Isaiah 43 (BOKCV)

1 Lakini sasa hili ndilo asemalo BWANA,yeye aliyekuumba, ee Yakobo,yeye aliyekuhuluku, ee Israeli:“Usiogope kwa maana nimekukomboa,nimekuita wewe kwa jina lako, wewe u wangu. 2 Unapopita kwenye maji makuu,nitakuwa pamoja nawe,unapopita katika mito ya maji,hayatakugharikisha.Utakapopita katika moto,hutaungua,miali ya moto haitakuunguza. 3 Kwa kuwa Mimi ndimi BWANA, Mungu wako,yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako.Ninaitoa Misri kuwa fidia yako,Kushi na Seba badala yako. 4 Kwa kuwa wewe ni wa thamani na wa kuheshimiwa machoni pangu,nami kwa kuwa ninakupenda,nitatoa watu badala yakona mataifa badala ya maisha yako. 5 Usiogope, kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe,nitawaleta watoto wako kutoka mashariki,na kukukusanya kutoka magharibi. 6 Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’nayo kusini, ‘Usiwazuie.’Walete wana wangu kutoka mbali,na binti zangu kutoka miisho ya dunia: 7 kila mmoja ambaye ameitwa kwa Jina langu,niliyemuumba kwa utukufu wangu,niliyemhuluku na kumfanya.” 8 Uwaongoze wale wenye macho lakini hawaoni,wenye masikio lakini hawasikii. 9 Mataifa yote yanakutanika pamoja,na makabila yanakusanyika.Ni nani miongoni mwao aliyetangulia kutuambia haya,na kututangazia mambo yaliyopita?Walete mashahidi wao ili kuwathibitisha kuwa walikuwa sahihi,ili wengine waweze kusikia, waseme, “Ni kweli.” 10 “Ninyi ni mashahidi wangu,” asema BWANA,“na mtumishi wangu niliyemchagua,ili mpate kunijua na kuniamini,na kutambua kwamba Mimi ndiye.Kabla yangu hakuna mungu aliyefanyizwa,wala hatakuwepo mwingine baada yangu. 11 Mimi, naam mimi, ndimi BWANA,zaidi yangu hakuna mwokozi. 12 Nimedhihirisha, kuokoa na kutangaza:Mimi, wala si mungu mgeni katikati yenu.Ninyi ni mashahidi wangu,” asema BWANA,“kwamba Mimi ndimi Mungu. 13 Naam, tangu siku za kale, Mimi ndiye.Hakuna hata mmoja awezaye kuokoakutoka mkononi wangu.Mimi ninapotenda,ni nani awezaye kutangua?” 14 Hili ndilo BWANA asemalo,Mkombozi wako, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli:“Kwa ajili yenu nitatumana Babelina kuwaleta Wakaldayo wote kama wakimbizi,katika meli walizozionea fahari. 15 Mimi ndimi BWANA, yeye Aliye Mtakatifu wako,Muumba wa Israeli, Mfalme wako.” 16 Hili ndilo asemalo BWANA,yeye aliyefanya njia baharini,mahali pa kupita kwenye maji mengi, 17 aliyeyakokota magari ya vita na farasi,jeshi pamoja na askari wa msaada,nao wakalala huko, wala hawatainuka tena kamwe,wakakomeshwa, na wakazimika kama utambi: 18 “Msiyakumbuke mambo yaliyopita,wala msiyatafakari mambo ya zamani. 19 Tazama, nitafanya jambo jipya!Sasa litachipuka, je, hamtalitambua?Nitafanya njia jangwanina vijito vya maji katika nchi kame. 20 Wanyama wa mwituni wataniheshimu,mbweha na bundi,kwa sababu ninawapatia maji jangwani,na vijito katika nchi kame,ili kuwapa watu wangu maji, wale niliowachagua, 21 watu wale niliowaumba kwa ajili yangu,ili wapate kutangaza sifa zangu. 22 “Hata hivyo hukuniita mimi, ee Yakobo,hujajitaabisha kwa ajili yangu, ee Israeli. 23 Hujaniletea kondoo kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa,wala kuniheshimu kwa dhabihu zako.Sikukulemea kwa sadaka za nafakawala kukuchosha kwa kuhitaji uvumba. 24 Hukuninunulia uvumba wowote wenye manukato,wala hukunipa kwa ukarimumafuta ya wanyama wa dhabihu zako.Lakini umenilemea kwa dhambi zako,na kunitaabisha kwa makosa yako. 25 “Mimi, naam mimi, ndimi nizifutaye dhambi zako,kwa ajili yangu mwenyewe,wala sizikumbuki dhambi zako tena. 26 Tafakari mambo yaliyopita,njoo na tuhojiane,leta shauri lako uweze kupewa haki yako. 27 Baba yako wa kwanza alitenda dhambi,wasemaji wako wameasi dhidi yangu. 28 Kwa hiyo nitawaaibisha wakuu wa Hekalu lako,nami nitamtoa Yakobo aangamizwe,na Israeli adhihakiwe.

In Other Versions

Isaiah 43 in the ANGEFD

Isaiah 43 in the ANTPNG2D

Isaiah 43 in the AS21

Isaiah 43 in the BAGH

Isaiah 43 in the BBPNG

Isaiah 43 in the BBT1E

Isaiah 43 in the BDS

Isaiah 43 in the BEV

Isaiah 43 in the BHAD

Isaiah 43 in the BIB

Isaiah 43 in the BLPT

Isaiah 43 in the BNT

Isaiah 43 in the BNTABOOT

Isaiah 43 in the BNTLV

Isaiah 43 in the BOATCB

Isaiah 43 in the BOATCB2

Isaiah 43 in the BOBCV

Isaiah 43 in the BOCNT

Isaiah 43 in the BOECS

Isaiah 43 in the BOGWICC

Isaiah 43 in the BOHCB

Isaiah 43 in the BOHCV

Isaiah 43 in the BOHLNT

Isaiah 43 in the BOHNTLTAL

Isaiah 43 in the BOICB

Isaiah 43 in the BOILNTAP

Isaiah 43 in the BOITCV

Isaiah 43 in the BOKCV2

Isaiah 43 in the BOKHWOG

Isaiah 43 in the BOKSSV

Isaiah 43 in the BOLCB

Isaiah 43 in the BOLCB2

Isaiah 43 in the BOMCV

Isaiah 43 in the BONAV

Isaiah 43 in the BONCB

Isaiah 43 in the BONLT

Isaiah 43 in the BONUT2

Isaiah 43 in the BOPLNT

Isaiah 43 in the BOSCB

Isaiah 43 in the BOSNC

Isaiah 43 in the BOTLNT

Isaiah 43 in the BOVCB

Isaiah 43 in the BOYCB

Isaiah 43 in the BPBB

Isaiah 43 in the BPH

Isaiah 43 in the BSB

Isaiah 43 in the CCB

Isaiah 43 in the CUV

Isaiah 43 in the CUVS

Isaiah 43 in the DBT

Isaiah 43 in the DGDNT

Isaiah 43 in the DHNT

Isaiah 43 in the DNT

Isaiah 43 in the ELBE

Isaiah 43 in the EMTV

Isaiah 43 in the ESV

Isaiah 43 in the FBV

Isaiah 43 in the FEB

Isaiah 43 in the GGMNT

Isaiah 43 in the GNT

Isaiah 43 in the HARY

Isaiah 43 in the HNT

Isaiah 43 in the IRVA

Isaiah 43 in the IRVB

Isaiah 43 in the IRVG

Isaiah 43 in the IRVH

Isaiah 43 in the IRVK

Isaiah 43 in the IRVM

Isaiah 43 in the IRVM2

Isaiah 43 in the IRVO

Isaiah 43 in the IRVP

Isaiah 43 in the IRVT

Isaiah 43 in the IRVT2

Isaiah 43 in the IRVU

Isaiah 43 in the ISVN

Isaiah 43 in the JSNT

Isaiah 43 in the KAPI

Isaiah 43 in the KBT1ETNIK

Isaiah 43 in the KBV

Isaiah 43 in the KJV

Isaiah 43 in the KNFD

Isaiah 43 in the LBA

Isaiah 43 in the LBLA

Isaiah 43 in the LNT

Isaiah 43 in the LSV

Isaiah 43 in the MAAL

Isaiah 43 in the MBV

Isaiah 43 in the MBV2

Isaiah 43 in the MHNT

Isaiah 43 in the MKNFD

Isaiah 43 in the MNG

Isaiah 43 in the MNT

Isaiah 43 in the MNT2

Isaiah 43 in the MRS1T

Isaiah 43 in the NAA

Isaiah 43 in the NASB

Isaiah 43 in the NBLA

Isaiah 43 in the NBS

Isaiah 43 in the NBVTP

Isaiah 43 in the NET2

Isaiah 43 in the NIV11

Isaiah 43 in the NNT

Isaiah 43 in the NNT2

Isaiah 43 in the NNT3

Isaiah 43 in the PDDPT

Isaiah 43 in the PFNT

Isaiah 43 in the RMNT

Isaiah 43 in the SBIAS

Isaiah 43 in the SBIBS

Isaiah 43 in the SBIBS2

Isaiah 43 in the SBICS

Isaiah 43 in the SBIDS

Isaiah 43 in the SBIGS

Isaiah 43 in the SBIHS

Isaiah 43 in the SBIIS

Isaiah 43 in the SBIIS2

Isaiah 43 in the SBIIS3

Isaiah 43 in the SBIKS

Isaiah 43 in the SBIKS2

Isaiah 43 in the SBIMS

Isaiah 43 in the SBIOS

Isaiah 43 in the SBIPS

Isaiah 43 in the SBISS

Isaiah 43 in the SBITS

Isaiah 43 in the SBITS2

Isaiah 43 in the SBITS3

Isaiah 43 in the SBITS4

Isaiah 43 in the SBIUS

Isaiah 43 in the SBIVS

Isaiah 43 in the SBT

Isaiah 43 in the SBT1E

Isaiah 43 in the SCHL

Isaiah 43 in the SNT

Isaiah 43 in the SUSU

Isaiah 43 in the SUSU2

Isaiah 43 in the SYNO

Isaiah 43 in the TBIAOTANT

Isaiah 43 in the TBT1E

Isaiah 43 in the TBT1E2

Isaiah 43 in the TFTIP

Isaiah 43 in the TFTU

Isaiah 43 in the TGNTATF3T

Isaiah 43 in the THAI

Isaiah 43 in the TNFD

Isaiah 43 in the TNT

Isaiah 43 in the TNTIK

Isaiah 43 in the TNTIL

Isaiah 43 in the TNTIN

Isaiah 43 in the TNTIP

Isaiah 43 in the TNTIZ

Isaiah 43 in the TOMA

Isaiah 43 in the TTENT

Isaiah 43 in the UBG

Isaiah 43 in the UGV

Isaiah 43 in the UGV2

Isaiah 43 in the UGV3

Isaiah 43 in the VBL

Isaiah 43 in the VDCC

Isaiah 43 in the YALU

Isaiah 43 in the YAPE

Isaiah 43 in the YBVTP

Isaiah 43 in the ZBP