Ezekiel 14 (BOKCV)
1 Baadhi ya wazee wa Israeli walinijia na kuketi mbele yangu. 2 Ndipo neno la BWANA likanijia kusema: 3 “Mwanadamu, watu hawa wameweka sanamu katika mioyo yao na kuweka vitu viovu vya kukwaza mbele ya macho yao. Je, kweli niwaruhusu waniulize jambo lolote? 4 Kwa hiyo sema nao uwaambie, ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Wakati Mwisraeli yeyote anapoweka sanamu moyoni mwake na kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akaenda kwa nabii, Mimi BWANA nitamjibu peke yangu sawasawa na ukubwa wa ibada yake ya sanamu. 5 Nitafanya jambo hili ili kukamata tena mioyo ya watu wa Israeli, ambao wote wameniacha kwa ajili ya sanamu zao.’ 6 “Kwa hiyo iambie nyumba ya Israeli, ‘Hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Tubuni! Geukeni kutoka kwenye sanamu zenu na mkatae matendo yenu yote ya machukizo! 7 “ ‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi katika Israeli anapojitenga nami na kujiwekea sanamu katika moyo wake na kwa hivyo kuweka kitu kiovu cha kukwaza mbele ya macho yake na kisha akamwendea nabii kuuliza shauri kwangu, mimi BWANA nitamjibu mwenyewe. 8 Nitaukaza uso wangu dhidi ya mtu huyo na kumwadhibu na kumfanya ishara kwa watu. Nitamkatilia mbali kutoka watu wangu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi BWANA. 9 “ ‘Naye nabii kama atakuwa ameshawishika kutoa unabii, Mimi BWANA nitakuwa nimemshawishi nabii huyo, nami nitaunyoosha mkono wangu dhidi yake na kumwangamiza kutoka miongoni mwa watu wangu Israeli. 10 Watachukua hatia yao, nabii atakuwa na hatia sawa na yule mtu aliyekuja kuuliza neno kwake. 11 “ ‘Ndipo watu wa Israeli hawataniacha tena, wala kujitia unajisi tena kwa dhambi zao zote. Ndipo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao, asema BWANA Mwenyezi.’ ” 12 Neno la BWANA likanijia kusema, 13 “Mwanadamu, kama nchi itanitenda dhambi kwa kutokuwa waaminifu nami nikinyoosha mkono wangu dhidi yake kukatilia mbali upatikanaji wake wa chakula na kuipelekea njaa na kuua watu wake na wanyama wao, 14 hata kama watu hawa watatu: Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa ndani ya nchi hiyo, ndio hao tu wangeweza kujiokoa wenyewe kwa uadilifu wao, asema BWANA Mwenyezi. 15 “Au kama nikipeleka wanyama pori katika nchi hiyo yote na kuifanya isiwe na watoto, nayo ikawa ukiwa kwamba hakuna mtu apitaye katika nchi hiyo kwa sababu ya wanyama pori, 16 hakika kama niishivyo, asema BWANA Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao peke yao wangeokolewa, lakini nchi ingekuwa ukiwa. 17 “Au kama nikileta upanga dhidi ya nchi hiyo na kusema, ‘Upanga na upite katika nchi yote,’ nami nikiua watu wake na wanyama wao, 18 hakika kama niishivyo, asema BWANA Mwenyezi, hata kama watu hawa watatu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kuokoa wana wao wala binti zao. Wao wenyewe tu wangeokolewa. 19 “Au kama nikipeleka tauni katika nchi hiyo na kumwaga ghadhabu yangu juu yake kwa njia ya kumwaga damu, kuua watu wake na wanyama wao, 20 hakika kama niishivyo, asema BWANA Mwenyezi, hata kama Noa, Danieli na Ayubu wangekuwa humo ndani yake, wasingeweza kumwokoa mwana wala binti. Wao wangeweza kujiokoa wenyewe tu kwa uadilifu wao. 21 “Kwa maana hili ndilo BWANA Mwenyezi asemalo: Itakuwa vibaya kiasi gani nitakapopeleka dhidi ya Yerusalemu hukumu zangu nne za kutisha, yaani, upanga, njaa, wanyama pori na tauni, ili kuua watu wake na wanyama wao! 22 Lakini watakuwepo wenye kuokoka, wana na binti wataletwa kutoka nje ya nchi hiyo. Watawajia ninyi, nanyi mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, mtafarijika kuhusu maafa niliyoleta juu ya Yerusalemu, kwa ajili ya yale yote niliyoleta juu yake. 23 Mtafarijika wakati mtakapoona mwenendo wao na matendo yao, kwa kuwa mtajua kwamba sikufanya lolote ndani yake bila sababu, asema BWANA Mwenyezi.”
In Other Versions
Ezekiel 14 in the ANGEFD
Ezekiel 14 in the ANTPNG2D
Ezekiel 14 in the AS21
Ezekiel 14 in the BAGH
Ezekiel 14 in the BBPNG
Ezekiel 14 in the BBT1E
Ezekiel 14 in the BDS
Ezekiel 14 in the BEV
Ezekiel 14 in the BHAD
Ezekiel 14 in the BIB
Ezekiel 14 in the BLPT
Ezekiel 14 in the BNT
Ezekiel 14 in the BNTABOOT
Ezekiel 14 in the BNTLV
Ezekiel 14 in the BOATCB
Ezekiel 14 in the BOATCB2
Ezekiel 14 in the BOBCV
Ezekiel 14 in the BOCNT
Ezekiel 14 in the BOECS
Ezekiel 14 in the BOGWICC
Ezekiel 14 in the BOHCB
Ezekiel 14 in the BOHCV
Ezekiel 14 in the BOHLNT
Ezekiel 14 in the BOHNTLTAL
Ezekiel 14 in the BOICB
Ezekiel 14 in the BOILNTAP
Ezekiel 14 in the BOITCV
Ezekiel 14 in the BOKCV2
Ezekiel 14 in the BOKHWOG
Ezekiel 14 in the BOKSSV
Ezekiel 14 in the BOLCB
Ezekiel 14 in the BOLCB2
Ezekiel 14 in the BOMCV
Ezekiel 14 in the BONAV
Ezekiel 14 in the BONCB
Ezekiel 14 in the BONLT
Ezekiel 14 in the BONUT2
Ezekiel 14 in the BOPLNT
Ezekiel 14 in the BOSCB
Ezekiel 14 in the BOSNC
Ezekiel 14 in the BOTLNT
Ezekiel 14 in the BOVCB
Ezekiel 14 in the BOYCB
Ezekiel 14 in the BPBB
Ezekiel 14 in the BPH
Ezekiel 14 in the BSB
Ezekiel 14 in the CCB
Ezekiel 14 in the CUV
Ezekiel 14 in the CUVS
Ezekiel 14 in the DBT
Ezekiel 14 in the DGDNT
Ezekiel 14 in the DHNT
Ezekiel 14 in the DNT
Ezekiel 14 in the ELBE
Ezekiel 14 in the EMTV
Ezekiel 14 in the ESV
Ezekiel 14 in the FBV
Ezekiel 14 in the FEB
Ezekiel 14 in the GGMNT
Ezekiel 14 in the GNT
Ezekiel 14 in the HARY
Ezekiel 14 in the HNT
Ezekiel 14 in the IRVA
Ezekiel 14 in the IRVB
Ezekiel 14 in the IRVG
Ezekiel 14 in the IRVH
Ezekiel 14 in the IRVK
Ezekiel 14 in the IRVM
Ezekiel 14 in the IRVM2
Ezekiel 14 in the IRVO
Ezekiel 14 in the IRVP
Ezekiel 14 in the IRVT
Ezekiel 14 in the IRVT2
Ezekiel 14 in the IRVU
Ezekiel 14 in the ISVN
Ezekiel 14 in the JSNT
Ezekiel 14 in the KAPI
Ezekiel 14 in the KBT1ETNIK
Ezekiel 14 in the KBV
Ezekiel 14 in the KJV
Ezekiel 14 in the KNFD
Ezekiel 14 in the LBA
Ezekiel 14 in the LBLA
Ezekiel 14 in the LNT
Ezekiel 14 in the LSV
Ezekiel 14 in the MAAL
Ezekiel 14 in the MBV
Ezekiel 14 in the MBV2
Ezekiel 14 in the MHNT
Ezekiel 14 in the MKNFD
Ezekiel 14 in the MNG
Ezekiel 14 in the MNT
Ezekiel 14 in the MNT2
Ezekiel 14 in the MRS1T
Ezekiel 14 in the NAA
Ezekiel 14 in the NASB
Ezekiel 14 in the NBLA
Ezekiel 14 in the NBS
Ezekiel 14 in the NBVTP
Ezekiel 14 in the NET2
Ezekiel 14 in the NIV11
Ezekiel 14 in the NNT
Ezekiel 14 in the NNT2
Ezekiel 14 in the NNT3
Ezekiel 14 in the PDDPT
Ezekiel 14 in the PFNT
Ezekiel 14 in the RMNT
Ezekiel 14 in the SBIAS
Ezekiel 14 in the SBIBS
Ezekiel 14 in the SBIBS2
Ezekiel 14 in the SBICS
Ezekiel 14 in the SBIDS
Ezekiel 14 in the SBIGS
Ezekiel 14 in the SBIHS
Ezekiel 14 in the SBIIS
Ezekiel 14 in the SBIIS2
Ezekiel 14 in the SBIIS3
Ezekiel 14 in the SBIKS
Ezekiel 14 in the SBIKS2
Ezekiel 14 in the SBIMS
Ezekiel 14 in the SBIOS
Ezekiel 14 in the SBIPS
Ezekiel 14 in the SBISS
Ezekiel 14 in the SBITS
Ezekiel 14 in the SBITS2
Ezekiel 14 in the SBITS3
Ezekiel 14 in the SBITS4
Ezekiel 14 in the SBIUS
Ezekiel 14 in the SBIVS
Ezekiel 14 in the SBT
Ezekiel 14 in the SBT1E
Ezekiel 14 in the SCHL
Ezekiel 14 in the SNT
Ezekiel 14 in the SUSU
Ezekiel 14 in the SUSU2
Ezekiel 14 in the SYNO
Ezekiel 14 in the TBIAOTANT
Ezekiel 14 in the TBT1E
Ezekiel 14 in the TBT1E2
Ezekiel 14 in the TFTIP
Ezekiel 14 in the TFTU
Ezekiel 14 in the TGNTATF3T
Ezekiel 14 in the THAI
Ezekiel 14 in the TNFD
Ezekiel 14 in the TNT
Ezekiel 14 in the TNTIK
Ezekiel 14 in the TNTIL
Ezekiel 14 in the TNTIN
Ezekiel 14 in the TNTIP
Ezekiel 14 in the TNTIZ
Ezekiel 14 in the TOMA
Ezekiel 14 in the TTENT
Ezekiel 14 in the UBG
Ezekiel 14 in the UGV
Ezekiel 14 in the UGV2
Ezekiel 14 in the UGV3
Ezekiel 14 in the VBL
Ezekiel 14 in the VDCC
Ezekiel 14 in the YALU
Ezekiel 14 in the YAPE
Ezekiel 14 in the YBVTP
Ezekiel 14 in the ZBP