Jeremiah 6 (BOKCV)

1 “Kimbieni kwa usalama wenu, enyi watu wa Benyamini!Kimbieni kutoka Yerusalemu!Pigeni tarumbeta katika Tekoa!Inueni ishara juu ya Beth-Hakeremu!Kwa kuwa maafa yanaonekana yakitoka kaskazini,na uharibifu wa kutisha. 2 Nitamwangamiza Binti Sayuni,aliye mzuri sana na mwororo. 3 Wachungaji pamoja na makundi yaowatakuja dhidi yake;watapiga mahema yao kumzunguka,kila mmoja akichunga kundi lake mwenyewe.” 4 “Jiandaeni kwa vita dhidi yake!Inukeni tumshambulie mchana!Lakini, ole wetu, mchana unaisha,na vivuli vya jioni vinazidi kuwa virefu. 5 Kwa hiyo inukeni, tufanye mashambulizi usiku,na kuharibu ngome zake!” 6 Hivi ndivyo asemavyo BWANA Mwenye Nguvu Zote:“Kateni miti mjenge bomakuzunguka Yerusalemu.Mji huu ni lazima uadhibiwe,umejazwa na uonevu. 7 Kama vile kisima kinavyomwaga maji yake,ndivyo anavyomwaga uovu wake.Ukatili na maangamizi yasikika ndani yake,ugonjwa wake na majeraha yake viko mbele yangu daima. 8 Pokea onyo, ee Yerusalemu,la sivyo nitageukia mbali nawena kuifanya nchi yako kuwa ukiwa,asiweze mtu kuishi ndani yake.” 9 Hivi ndivyo asemavyo BWANA Mwenye Nguvu Zote:“Wao na wayakusanye mabaki ya Israelikwa uangalifu kama kwenye mzabibu;pitisha mkono wako kwenye matawi tena,kama yeye avunaye zabibu.” 10 Niseme na nani na kumpa onyo?Ni nani atakayenisikiliza mimi?Masikio yao yameziba,kwa hiyo hawawezi kusikia.Neno la BWANA ni chukizo kwao,hawalifurahii. 11 Lakini nimejaa ghadhabu ya BWANA,nami siwezi kuizuia. “Wamwagie watoto walioko barabarani,na juu ya vijana waume waliokusanyika;mume na mke watakumbwa pamoja ndani yake,hata nao wazee waliolemewa na miaka. 12 Nyumba zao zitapewa watu wengine,pamoja na mashamba yao na wake zao,nitakapounyoosha mkono wangudhidi ya wale waishio katika nchi,”asema BWANA. 13 “Kuanzia aliye mdogo kabisa hadi aliye mkubwa kabisa,wote wana tamaa ya kupata faida zaidi;manabii na makuhani wanafanana,wote wanafanya udanganyifu. 14 Wanafunga majeraha ya watu wangubila uangalifu.Wanasema, ‘Amani, amani,’wakati hakuna amani. 15 Je, wanaona aibu kwa ajili ya tabia yaoinayochukiza mno?Hapana, hawana aibu hata kidogo;hawajui hata kuona haya.Kwa hiyo wataanguka miongoni mwa hao walioanguka,watashushwa chini nitakapowaadhibu,”asema BWANA. 16 Hivi ndivyo asemavyo BWANA:“Simama kwenye njia panda utazame,ulizia mapito ya zamani,ulizia wapi ilipo njia nzuri, uifuate hiyo,nanyi mtapata raha nafsini mwenu.Lakini ninyi mlisema, ‘Hatutaipita hiyo.’ 17 Niliweka walinzi juu yenu na kusema,‘Sikieni sauti ya tarumbeta!’Lakini mkasema, ‘Hatutasikiliza.’ 18 Kwa hiyo sikilizeni, enyi mataifa,angalieni, enyi mashahidi,lile litakalowatokea. 19 Sikia, ee nchi:Ninaleta maafa juu ya watu hawa,matunda ya mipango yao,kwa sababu hawakusikiliza maneno yanguna wameikataa sheria yangu. 20 Unanifaa nini uvumba kutoka Sheba,au udi wa harufu nzuri kutoka nchi ya mbali?Sadaka zako za kuteketezwa hazikubaliki,dhabihu zako hazinifurahishi mimi.” 21 Kwa hiyo hivi ndivyo asemavyo BWANA:“Nitaweka vikwazo mbele ya watu hawa.Baba na wana wao watajikwaa juu yake,majirani na marafiki wataangamia.” 22 Hivi ndivyo asemavyo BWANA:“Tazama, jeshi linakujakutoka nchi ya kaskazini,taifa kubwa linaamshwakutoka miisho ya dunia. 23 Wamejifunga pinde na mkuki,ni wakatili na hawana huruma.Wanatoa sauti kama bahari inayongurumawanapoendesha farasi zao.Wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vitaili kukushambulia, ee Binti Sayuni.” 24 Tumesikia taarifa zao,nayo mikono yetu imelegea.Uchungu umetushika,maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa. 25 Usitoke kwenda mashambaniau kutembea barabarani,kwa kuwa adui ana upanga,na kuna vitisho kila upande. 26 Enyi watu wangu, vaeni maguniamjivingirishe kwenye majivu,ombolezeni kwa kilio cha uchungukama amliliaye mwana pekee,kwa maana ghafulamharabu atatujia. 27 “Nimekufanya wewe kuwa kitu cha kujaribu chuma,nao watu wangu kama mawe yenye madini,ili upate kuzijua na kuzijaribu njia zao. 28 Wote ni waasi sugu,wakienda huku na huko kusengenya.Wao ni shaba na chuma,wote wanatenda upotovu. 29 Mivuo inavuma kwa nguvu,kinachoungua kwa huo moto ni risasi,lakini pamoja na kusafisha kote huku ni bure;waovu hawaondolewi. 30 Wanaitwa fedha iliyokataliwa,kwa sababu BWANA amewakataa.”

In Other Versions

Jeremiah 6 in the ANGEFD

Jeremiah 6 in the ANTPNG2D

Jeremiah 6 in the AS21

Jeremiah 6 in the BAGH

Jeremiah 6 in the BBPNG

Jeremiah 6 in the BBT1E

Jeremiah 6 in the BDS

Jeremiah 6 in the BEV

Jeremiah 6 in the BHAD

Jeremiah 6 in the BIB

Jeremiah 6 in the BLPT

Jeremiah 6 in the BNT

Jeremiah 6 in the BNTABOOT

Jeremiah 6 in the BNTLV

Jeremiah 6 in the BOATCB

Jeremiah 6 in the BOATCB2

Jeremiah 6 in the BOBCV

Jeremiah 6 in the BOCNT

Jeremiah 6 in the BOECS

Jeremiah 6 in the BOGWICC

Jeremiah 6 in the BOHCB

Jeremiah 6 in the BOHCV

Jeremiah 6 in the BOHLNT

Jeremiah 6 in the BOHNTLTAL

Jeremiah 6 in the BOICB

Jeremiah 6 in the BOILNTAP

Jeremiah 6 in the BOITCV

Jeremiah 6 in the BOKCV2

Jeremiah 6 in the BOKHWOG

Jeremiah 6 in the BOKSSV

Jeremiah 6 in the BOLCB

Jeremiah 6 in the BOLCB2

Jeremiah 6 in the BOMCV

Jeremiah 6 in the BONAV

Jeremiah 6 in the BONCB

Jeremiah 6 in the BONLT

Jeremiah 6 in the BONUT2

Jeremiah 6 in the BOPLNT

Jeremiah 6 in the BOSCB

Jeremiah 6 in the BOSNC

Jeremiah 6 in the BOTLNT

Jeremiah 6 in the BOVCB

Jeremiah 6 in the BOYCB

Jeremiah 6 in the BPBB

Jeremiah 6 in the BPH

Jeremiah 6 in the BSB

Jeremiah 6 in the CCB

Jeremiah 6 in the CUV

Jeremiah 6 in the CUVS

Jeremiah 6 in the DBT

Jeremiah 6 in the DGDNT

Jeremiah 6 in the DHNT

Jeremiah 6 in the DNT

Jeremiah 6 in the ELBE

Jeremiah 6 in the EMTV

Jeremiah 6 in the ESV

Jeremiah 6 in the FBV

Jeremiah 6 in the FEB

Jeremiah 6 in the GGMNT

Jeremiah 6 in the GNT

Jeremiah 6 in the HARY

Jeremiah 6 in the HNT

Jeremiah 6 in the IRVA

Jeremiah 6 in the IRVB

Jeremiah 6 in the IRVG

Jeremiah 6 in the IRVH

Jeremiah 6 in the IRVK

Jeremiah 6 in the IRVM

Jeremiah 6 in the IRVM2

Jeremiah 6 in the IRVO

Jeremiah 6 in the IRVP

Jeremiah 6 in the IRVT

Jeremiah 6 in the IRVT2

Jeremiah 6 in the IRVU

Jeremiah 6 in the ISVN

Jeremiah 6 in the JSNT

Jeremiah 6 in the KAPI

Jeremiah 6 in the KBT1ETNIK

Jeremiah 6 in the KBV

Jeremiah 6 in the KJV

Jeremiah 6 in the KNFD

Jeremiah 6 in the LBA

Jeremiah 6 in the LBLA

Jeremiah 6 in the LNT

Jeremiah 6 in the LSV

Jeremiah 6 in the MAAL

Jeremiah 6 in the MBV

Jeremiah 6 in the MBV2

Jeremiah 6 in the MHNT

Jeremiah 6 in the MKNFD

Jeremiah 6 in the MNG

Jeremiah 6 in the MNT

Jeremiah 6 in the MNT2

Jeremiah 6 in the MRS1T

Jeremiah 6 in the NAA

Jeremiah 6 in the NASB

Jeremiah 6 in the NBLA

Jeremiah 6 in the NBS

Jeremiah 6 in the NBVTP

Jeremiah 6 in the NET2

Jeremiah 6 in the NIV11

Jeremiah 6 in the NNT

Jeremiah 6 in the NNT2

Jeremiah 6 in the NNT3

Jeremiah 6 in the PDDPT

Jeremiah 6 in the PFNT

Jeremiah 6 in the RMNT

Jeremiah 6 in the SBIAS

Jeremiah 6 in the SBIBS

Jeremiah 6 in the SBIBS2

Jeremiah 6 in the SBICS

Jeremiah 6 in the SBIDS

Jeremiah 6 in the SBIGS

Jeremiah 6 in the SBIHS

Jeremiah 6 in the SBIIS

Jeremiah 6 in the SBIIS2

Jeremiah 6 in the SBIIS3

Jeremiah 6 in the SBIKS

Jeremiah 6 in the SBIKS2

Jeremiah 6 in the SBIMS

Jeremiah 6 in the SBIOS

Jeremiah 6 in the SBIPS

Jeremiah 6 in the SBISS

Jeremiah 6 in the SBITS

Jeremiah 6 in the SBITS2

Jeremiah 6 in the SBITS3

Jeremiah 6 in the SBITS4

Jeremiah 6 in the SBIUS

Jeremiah 6 in the SBIVS

Jeremiah 6 in the SBT

Jeremiah 6 in the SBT1E

Jeremiah 6 in the SCHL

Jeremiah 6 in the SNT

Jeremiah 6 in the SUSU

Jeremiah 6 in the SUSU2

Jeremiah 6 in the SYNO

Jeremiah 6 in the TBIAOTANT

Jeremiah 6 in the TBT1E

Jeremiah 6 in the TBT1E2

Jeremiah 6 in the TFTIP

Jeremiah 6 in the TFTU

Jeremiah 6 in the TGNTATF3T

Jeremiah 6 in the THAI

Jeremiah 6 in the TNFD

Jeremiah 6 in the TNT

Jeremiah 6 in the TNTIK

Jeremiah 6 in the TNTIL

Jeremiah 6 in the TNTIN

Jeremiah 6 in the TNTIP

Jeremiah 6 in the TNTIZ

Jeremiah 6 in the TOMA

Jeremiah 6 in the TTENT

Jeremiah 6 in the UBG

Jeremiah 6 in the UGV

Jeremiah 6 in the UGV2

Jeremiah 6 in the UGV3

Jeremiah 6 in the VBL

Jeremiah 6 in the VDCC

Jeremiah 6 in the YALU

Jeremiah 6 in the YAPE

Jeremiah 6 in the YBVTP

Jeremiah 6 in the ZBP