James 1 (BOKCV)

1 Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo:Kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika ulimwenguni:Salamu. 2 Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali, 3 kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. 4 Saburi na iwe na kazi timilifu, ili mpate kuwa wakamilifu, mmekamilishwa, bila kupungukiwa na kitu chochote. 5 Kama mtu yeyote miongoni mwenu amepungukiwa na hekima na amwombe Mungu, yeye awapaye watu wote kwa ukarimu wala hana kinyongo, naye atapewa. 6 Lakini anapoomba, lazima aamini wala asiwe na shaka, kwa sababu mtu aliye na shaka ni kama wimbi la bahari, lililochukuliwa na upepo na kutupwa huku na huku. 7 Mtu kama huyo asidhani ya kuwa atapata kitu chochote kutoka kwa Bwana. 8 Yeye ni mtu mwenye nia mbili, mwenye kusitasita katika njia zake zote. 9 Ndugu asiye na cheo kikubwa yampasa ajivunie hali hiyo maana ametukuzwa. 10 Lakini yeye aliye tajiri afurahi kwa kuwa ameshushwa, kwa sababu atatoweka kama ua la shambani. 11 Kwa maana jua kali lenye kuchoma huchomoza na kuliunguza, likayakausha majani, na ua lake likapukutika, nao uzuri wake huharibika. Vivyo hivyo tajiri naye atanyauka akiwa anaendelea na shughuli zake. 12 Heri mtu anayevumilia wakati wa majaribu, kwa sababu akiisha kushinda hilo jaribio atapewa taji la uzima Mungu alilowaahidia wale wampendao. 13 Mtu anapojaribiwa asiseme, “Ninajaribiwa na Mungu.” Kwa maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu wala yeye hamjaribu mtu yeyote. 14 Lakini kila mtu hujaribiwa wakati anapovutwa na kudanganywa na tamaa zake mwenyewe zilizo mbaya. 15 Basi ile tamaa mbaya ikishachukua mimba, huzaa dhambi, nayo ile dhambi ikikomaa, huzaa mauti. 16 Ndugu zangu wapendwa, msidanganyike. 17 Kila kitolewacho kilicho chema na kilicho kamili, hutoka juu, na hushuka kutoka kwa Baba wa mianga, ambaye kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeukageuka. 18 Kwa mapenzi yake mwenyewe alituzaa kwa neno la kweli, kusudi tuwe kama mazao ya kwanza katika viumbe vyake vyote. 19 Ndugu zangu wapendwa, fahamuni jambo hili: Kila mtu awe mwepesi wa kusikiliza, lakini asiwe mwepesi wa kusema wala wa kukasirika. 20 Kwa maana hasira ya mwanadamu haitendi haki ya Mungu. 21 Kwa hiyo, ondoleeni mbali uchafu wote na uovu ambao umezidi kuwa mwingi, mkalipokee kwa unyenyekevu lile Neno lililopandwa ndani yenu ambalo laweza kuokoa nafsi zenu. 22 Basi kuweni watendaji wa Neno wala msiwe wasikiaji tu, huku mkijidanganya nafsi zenu. 23 Kwa maana kama mtu ni msikiaji tu wa Neno wala hatendi kile linachosema, yeye ni kama mtu ajitazamaye uso wake kwenye kioo 24 na baada ya kujiona alivyo, huenda zake na mara husahau jinsi alivyo. 25 Lakini yeye anayeangalia kwa bidii katika sheria kamilifu, ile iletayo uhuru, naye akaendelea kufanya hivyo bila kusahau alichosikia, bali akalitenda, atabarikiwa katika kile anachofanya. 26 Kama mtu akidhani ya kuwa anayo dini lakini hauzuii ulimi wake kwa hatamu, hujidanganya moyoni mwake, wala dini yake mtu huyo haifai kitu. 27 Dini iliyo safi, isiyo na uchafu, inayokubalika mbele za Mungu Baba yetu, ndiyo hii: Kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao na kujilinda usitiwe madoa na dunia.

In Other Versions

James 1 in the ANGEFD

James 1 in the ANTPNG2D

James 1 in the AS21

James 1 in the BAGH

James 1 in the BBPNG

James 1 in the BBT1E

James 1 in the BDS

James 1 in the BEV

James 1 in the BHAD

James 1 in the BIB

James 1 in the BLPT

James 1 in the BNT

James 1 in the BNTABOOT

James 1 in the BNTLV

James 1 in the BOATCB

James 1 in the BOATCB2

James 1 in the BOBCV

James 1 in the BOCNT

James 1 in the BOECS

James 1 in the BOGWICC

James 1 in the BOHCB

James 1 in the BOHCV

James 1 in the BOHLNT

James 1 in the BOHNTLTAL

James 1 in the BOICB

James 1 in the BOILNTAP

James 1 in the BOITCV

James 1 in the BOKCV2

James 1 in the BOKHWOG

James 1 in the BOKSSV

James 1 in the BOLCB

James 1 in the BOLCB2

James 1 in the BOMCV

James 1 in the BONAV

James 1 in the BONCB

James 1 in the BONLT

James 1 in the BONUT2

James 1 in the BOPLNT

James 1 in the BOSCB

James 1 in the BOSNC

James 1 in the BOTLNT

James 1 in the BOVCB

James 1 in the BOYCB

James 1 in the BPBB

James 1 in the BPH

James 1 in the BSB

James 1 in the CCB

James 1 in the CUV

James 1 in the CUVS

James 1 in the DBT

James 1 in the DGDNT

James 1 in the DHNT

James 1 in the DNT

James 1 in the ELBE

James 1 in the EMTV

James 1 in the ESV

James 1 in the FBV

James 1 in the FEB

James 1 in the GGMNT

James 1 in the GNT

James 1 in the HARY

James 1 in the HNT

James 1 in the IRVA

James 1 in the IRVB

James 1 in the IRVG

James 1 in the IRVH

James 1 in the IRVK

James 1 in the IRVM

James 1 in the IRVM2

James 1 in the IRVO

James 1 in the IRVP

James 1 in the IRVT

James 1 in the IRVT2

James 1 in the IRVU

James 1 in the ISVN

James 1 in the JSNT

James 1 in the KAPI

James 1 in the KBT1ETNIK

James 1 in the KBV

James 1 in the KJV

James 1 in the KNFD

James 1 in the LBA

James 1 in the LBLA

James 1 in the LNT

James 1 in the LSV

James 1 in the MAAL

James 1 in the MBV

James 1 in the MBV2

James 1 in the MHNT

James 1 in the MKNFD

James 1 in the MNG

James 1 in the MNT

James 1 in the MNT2

James 1 in the MRS1T

James 1 in the NAA

James 1 in the NASB

James 1 in the NBLA

James 1 in the NBS

James 1 in the NBVTP

James 1 in the NET2

James 1 in the NIV11

James 1 in the NNT

James 1 in the NNT2

James 1 in the NNT3

James 1 in the PDDPT

James 1 in the PFNT

James 1 in the RMNT

James 1 in the SBIAS

James 1 in the SBIBS

James 1 in the SBIBS2

James 1 in the SBICS

James 1 in the SBIDS

James 1 in the SBIGS

James 1 in the SBIHS

James 1 in the SBIIS

James 1 in the SBIIS2

James 1 in the SBIIS3

James 1 in the SBIKS

James 1 in the SBIKS2

James 1 in the SBIMS

James 1 in the SBIOS

James 1 in the SBIPS

James 1 in the SBISS

James 1 in the SBITS

James 1 in the SBITS2

James 1 in the SBITS3

James 1 in the SBITS4

James 1 in the SBIUS

James 1 in the SBIVS

James 1 in the SBT

James 1 in the SBT1E

James 1 in the SCHL

James 1 in the SNT

James 1 in the SUSU

James 1 in the SUSU2

James 1 in the SYNO

James 1 in the TBIAOTANT

James 1 in the TBT1E

James 1 in the TBT1E2

James 1 in the TFTIP

James 1 in the TFTU

James 1 in the TGNTATF3T

James 1 in the THAI

James 1 in the TNFD

James 1 in the TNT

James 1 in the TNTIK

James 1 in the TNTIL

James 1 in the TNTIN

James 1 in the TNTIP

James 1 in the TNTIZ

James 1 in the TOMA

James 1 in the TTENT

James 1 in the UBG

James 1 in the UGV

James 1 in the UGV2

James 1 in the UGV3

James 1 in the VBL

James 1 in the VDCC

James 1 in the YALU

James 1 in the YAPE

James 1 in the YBVTP

James 1 in the ZBP