Ezekiel 12 (BOKCV)
1 Neno la BWANA likanijia kusema: 2 “Mwanadamu, unaishi miongoni mwa watu waasi. Wana macho ya kuona, lakini hawaoni na masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa kuwa ni watu waasi. 3 “Kwa hiyo, mwanadamu, funga mizigo yako kwa kwenda uhamishoni tena wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toka nje na uende mahali pengine kutoka hapo ulipo. Labda wataelewa, ingawa wao ni nyumba ya kuasi. 4 Wakati wa mchana, wakiwa wanakutazama, toa nje mizigo yako iliyofungwa kwa ajili ya kwenda uhamishoni. Kisha wakati wa jioni, wakiwa wanakutazama toka nje kama wale waendao uhamishoni. 5 Wakiwa wanakutazama, toboa ukuta utolee mizigo yako hapo. 6 Beba mizigo hiyo begani mwako wakikuangalia uichukue nje wakati wa giza la jioni. Funika uso wako ili usione nchi, kwa maana nimekufanya ishara kwa nyumba ya Israeli.” 7 Basi nikafanya kama nilivyoamriwa. Wakati wa mchana nilitoa vitu vyangu nje vilivyofungwa tayari kwa uhamishoni. Kisha wakati wa jioni nikatoboa ukuta kwa mikono yangu. Nikachukua mizigo yangu nje wakati wa giza la jioni, nikiwa nimeibeba mabegani mwangu huku wakinitazama. 8 Asubuhi neno la BWANA likanijia kusema: 9 “Mwanadamu, je, nyumba ile ya kuasi ya Israeli haikukuuliza, ‘Unafanya nini?’ 10 “Waambie, ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Neno hili linamhusu mkuu aliye katika Yerusalemu na nyumba yote ya Israeli ambao wako huko.’ 11 Waambie, ‘Mimi ndiye ishara kwenu.’“Kama vile nilivyotenda, basi litatendeka vivyo hivyo kwao. Watakwenda uhamishoni kama mateka. 12 “Naye mkuu aliye miongoni mwao atabeba mizigo yake begani mwake kwenye giza la jioni na kuondoka na tundu litatobolewa ukutani kwa ajili yake ili kupitia hapo. Atafunika uso wake ili kwamba asiweze kuiona nchi. 13 Nitatandaza wavu wangu kwa ajili yake, naye atanaswa kwenye mtego wangu, nitamleta mpaka Babeli, nchi ya Wakaldayo, lakini hataiona, naye atafia huko. 14 Wote wanaomzunguka nitawatawanya pande zote, watumishi wake na majeshi yake yote, nami nitawafuatilia kwa upanga uliofutwa. 15 “Wao watajua kwamba Mimi ndimi BWANA, nitakapowatawanya miongoni mwa mataifa na kuwafukuza huku na huko katika nchi zote. 16 Lakini nitawaacha wachache wao waokoke na upanga, njaa na tauni, ili kwamba katika mataifa watakakokwenda waweze kutambua matendo ya machukizo waliotenda. Ndipo watajua kuwa Mimi ndimi BWANA.” 17 Neno la BWANA likanijia kusema: 18 “Mwanadamu, tetemeka wakati ulapo chakula chako, tetemeka kwa hofu wakati unywapo maji yako. 19 Waambie watu wa nchi: ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo kuhusu hao wanaoishi Yerusalemu na katika nchi ya Israeli: Watakula chakula chao kwa wasiwasi na kunywa maji yao kwa kufadhaika, kwa kuwa nchi yao itanyangʼanywa kila kitu chake kwa sababu ya udhalimu wa wote wanaoishi humo. 20 Miji inayokaliwa na watu itaharibiwa na nchi itakuwa ukiwa. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi ndimi BWANA.’ ” 21 Neno la BWANA likanijia kusema: 22 “Mwanadamu, ni nini hii mithali mlio nayo katika nchi ya Israeli: ‘Siku zinapita na hakuna maono yoyote yanayotimia?’ 23 Waambie, ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Nitaikomesha mithali hii, nao hawataitumia tena katika Israeli.’ Waambie, ‘Siku zimekaribia wakati kila maono yatakapotimizwa. 24 Kwa maana hapatakuwepo tena na maono ya uongo wala ubashiri wa udanganyifu miongoni mwa watu wa Israeli. 25 Lakini Mimi BWANA nitasema neno nitakalo, nalo litatimizwa bila kuchelewa. Kwa maana katika siku zako, wewe nyumba ya kuasi, nitatimiza kila nisemalo, asema BWANA Mwenyezi.’ ” 26 Neno la BWANA likanijia kusema: 27 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli inasema, ‘Maono yale anayoyaona ni kwa ajili ya miaka mingi ijayo, naye hutabiri kuhusu siku zijazo zilizo mbali.’ 28 “Kwa hiyo, waambie, ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Hakuna maneno yangu yatakayocheleweshwa tena zaidi, lolote nisemalo litatimizwa, asema BWANA Mwenyezi.’ ”
In Other Versions
Ezekiel 12 in the ANGEFD
Ezekiel 12 in the ANTPNG2D
Ezekiel 12 in the AS21
Ezekiel 12 in the BAGH
Ezekiel 12 in the BBPNG
Ezekiel 12 in the BBT1E
Ezekiel 12 in the BDS
Ezekiel 12 in the BEV
Ezekiel 12 in the BHAD
Ezekiel 12 in the BIB
Ezekiel 12 in the BLPT
Ezekiel 12 in the BNT
Ezekiel 12 in the BNTABOOT
Ezekiel 12 in the BNTLV
Ezekiel 12 in the BOATCB
Ezekiel 12 in the BOATCB2
Ezekiel 12 in the BOBCV
Ezekiel 12 in the BOCNT
Ezekiel 12 in the BOECS
Ezekiel 12 in the BOGWICC
Ezekiel 12 in the BOHCB
Ezekiel 12 in the BOHCV
Ezekiel 12 in the BOHLNT
Ezekiel 12 in the BOHNTLTAL
Ezekiel 12 in the BOICB
Ezekiel 12 in the BOILNTAP
Ezekiel 12 in the BOITCV
Ezekiel 12 in the BOKCV2
Ezekiel 12 in the BOKHWOG
Ezekiel 12 in the BOKSSV
Ezekiel 12 in the BOLCB
Ezekiel 12 in the BOLCB2
Ezekiel 12 in the BOMCV
Ezekiel 12 in the BONAV
Ezekiel 12 in the BONCB
Ezekiel 12 in the BONLT
Ezekiel 12 in the BONUT2
Ezekiel 12 in the BOPLNT
Ezekiel 12 in the BOSCB
Ezekiel 12 in the BOSNC
Ezekiel 12 in the BOTLNT
Ezekiel 12 in the BOVCB
Ezekiel 12 in the BOYCB
Ezekiel 12 in the BPBB
Ezekiel 12 in the BPH
Ezekiel 12 in the BSB
Ezekiel 12 in the CCB
Ezekiel 12 in the CUV
Ezekiel 12 in the CUVS
Ezekiel 12 in the DBT
Ezekiel 12 in the DGDNT
Ezekiel 12 in the DHNT
Ezekiel 12 in the DNT
Ezekiel 12 in the ELBE
Ezekiel 12 in the EMTV
Ezekiel 12 in the ESV
Ezekiel 12 in the FBV
Ezekiel 12 in the FEB
Ezekiel 12 in the GGMNT
Ezekiel 12 in the GNT
Ezekiel 12 in the HARY
Ezekiel 12 in the HNT
Ezekiel 12 in the IRVA
Ezekiel 12 in the IRVB
Ezekiel 12 in the IRVG
Ezekiel 12 in the IRVH
Ezekiel 12 in the IRVK
Ezekiel 12 in the IRVM
Ezekiel 12 in the IRVM2
Ezekiel 12 in the IRVO
Ezekiel 12 in the IRVP
Ezekiel 12 in the IRVT
Ezekiel 12 in the IRVT2
Ezekiel 12 in the IRVU
Ezekiel 12 in the ISVN
Ezekiel 12 in the JSNT
Ezekiel 12 in the KAPI
Ezekiel 12 in the KBT1ETNIK
Ezekiel 12 in the KBV
Ezekiel 12 in the KJV
Ezekiel 12 in the KNFD
Ezekiel 12 in the LBA
Ezekiel 12 in the LBLA
Ezekiel 12 in the LNT
Ezekiel 12 in the LSV
Ezekiel 12 in the MAAL
Ezekiel 12 in the MBV
Ezekiel 12 in the MBV2
Ezekiel 12 in the MHNT
Ezekiel 12 in the MKNFD
Ezekiel 12 in the MNG
Ezekiel 12 in the MNT
Ezekiel 12 in the MNT2
Ezekiel 12 in the MRS1T
Ezekiel 12 in the NAA
Ezekiel 12 in the NASB
Ezekiel 12 in the NBLA
Ezekiel 12 in the NBS
Ezekiel 12 in the NBVTP
Ezekiel 12 in the NET2
Ezekiel 12 in the NIV11
Ezekiel 12 in the NNT
Ezekiel 12 in the NNT2
Ezekiel 12 in the NNT3
Ezekiel 12 in the PDDPT
Ezekiel 12 in the PFNT
Ezekiel 12 in the RMNT
Ezekiel 12 in the SBIAS
Ezekiel 12 in the SBIBS
Ezekiel 12 in the SBIBS2
Ezekiel 12 in the SBICS
Ezekiel 12 in the SBIDS
Ezekiel 12 in the SBIGS
Ezekiel 12 in the SBIHS
Ezekiel 12 in the SBIIS
Ezekiel 12 in the SBIIS2
Ezekiel 12 in the SBIIS3
Ezekiel 12 in the SBIKS
Ezekiel 12 in the SBIKS2
Ezekiel 12 in the SBIMS
Ezekiel 12 in the SBIOS
Ezekiel 12 in the SBIPS
Ezekiel 12 in the SBISS
Ezekiel 12 in the SBITS
Ezekiel 12 in the SBITS2
Ezekiel 12 in the SBITS3
Ezekiel 12 in the SBITS4
Ezekiel 12 in the SBIUS
Ezekiel 12 in the SBIVS
Ezekiel 12 in the SBT
Ezekiel 12 in the SBT1E
Ezekiel 12 in the SCHL
Ezekiel 12 in the SNT
Ezekiel 12 in the SUSU
Ezekiel 12 in the SUSU2
Ezekiel 12 in the SYNO
Ezekiel 12 in the TBIAOTANT
Ezekiel 12 in the TBT1E
Ezekiel 12 in the TBT1E2
Ezekiel 12 in the TFTIP
Ezekiel 12 in the TFTU
Ezekiel 12 in the TGNTATF3T
Ezekiel 12 in the THAI
Ezekiel 12 in the TNFD
Ezekiel 12 in the TNT
Ezekiel 12 in the TNTIK
Ezekiel 12 in the TNTIL
Ezekiel 12 in the TNTIN
Ezekiel 12 in the TNTIP
Ezekiel 12 in the TNTIZ
Ezekiel 12 in the TOMA
Ezekiel 12 in the TTENT
Ezekiel 12 in the UBG
Ezekiel 12 in the UGV
Ezekiel 12 in the UGV2
Ezekiel 12 in the UGV3
Ezekiel 12 in the VBL
Ezekiel 12 in the VDCC
Ezekiel 12 in the YALU
Ezekiel 12 in the YAPE
Ezekiel 12 in the YBVTP
Ezekiel 12 in the ZBP