in the IRVT

Deuteronomy 23 in the IRVT2

Deuteronomy 23 in the IRVU

Deuteronomy 23 in the ISVN

Deuteronomy 23 in the JSNT

Deuteronomy 23 in the KAPI

Deuteronomy 23 in the KBT1ETNIK

Deuteronomy 23 in the KBV

Deuteronomy 23 in the KJV

Deuteronomy 23 in the KNFD

Deuteronomy 23 in the LBA

Deuteronomy 23 in the LBLA

Deuteronomy 23 in the LNT

Deuteronomy 23 in the LSV

Deuteronomy 23 in the MAAL

Deuteronomy 23 in the MBV

Deuteronomy 23 in the MBV2

Deuteronomy 23 in the MHNT

Deuteronomy 23 in the MKNFD

Deuteronomy 23 in the MNG

Deuteronomy 23 in the MNT

Deuteronomy 23 in the MNT2

Deuteronomy 23 in the MRS1T

Deuteronomy 23 in the NAA

Deuteronomy 23 in the NASB

Deuteronomy 23 in the NBLA

Deuteronomy 23 in the NBS

Deuteronomy 23 in the NBVTP

Deuteronomy 23 in the NET2

Deuteronomy 23 in the NIV11

Deuteronomy 23 in the NNT

Deuteronomy 23 in the NNT2

Deuteronomy 23 in the NNT3

Deuteronomy 23 in the PDDPT

Deuteronomy 23 in the PFNT

Deuteronomy 23 in the RMNT

Deuteronomy 23 in the SBIAS

Deuteronomy 23 in the SBIBS

Deuteronomy 23 in the SBIBS2

Deuteronomy 23 in the SBICS

Deuteronomy 23 in the SBIDS

Deuteronomy 23 in the SBIGS

Deuteronomy 23 in the SBIHS

Deuteronomy 23 in the SBIIS

Deuteronomy 23 in the SBIIS2

Deuteronomy 23 in the SBIIS3

Deuteronomy 23 in the SBIKS

Deuteronomy 23 in the SBIKS2

Deuteronomy 23 in the SBIMS

Deuteronomy 23 in the SBIOS

Deuteronomy 23 in the SBIPS

Deuteronomy 23 in the SBISS

Deuteronomy 23 in the SBITS

Deuteronomy 23 in the SBITS2

Deuteronomy 23 in the SBITS3

Deuteronomy 23 in the SBITS4

Deuteronomy 23 in the SBIUS

Deuteronomy 23 in the SBIVS

Deuteronomy 23 in the SBT

Deuteronomy 23 in the SBT1E

Deuteronomy 23 in the SCHL

Deuteronomy 23 in the SNT

Deuteronomy 23 in the SUSU

Deuteronomy 23 in the SUSU2

Deuteronomy 23 in the SYNO

Deuteronomy 23 in the TBIAOTANT

Deuteronomy 23 in the TBT1E

Deuteronomy 23 in the TBT1E2

Deuteronomy 23 in the TFTIP

Deuteronomy 23 in the TFTU

Deuteronomy 23 in the TGNTATF3T

Deuteronomy 23 in the THAI

Deuteronomy 23 in the TNFD

Deuteronomy 23 in the TNT

Deuteronomy 23 in the TNTIK

Deuteronomy 23 in the TNTIL

Deuteronomy 23 in the TNTIN

Deuteronomy 23 in the TNTIP

Deuteronomy 23 in the TNTIZ

Deuteronomy 23 in the TOMA

Deuteronomy 23 in the TTENT

Deuteronomy 23 in the UBG

Deuteronomy 23 in the UGV

Deuteronomy 23 in the UGV2

Deuteronomy 23 in the UGV3

Deuteronomy 23 in the VBL

Deuteronomy 23 in the VDCC

Deuteronomy 23 in the YALU

Deuteronomy 23 in the YAPE

Deuteronomy 23 in the YBVTP

Deuteronomy 23 in the ZBP