Isaiah 42 (BOKCV)

1 “Huyu hapa mtumishi wangu, ninayemtegemeza,mteule wangu, ambaye ninapendezwa naye;nitaweka Roho yangu juu yake,naye ataleta haki kwa mataifa. 2 Hatapaza sauti wala kupiga kelele,wala hataiinua sauti yake barabarani. 3 Mwanzi uliopondeka hatauvunja,na utambi unaofuka moshi hatauzima.Kwa uaminifu ataleta haki, 4 hatazimia roho wala kukata tamaa,mpaka atakaposimamisha haki juu ya dunia.Visiwa vitaweka tumaini lao katika sheria yake.” 5 Hili ndilo asemalo Mungu, BWANA,yeye aliyeziumba mbingu na kuzitanda,aliyeitandaza dunia na vyote vitokavyo humo,awapaye watu wake pumzi,na uzima kwa wale waendao humo: 6 “Mimi, BWANA, nimekuita katika haki;nitakushika mkono wako.Nitakulinda na kukufanyakuwa Agano kwa ajili ya watuna nuru kwa Mataifa, 7 kuwafungua macho wale wasioona,kuwaacha huru kutoka kifungoni waliofungwa jela,na kuwafungua kutoka gerezaniwale wanaokaa gizani. 8 “Mimi ndimi BWANA; hilo ndilo Jina langu!Sitampa mwingine utukufu wanguwala sanamu sifa zangu. 9 Tazama, mambo ya kwanza yametokea,nami natangaza mambo mapya;kabla hayajatokeanawatangazia habari zake.” 10 Mwimbieni BWANA wimbo mpya,sifa zake toka miisho ya dunia,ninyi mshukao chini baharini,na vyote vilivyomo ndani yake,enyi visiwa na wote wakaao ndani yake. 11 Jangwa na miji yake na vipaze sauti zao;makao anamoishi Kedari na yashangilie.Watu wa Sela waimbe kwa furaha,na wapige kelele kutoka vilele vya milima. 12 Wampe BWANA utukufu,na kutangaza sifa zake katika visiwa. 13 BWANA ataenda kama mtu mwenye nguvu,kama shujaa atachochea shauku yake,kwa kelele ataamsha kilio cha vita,naye atashinda adui zake. 14 “Kwa muda mrefu nimenyamaza kimya,nimekaa kimya na kujizuia.Lakini sasa, kama mwanamke wakati wa kujifungua,ninapiga kelele, ninatweta na kushusha pumzi. 15 Nitaharibu milima na vilimana kukausha mimea yako yote;nitafanya mito kuwa visiwana kukausha mabwawa. 16 Nitawaongoza vipofu kwenye njia ambayo hawajaijua,kwenye mapito wasiyoyazoea nitawaongoza;nitafanya giza kuwa nuru mbele yao,na kufanya mahali palipoparuza kuwa laini.Haya ndiyo mambo nitakayofanya;mimi sitawaacha. 17 Lakini wale wanaotumaini sanamu,wanaoviambia vinyago, ‘Ninyi ndio miungu yetu,’watarudishwa nyuma kwa aibu kubwa. 18 “Sikieni, enyi viziwi;tazameni, enyi vipofu, mpate kuona! 19 Ni nani aliye kipofu isipokuwa mtumishi wangu,na kiziwi kama mjumbe ninayemtuma?Ni nani aliye kipofu kama yeye aliyejitoa kwangu,aliye kipofu kama mtumishi wa BWANA? 20 Mmeona vitu vingi, lakini hamkuzingatia;masikio yenu yako wazi, lakini hamsikii chochote.” 21 Ilimpendeza BWANAkwa ajili ya haki yakekufanya sheria yake kuwa kuu na tukufu. 22 Lakini hili ni taifa lililoibwa na kutekwa nyara,wote wamenaswa katika mashimo,au wamefichwa katika magereza.Wamekuwa nyara,wala hapana yeyote awaokoaye.Wamefanywa mateka,wala hapana yeyote asemaye, “Warudishe.” 23 Ni nani miongoni mwenu atakayesikiliza hili,au atakayezingatia kwa makini katika wakati ujao? 24 Ni nani aliyemtoa Yakobo kuwa mateka,na Israeli kwa wateka nyara?Je, hakuwa yeye, BWANA,ambaye tumetenda dhambi dhidi yake?Kwa kuwa hawakufuata njia zake,hawakutii sheria zake. 25 Hivyo akawamwagia hasira yake inayowaka,ukali wa vita.Iliwazunguka kwa miali ya moto, lakini hata hivyo hawakuelewa;iliwateketeza, lakini hawakuyatia moyoni.

In Other Versions

Isaiah 42 in the ANGEFD

Isaiah 42 in the ANTPNG2D

Isaiah 42 in the AS21

Isaiah 42 in the BAGH

Isaiah 42 in the BBPNG

Isaiah 42 in the BBT1E

Isaiah 42 in the BDS

Isaiah 42 in the BEV

Isaiah 42 in the BHAD

Isaiah 42 in the BIB

Isaiah 42 in the BLPT

Isaiah 42 in the BNT

Isaiah 42 in the BNTABOOT

Isaiah 42 in the BNTLV

Isaiah 42 in the BOATCB

Isaiah 42 in the BOATCB2

Isaiah 42 in the BOBCV

Isaiah 42 in the BOCNT

Isaiah 42 in the BOECS

Isaiah 42 in the BOGWICC

Isaiah 42 in the BOHCB

Isaiah 42 in the BOHCV

Isaiah 42 in the BOHLNT

Isaiah 42 in the BOHNTLTAL

Isaiah 42 in the BOICB

Isaiah 42 in the BOILNTAP

Isaiah 42 in the BOITCV

Isaiah 42 in the BOKCV2

Isaiah 42 in the BOKHWOG

Isaiah 42 in the BOKSSV

Isaiah 42 in the BOLCB

Isaiah 42 in the BOLCB2

Isaiah 42 in the BOMCV

Isaiah 42 in the BONAV

Isaiah 42 in the BONCB

Isaiah 42 in the BONLT

Isaiah 42 in the BONUT2

Isaiah 42 in the BOPLNT

Isaiah 42 in the BOSCB

Isaiah 42 in the BOSNC

Isaiah 42 in the BOTLNT

Isaiah 42 in the BOVCB

Isaiah 42 in the BOYCB

Isaiah 42 in the BPBB

Isaiah 42 in the BPH

Isaiah 42 in the BSB

Isaiah 42 in the CCB

Isaiah 42 in the CUV

Isaiah 42 in the CUVS

Isaiah 42 in the DBT

Isaiah 42 in the DGDNT

Isaiah 42 in the DHNT

Isaiah 42 in the DNT

Isaiah 42 in the ELBE

Isaiah 42 in the EMTV

Isaiah 42 in the ESV

Isaiah 42 in the FBV

Isaiah 42 in the FEB

Isaiah 42 in the GGMNT

Isaiah 42 in the GNT

Isaiah 42 in the HARY

Isaiah 42 in the HNT

Isaiah 42 in the IRVA

Isaiah 42 in the IRVB

Isaiah 42 in the IRVG

Isaiah 42 in the IRVH

Isaiah 42 in the IRVK

Isaiah 42 in the IRVM

Isaiah 42 in the IRVM2

Isaiah 42 in the IRVO

Isaiah 42 in the IRVP

Isaiah 42 in the IRVT

Isaiah 42 in the IRVT2

Isaiah 42 in the IRVU

Isaiah 42 in the ISVN

Isaiah 42 in the JSNT

Isaiah 42 in the KAPI

Isaiah 42 in the KBT1ETNIK

Isaiah 42 in the KBV

Isaiah 42 in the KJV

Isaiah 42 in the KNFD

Isaiah 42 in the LBA

Isaiah 42 in the LBLA

Isaiah 42 in the LNT

Isaiah 42 in the LSV

Isaiah 42 in the MAAL

Isaiah 42 in the MBV

Isaiah 42 in the MBV2

Isaiah 42 in the MHNT

Isaiah 42 in the MKNFD

Isaiah 42 in the MNG

Isaiah 42 in the MNT

Isaiah 42 in the MNT2

Isaiah 42 in the MRS1T

Isaiah 42 in the NAA

Isaiah 42 in the NASB

Isaiah 42 in the NBLA

Isaiah 42 in the NBS

Isaiah 42 in the NBVTP

Isaiah 42 in the NET2

Isaiah 42 in the NIV11

Isaiah 42 in the NNT

Isaiah 42 in the NNT2

Isaiah 42 in the NNT3

Isaiah 42 in the PDDPT

Isaiah 42 in the PFNT

Isaiah 42 in the RMNT

Isaiah 42 in the SBIAS

Isaiah 42 in the SBIBS

Isaiah 42 in the SBIBS2

Isaiah 42 in the SBICS

Isaiah 42 in the SBIDS

Isaiah 42 in the SBIGS

Isaiah 42 in the SBIHS

Isaiah 42 in the SBIIS

Isaiah 42 in the SBIIS2

Isaiah 42 in the SBIIS3

Isaiah 42 in the SBIKS

Isaiah 42 in the SBIKS2

Isaiah 42 in the SBIMS

Isaiah 42 in the SBIOS

Isaiah 42 in the SBIPS

Isaiah 42 in the SBISS

Isaiah 42 in the SBITS

Isaiah 42 in the SBITS2

Isaiah 42 in the SBITS3

Isaiah 42 in the SBITS4

Isaiah 42 in the SBIUS

Isaiah 42 in the SBIVS

Isaiah 42 in the SBT

Isaiah 42 in the SBT1E

Isaiah 42 in the SCHL

Isaiah 42 in the SNT

Isaiah 42 in the SUSU

Isaiah 42 in the SUSU2

Isaiah 42 in the SYNO

Isaiah 42 in the TBIAOTANT

Isaiah 42 in the TBT1E

Isaiah 42 in the TBT1E2

Isaiah 42 in the TFTIP

Isaiah 42 in the TFTU

Isaiah 42 in the TGNTATF3T

Isaiah 42 in the THAI

Isaiah 42 in the TNFD

Isaiah 42 in the TNT

Isaiah 42 in the TNTIK

Isaiah 42 in the TNTIL

Isaiah 42 in the TNTIN

Isaiah 42 in the TNTIP

Isaiah 42 in the TNTIZ

Isaiah 42 in the TOMA

Isaiah 42 in the TTENT

Isaiah 42 in the UBG

Isaiah 42 in the UGV

Isaiah 42 in the UGV2

Isaiah 42 in the UGV3

Isaiah 42 in the VBL

Isaiah 42 in the VDCC

Isaiah 42 in the YALU

Isaiah 42 in the YAPE

Isaiah 42 in the YBVTP

Isaiah 42 in the ZBP