Isaiah 45 (BOKCV)

1 “Hili ndilo asemalo BWANA kwa mpakwa mafuta wake,Koreshi, ambaye nimemshika mkono wake wa kuumekutiisha mataifa mbele yakena kuwavua wafalme silaha zao,kufungua milango mbele yakeili malango yasije yakafungwa: 2 Nitakwenda mbele yakona kusawazisha milima;nitavunjavunja malango ya shabana kukatakata mapingo ya chuma. 3 Nitakupa hazina za gizani,mali zilizofichwa mahali pa siri,ili upate kujua ya kwamba Mimi ndimi BWANA,Mungu wa Israeli, akuitaye kwa jina lako. 4 Kwa ajili ya Yakobo mtumishi wangu,Israeli niliyemchagua,nimekuita wewe kwa jina lako,na kukupa jina la heshima,ingawa wewe hunitambui. 5 Mimi ndimi BWANA, wala hakuna mwingine,zaidi yangu hakuna Mungu.Nitakutia nguvu,ingawa wewe hujanitambua, 6 ili kutoka mawio ya juampaka machweo yake,watu wapate kujua kwamba hakuna Mungu mwingine ila Mimi.Mimi ndimi BWANA wala hakuna mwingine. 7 Mimi ninaumba nuru na kuhuluku giza,ninaleta mafanikio na kusababisha maafa.Mimi, BWANA, huyatenda haya yote. 8 “Enyi mbingu juu, nyesheni haki,mawingu na yaidondoshe.Dunia na ifunguke sana,wokovu na uchipuke,haki na ikue pamoja nao.Mimi, BWANA, ndiye niliyeiumba. 9 “Ole wake yeye ashindanaye na Muumba wake,yeye ambaye ni kigae tu kati ya vigae juu ya ardhi.Je, udongo wa kufinyangia humwambia mfinyanzi,‘Unatengeneza nini wewe?’Je, kazi yako husema,‘Hana mikono’? 10 Ole wake amwambiaye baba yake,‘Umezaa nini?’Au kumwambia mama yake,‘Umezaa kitu gani?’ 11 “Hili ndilo asemalo BWANA,yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli na Muumba wake:Kuhusu mambo yatakayokuja,je, unaniuliza habari za watoto wangu,au kunipa amri kuhusu kazi za mikono yangu? 12 Mimi ndiye niliyeumba duniana kumuumba mwanadamu juu yake.Mikono yangu mwenyewe ndiyo iliyozitanda mbingu,nikayapanga majeshi yake yote ya angani. 13 Mimi nitamwinua Koreshi katika haki yangu:nitazinyoosha njia zake zote.Yeye atajenga mji wangu upya,na kuwaweka huru watu wangu walio uhamishoni,lakini si kwa kulipiwa fedha wala kupewa zawadi,asema BWANA Mwenye Nguvu Zote.” 14 Hili ndilo asemalo BWANA:“Mazao ya Misri na bidhaa za Kushi,nao wale Waseba warefu,watakujia na kuwa wako,watakujia wakijikokota nyuma yako,watakujia wamefungwa minyororo.Watasujudu mbele yakowakikusihi na kusema,‘Hakika Mungu yu pamoja nawe,wala hakuna mwingine;hakuna Mungu mwingine.’ ” 15 Hakika wewe u Mungu unayejificha,Ee Mungu na Mwokozi wa Israeli. 16 Wote watengenezao sanamu wataaibika na kutahayarika;wataenda kutahayarika pamoja. 17 Lakini Israeli ataokolewa na BWANAkwa wokovu wa milele;kamwe hutaaibika wala kutatahayarika,milele yote. 18 Kwa kuwa hili ndilo asemalo BWANA,yeye aliyeumba mbingu,ndiye Mungu;yeye aliyeifanya dunia na kuiumba,yeye ndiye aliiwekea misingi imara,hakuiumba ili iwe tupu,bali aliiumba ikaliwe na viumbe vyake.Anasema:“Mimi ndimi BWANA,wala hakuna mwingine. 19 Sijasema sirini,kutoka mahali fulani katika nchi ya giza;sijawaambia wazao wa Yakobo,‘Nitafuteni bure.’Mimi, BWANA, nasema kweli;ninatangaza lililo sahihi. 20 “Kusanyikeni pamoja mje,enyi wakimbizi kutoka mataifa.Wale wabebao sanamu za mti ni watu wasio na akili,wale waombao miungu isiyoweza kuokoa. 21 Tangazeni litakalokuwepo, lisemeni hilo,wao na wafanye shauri pamoja.Ni nani aliyetangulia kusema hili tangu zamani,aliyetangaza tangu zamani za kale?Je, haikuwa Mimi, BWANA?Wala hapana Mungu mwinginezaidi yangu mimi,Mungu mwenye haki na Mwokozi;hapana mwingine ila mimi. 22 “Nigeukieni mimi, nanyi mkaokolewe,enyi miisho yote ya dunia;kwa maana mimi ndimi Mungu,wala hapana mwingine. 23 Nimeapa kwa nafsi yangu,kinywa changu kimenena katika uadilifu woteneno ambalo halitatanguka:Kila goti litapigwa mbele zangu,kwangu mimi kila ulimi utaapa. 24 Watasema kuhusu mimi,‘Katika BWANA peke yakendiko kuna haki na nguvu.’ ”Wote ambao wamemkasirikia Munguwatamjia yeye, nao watatahayarika. 25 Lakini katika BWANA wazao wote wa Israeliwataonekana wenye haki na watashangilia.

In Other Versions

Isaiah 45 in the ANGEFD

Isaiah 45 in the ANTPNG2D

Isaiah 45 in the AS21

Isaiah 45 in the BAGH

Isaiah 45 in the BBPNG

Isaiah 45 in the BBT1E

Isaiah 45 in the BDS

Isaiah 45 in the BEV

Isaiah 45 in the BHAD

Isaiah 45 in the BIB

Isaiah 45 in the BLPT

Isaiah 45 in the BNT

Isaiah 45 in the BNTABOOT

Isaiah 45 in the BNTLV

Isaiah 45 in the BOATCB

Isaiah 45 in the BOATCB2

Isaiah 45 in the BOBCV

Isaiah 45 in the BOCNT

Isaiah 45 in the BOECS

Isaiah 45 in the BOGWICC

Isaiah 45 in the BOHCB

Isaiah 45 in the BOHCV

Isaiah 45 in the BOHLNT

Isaiah 45 in the BOHNTLTAL

Isaiah 45 in the BOICB

Isaiah 45 in the BOILNTAP

Isaiah 45 in the BOITCV

Isaiah 45 in the BOKCV2

Isaiah 45 in the BOKHWOG

Isaiah 45 in the BOKSSV

Isaiah 45 in the BOLCB

Isaiah 45 in the BOLCB2

Isaiah 45 in the BOMCV

Isaiah 45 in the BONAV

Isaiah 45 in the BONCB

Isaiah 45 in the BONLT

Isaiah 45 in the BONUT2

Isaiah 45 in the BOPLNT

Isaiah 45 in the BOSCB

Isaiah 45 in the BOSNC

Isaiah 45 in the BOTLNT

Isaiah 45 in the BOVCB

Isaiah 45 in the BOYCB

Isaiah 45 in the BPBB

Isaiah 45 in the BPH

Isaiah 45 in the BSB

Isaiah 45 in the CCB

Isaiah 45 in the CUV

Isaiah 45 in the CUVS

Isaiah 45 in the DBT

Isaiah 45 in the DGDNT

Isaiah 45 in the DHNT

Isaiah 45 in the DNT

Isaiah 45 in the ELBE

Isaiah 45 in the EMTV

Isaiah 45 in the ESV

Isaiah 45 in the FBV

Isaiah 45 in the FEB

Isaiah 45 in the GGMNT

Isaiah 45 in the GNT

Isaiah 45 in the HARY

Isaiah 45 in the HNT

Isaiah 45 in the IRVA

Isaiah 45 in the IRVB

Isaiah 45 in the IRVG

Isaiah 45 in the IRVH

Isaiah 45 in the IRVK

Isaiah 45 in the IRVM

Isaiah 45 in the IRVM2

Isaiah 45 in the IRVO

Isaiah 45 in the IRVP

Isaiah 45 in the IRVT

Isaiah 45 in the IRVT2

Isaiah 45 in the IRVU

Isaiah 45 in the ISVN

Isaiah 45 in the JSNT

Isaiah 45 in the KAPI

Isaiah 45 in the KBT1ETNIK

Isaiah 45 in the KBV

Isaiah 45 in the KJV

Isaiah 45 in the KNFD

Isaiah 45 in the LBA

Isaiah 45 in the LBLA

Isaiah 45 in the LNT

Isaiah 45 in the LSV

Isaiah 45 in the MAAL

Isaiah 45 in the MBV

Isaiah 45 in the MBV2

Isaiah 45 in the MHNT

Isaiah 45 in the MKNFD

Isaiah 45 in the MNG

Isaiah 45 in the MNT

Isaiah 45 in the MNT2

Isaiah 45 in the MRS1T

Isaiah 45 in the NAA

Isaiah 45 in the NASB

Isaiah 45 in the NBLA

Isaiah 45 in the NBS

Isaiah 45 in the NBVTP

Isaiah 45 in the NET2

Isaiah 45 in the NIV11

Isaiah 45 in the NNT

Isaiah 45 in the NNT2

Isaiah 45 in the NNT3

Isaiah 45 in the PDDPT

Isaiah 45 in the PFNT

Isaiah 45 in the RMNT

Isaiah 45 in the SBIAS

Isaiah 45 in the SBIBS

Isaiah 45 in the SBIBS2

Isaiah 45 in the SBICS

Isaiah 45 in the SBIDS

Isaiah 45 in the SBIGS

Isaiah 45 in the SBIHS

Isaiah 45 in the SBIIS

Isaiah 45 in the SBIIS2

Isaiah 45 in the SBIIS3

Isaiah 45 in the SBIKS

Isaiah 45 in the SBIKS2

Isaiah 45 in the SBIMS

Isaiah 45 in the SBIOS

Isaiah 45 in the SBIPS

Isaiah 45 in the SBISS

Isaiah 45 in the SBITS

Isaiah 45 in the SBITS2

Isaiah 45 in the SBITS3

Isaiah 45 in the SBITS4

Isaiah 45 in the SBIUS

Isaiah 45 in the SBIVS

Isaiah 45 in the SBT

Isaiah 45 in the SBT1E

Isaiah 45 in the SCHL

Isaiah 45 in the SNT

Isaiah 45 in the SUSU

Isaiah 45 in the SUSU2

Isaiah 45 in the SYNO

Isaiah 45 in the TBIAOTANT

Isaiah 45 in the TBT1E

Isaiah 45 in the TBT1E2

Isaiah 45 in the TFTIP

Isaiah 45 in the TFTU

Isaiah 45 in the TGNTATF3T

Isaiah 45 in the THAI

Isaiah 45 in the TNFD

Isaiah 45 in the TNT

Isaiah 45 in the TNTIK

Isaiah 45 in the TNTIL

Isaiah 45 in the TNTIN

Isaiah 45 in the TNTIP

Isaiah 45 in the TNTIZ

Isaiah 45 in the TOMA

Isaiah 45 in the TTENT

Isaiah 45 in the UBG

Isaiah 45 in the UGV

Isaiah 45 in the UGV2

Isaiah 45 in the UGV3

Isaiah 45 in the VBL

Isaiah 45 in the VDCC

Isaiah 45 in the YALU

Isaiah 45 in the YAPE

Isaiah 45 in the YBVTP

Isaiah 45 in the ZBP