Jeremiah 15 (BOKCV)

1 Kisha BWANA akaniambia: “Hata kama Mose na Samweli wangesimama mbele zangu, moyo wangu usingewaelekea watu hawa. Waondoe mbele za macho yangu! Waache waende! 2 Nao kama wakikuuliza, ‘Twende wapi?’ Waambie, ‘Hili ndilo BWANA asemalo:“ ‘Wale waliowekwa kwa ajili ya kufa, wakafe;waliowekwa kwa ajili ya upanga, kwa upanga;waliowekwa kwa ajili ya njaa, kwa njaa:waliowekwa kwa ajili ya kutekwa, watekwe.’ ” 3 BWANA asema, “Nitatuma aina nne za waharabu dhidi yao: nazo ni upanga ili kuua na mbwa ili wakokote mbali, ndege wa angani na wanyama wa nchi ili kula na kuangamiza. 4 Nitawafanya wawe machukizo kwa falme zote za dunia kwa sababu ya kile alichofanya Manase mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda huko Yerusalemu. 5 “Ni nani atakayekuhurumia, ee Yerusalemu?Ni nani atakayeomboleza kwa ajili yako?Ni nani atakayesimama ili kuulizakuhusu hali yako? 6 Umenikataa mimi,” asema BWANA.“Unazidi kukengeuka.Hivyo nitanyoosha mkono wangu juu yako na kukuangamiza,siwezi kuendelea kukuonea huruma. 7 Nitawapepeta kwa uma wa kupepeteakwenye malango ya miji katika nchi.Nitaleta msiba na maangamizi juu ya watu wangu,kwa maana hawajabadili njia zao. 8 Nitawafanya wajane wao kuwa wengikuliko mchanga wa bahari.Wakati wa adhuhuri nitamleta mharabudhidi ya mama wa vijana wao waume;kwa ghafula nitaleta juu yaomaumivu makuu na hofu kuu. 9 Mama mwenye watoto saba atazimiana kupumua pumzi yake ya mwisho.Jua lake litatua kungali bado mchana,atatahayarika na kufedheheka.Wale wote waliobaki nitawaua kwa upangambele ya adui zao,”asema BWANA. 10 Ole wangu, mama yangu, kwamba ulinizaa,mtu ambaye ulimwengu woteunashindana na kugombana naye!Sikukopa wala sikukopesha,lakini kila mmoja ananilaani. 11 BWANA akasema,“Hakika nitakuokoa kwa kusudi jema,hakika nitawafanya adui zako wakuombe msaadanyakati za maafa na nyakati za dhiki. 12 “Je, mtu aweza kuvunja chuma,chuma kitokacho kaskazini, au shaba? 13 Utajiri wako na hazina zako nitavitoa kuwa nyara,bila gharama,kwa sababu ya dhambi zako zotekatika nchi yako yote. 14 Nitakufanya uwe mtumwa wa adui zakokatika nchi usiyoijua,kwa kuwa katika hasira yangu moto umewashwautakaowaka juu yako daima.” 15 Wewe unafahamu, Ee BWANA,unikumbuke na unitunze mimi.Lipiza kisasi juu ya watesi wangu.Kwa uvumilivu wako usiniondolee mbali;kumbuka jinsi ninavyoshutumiwa. 16 Maneno yako yalipokuja, niliyala;yakawa shangwe yanguna furaha ya moyo wangu,kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako,Ee BWANA Mungu Mwenye Nguvu Zote. 17 Kamwe sikuketi katika kundi la wafanyao sherehe,wala kamwe sikujifurahisha pamoja nao;niliketi peke yangu kwa sababu mkono wako ulikuwa juu yangu,na wewe ulikuwa umenijaza hasira. 18 Kwa nini maumivu yangu hayakomi,na jeraha langu ni la kuhuzunisha,wala haliponyeki?Je, utakuwa kwangu kama kijito cha udanganyifu,kama chemchemi iliyokauka? 19 Kwa hiyo hili ndilo asemalo BWANA:“Kama ukitubu, nitakurejezaili uweze kunitumikia;kama ukinena maneno yenye maana,wala si ya upuzi,utakuwa mnenaji wangu.Watu hawa ndio watakaokugeukia,wala si wewe utakayewageukia wao. 20 Nitakufanya wewe uwe ukuta kwa watu hawa,ngome ya ukuta wa shaba;watapigana nawelakini hawatakushinda,kwa maana mimi niko pamoja nawekukuponya na kukuokoa,”asema BWANA. 21 “Nitakuokoa kutoka mikono ya waovu,na kukukomboa kutoka makucha ya watu wakatili.”

In Other Versions

Jeremiah 15 in the ANGEFD

Jeremiah 15 in the ANTPNG2D

Jeremiah 15 in the AS21

Jeremiah 15 in the BAGH

Jeremiah 15 in the BBPNG

Jeremiah 15 in the BBT1E

Jeremiah 15 in the BDS

Jeremiah 15 in the BEV

Jeremiah 15 in the BHAD

Jeremiah 15 in the BIB

Jeremiah 15 in the BLPT

Jeremiah 15 in the BNT

Jeremiah 15 in the BNTABOOT

Jeremiah 15 in the BNTLV

Jeremiah 15 in the BOATCB

Jeremiah 15 in the BOATCB2

Jeremiah 15 in the BOBCV

Jeremiah 15 in the BOCNT

Jeremiah 15 in the BOECS

Jeremiah 15 in the BOGWICC

Jeremiah 15 in the BOHCB

Jeremiah 15 in the BOHCV

Jeremiah 15 in the BOHLNT

Jeremiah 15 in the BOHNTLTAL

Jeremiah 15 in the BOICB

Jeremiah 15 in the BOILNTAP

Jeremiah 15 in the BOITCV

Jeremiah 15 in the BOKCV2

Jeremiah 15 in the BOKHWOG

Jeremiah 15 in the BOKSSV

Jeremiah 15 in the BOLCB

Jeremiah 15 in the BOLCB2

Jeremiah 15 in the BOMCV

Jeremiah 15 in the BONAV

Jeremiah 15 in the BONCB

Jeremiah 15 in the BONLT

Jeremiah 15 in the BONUT2

Jeremiah 15 in the BOPLNT

Jeremiah 15 in the BOSCB

Jeremiah 15 in the BOSNC

Jeremiah 15 in the BOTLNT

Jeremiah 15 in the BOVCB

Jeremiah 15 in the BOYCB

Jeremiah 15 in the BPBB

Jeremiah 15 in the BPH

Jeremiah 15 in the BSB

Jeremiah 15 in the CCB

Jeremiah 15 in the CUV

Jeremiah 15 in the CUVS

Jeremiah 15 in the DBT

Jeremiah 15 in the DGDNT

Jeremiah 15 in the DHNT

Jeremiah 15 in the DNT

Jeremiah 15 in the ELBE

Jeremiah 15 in the EMTV

Jeremiah 15 in the ESV

Jeremiah 15 in the FBV

Jeremiah 15 in the FEB

Jeremiah 15 in the GGMNT

Jeremiah 15 in the GNT

Jeremiah 15 in the HARY

Jeremiah 15 in the HNT

Jeremiah 15 in the IRVA

Jeremiah 15 in the IRVB

Jeremiah 15 in the IRVG

Jeremiah 15 in the IRVH

Jeremiah 15 in the IRVK

Jeremiah 15 in the IRVM

Jeremiah 15 in the IRVM2

Jeremiah 15 in the IRVO

Jeremiah 15 in the IRVP

Jeremiah 15 in the IRVT

Jeremiah 15 in the IRVT2

Jeremiah 15 in the IRVU

Jeremiah 15 in the ISVN

Jeremiah 15 in the JSNT

Jeremiah 15 in the KAPI

Jeremiah 15 in the KBT1ETNIK

Jeremiah 15 in the KBV

Jeremiah 15 in the KJV

Jeremiah 15 in the KNFD

Jeremiah 15 in the LBA

Jeremiah 15 in the LBLA

Jeremiah 15 in the LNT

Jeremiah 15 in the LSV

Jeremiah 15 in the MAAL

Jeremiah 15 in the MBV

Jeremiah 15 in the MBV2

Jeremiah 15 in the MHNT

Jeremiah 15 in the MKNFD

Jeremiah 15 in the MNG

Jeremiah 15 in the MNT

Jeremiah 15 in the MNT2

Jeremiah 15 in the MRS1T

Jeremiah 15 in the NAA

Jeremiah 15 in the NASB

Jeremiah 15 in the NBLA

Jeremiah 15 in the NBS

Jeremiah 15 in the NBVTP

Jeremiah 15 in the NET2

Jeremiah 15 in the NIV11

Jeremiah 15 in the NNT

Jeremiah 15 in the NNT2

Jeremiah 15 in the NNT3

Jeremiah 15 in the PDDPT

Jeremiah 15 in the PFNT

Jeremiah 15 in the RMNT

Jeremiah 15 in the SBIAS

Jeremiah 15 in the SBIBS

Jeremiah 15 in the SBIBS2

Jeremiah 15 in the SBICS

Jeremiah 15 in the SBIDS

Jeremiah 15 in the SBIGS

Jeremiah 15 in the SBIHS

Jeremiah 15 in the SBIIS

Jeremiah 15 in the SBIIS2

Jeremiah 15 in the SBIIS3

Jeremiah 15 in the SBIKS

Jeremiah 15 in the SBIKS2

Jeremiah 15 in the SBIMS

Jeremiah 15 in the SBIOS

Jeremiah 15 in the SBIPS

Jeremiah 15 in the SBISS

Jeremiah 15 in the SBITS

Jeremiah 15 in the SBITS2

Jeremiah 15 in the SBITS3

Jeremiah 15 in the SBITS4

Jeremiah 15 in the SBIUS

Jeremiah 15 in the SBIVS

Jeremiah 15 in the SBT

Jeremiah 15 in the SBT1E

Jeremiah 15 in the SCHL

Jeremiah 15 in the SNT

Jeremiah 15 in the SUSU

Jeremiah 15 in the SUSU2

Jeremiah 15 in the SYNO

Jeremiah 15 in the TBIAOTANT

Jeremiah 15 in the TBT1E

Jeremiah 15 in the TBT1E2

Jeremiah 15 in the TFTIP

Jeremiah 15 in the TFTU

Jeremiah 15 in the TGNTATF3T

Jeremiah 15 in the THAI

Jeremiah 15 in the TNFD

Jeremiah 15 in the TNT

Jeremiah 15 in the TNTIK

Jeremiah 15 in the TNTIL

Jeremiah 15 in the TNTIN

Jeremiah 15 in the TNTIP

Jeremiah 15 in the TNTIZ

Jeremiah 15 in the TOMA

Jeremiah 15 in the TTENT

Jeremiah 15 in the UBG

Jeremiah 15 in the UGV

Jeremiah 15 in the UGV2

Jeremiah 15 in the UGV3

Jeremiah 15 in the VBL

Jeremiah 15 in the VDCC

Jeremiah 15 in the YALU

Jeremiah 15 in the YAPE

Jeremiah 15 in the YBVTP

Jeremiah 15 in the ZBP