Jeremiah 50 (BOKCV)

1 Hili ndilo neno alilosema BWANA kupitia nabii Yeremia kuhusu Babeli na nchi ya Wakaldayo: 2 “Tangazeni na mhubiri katikati ya mataifa,twekeni bendera na mkahubiri;msiache kitu chochote, bali semeni,‘Babeli utatekwa;Beli ataaibishwa,Merodaki atajazwa na hofu kuu.Sanamu zake zitaaibishwana vinyago vyake vitajazwa hofu kuu.’ 3 Taifa kutoka kaskazini litamshambulia,na kuifanya nchi yake ukiwa.Hakuna hata mmoja atakayeishi ndani yake,watu na wanyama wataikimbia. 4 “Katika siku hizo, wakati huo,”asema BWANA,“watu wa Israeli pamoja na watu wa Yudawataenda wakilia ili kumtafuta BWANA Mungu wao. 5 Wataiuliza njia iendayo Sayunina kuelekeza nyuso zao huko.Watakuja na kuambatana na BWANAkatika agano la mileleambalo halitasahaulika. 6 “Watu wangu wamekuwa kondoo waliopotea;wachungaji wao wamewapotoshana kuwasababisha kuzururajuu ya milima.Walitangatanga juu ya mlima na kilima,na kusahau mahali pao wenyewe pa kupumzikia. 7 Yeyote aliyewakuta aliwala;adui zao walisema, ‘Sisi hatuna hatia,kwa kuwa wao walitenda dhambi dhidi ya BWANA, malisho yao halisi, BWANA, aliye tumaini la baba zao.’ 8 “Kimbieni kutoka Babeli;ondokeni katika nchi ya Wakaldayotena kuweni kama mbuzi wale waongozao kundi. 9 Kwa maana nitaamsha na kuleta dhidi ya Babelimuungano wa mataifa makubwa kutoka nchi ya kaskazini.Watashika nafasi zao dhidi yake,naye kutokea kaskazini atatekwa.Mishale yao itakuwa kama mishale ya mashujaa walio hodari,ambao hawawezi kurudi mikono mitupu. 10 Kwa hiyo Ukaldayo utatekwa nyara;wote wamtekao nyara watapata za kutosha,”asema BWANA. 11 “Kwa sababu hushangilia na kufurahi,wewe utekaye urithi wangu,kwa sababu unachezacheza kama mtamba anayepura nafaka,na kulia kama farasi dume, 12 mama yako ataaibika mno,yeye aliyekuzaa atatahayari.Atakuwa mdogo kuliko mataifa mengine yote,atakuwa nyika, nchi kame na jangwa. 13 Kwa sababu ya hasira ya BWANA hatakaliwa na mtu,lakini ataachwa ukiwa kabisa.Wote watakaopita Babeli watatiwa hofu na kudhihakikwa sababu ya majeraha yake yote. 14 “Shikeni nafasi zenu kuzunguka Babeli,enyi nyote mvutao upinde.Mpigeni! Msibakize mshale wowote,kwa kuwa ametenda dhambi dhidi ya BWANA. 15 Piga kelele dhidi yake kila upande!Anajisalimisha, minara yake inaanguka,kuta zake zimebomoka.Kwa kuwa hiki ni kisasi cha BWANA,mlipizeni kisasi;mtendeeni kama alivyowatendea wengine. 16 Katilieni mbali mpanzi kutoka Babeli,pamoja na mvunaji na mundu wake akivuna.Kwa sababu ya upanga wa mdhalimukila mmoja na arejee kwa watu wake mwenyewe,kila mmoja na akimbiliekwenye nchi yake mwenyewe. 17 “Israeli ni kundi lililotawanyikaambalo simba wamelifukuzia mbali.Wa kwanza kumla alikuwa mfalme wa Ashuru,wa mwisho kuponda mifupa yakealikuwa Nebukadneza mfalme wa Babeli.” 18 Kwa hiyo hili ndilo BWANA Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo:“Nitamwadhibu mfalme wa Babeli na nchi yakekama nilivyomwadhibu mfalme wa Ashuru. 19 Lakini nitamrudisha Israeli katika malisho yake mwenyewenaye atalisha huko Karmeli na Bashani;njaa yake itashibishwajuu ya vilima vya Efraimu na Gileadi. 20 Katika siku hizo, wakati huo,”asema BWANA,“uchunguzi utafanyika kwa ajili ya kosa la Israeli,lakini halitakuwepo,kwa ajili ya dhambi za Yuda,lakini haitapatikana hata moja,kwa kuwa nitawasamehemabaki nitakaowaacha. 21 “Shambulieni nchi ya Merathaimuna wale waishio huko Pekodi.Wafuatieni, wauenina kuwaangamiza kabisa,”asema BWANA.“Fanyeni kila kitu nilichowaamuru. 22 Kelele ya vita iko ndani ya nchi,kelele ya maangamizi makuu! 23 Tazama jinsi nyundo ya dunia yoteilivyovunjika na kuharibika!Tazama jinsi Babeli ilivyokuwa ukiwamiongoni mwa mataifa! 24 Nimetega mtego kwa ajili yako, ee Babeli,nawe ukakamatwa kabla haujafahamu;ulipatikana na ukakamatwakwa sababu ulimpinga BWANA. 25 BWANA amefungua ghala lake la silahana kuzitoa silaha za ghadhabu yake,kwa kuwa BWANA Mwenyezi Mwenye Nguvu Zoteanayo kazi ya kufanyakatika nchi ya Wakaldayo. 26 Njooni dhidi yake kutoka mbali.Zifungueni ghala zake za nafaka;mlundikeni kama lundo la nafaka.Mwangamizeni kabisana msimwachie mabaki yoyote. 27 Waueni mafahali wake wachanga wote;waacheni washuke machinjoni!Ole wao! Kwa kuwa siku yao imewadia,wakati wao wa kuadhibiwa. 28 Wasikilizeni watoro na wakimbizi kutoka Babeliwakitangaza katika Sayunijinsi BWANA, Mungu wetu alivyolipiza kisasi,kisasi kwa ajili ya Hekalu lake. 29 “Waiteni wapiga mishale dhidi ya Babeli,wote wale wavutao upinde.Pigeni kambi kumzunguka kabisa,asitoroke mtu yeyote.Mlipizeni kwa matendo yake;mtendeeni kama alivyotenda.Kwa kuwa alimdharau BWANA,yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli. 30 Kwa hiyo, vijana wake wanaume wataanguka barabarani;askari wake wote watanyamazishwa siku ile,”asema BWANA. 31 “Tazama, niko kinyume nawe, ewe mwenye majivuno,”asema Bwana, BWANA Mwenye Nguvu Zote,“kwa kuwa siku yako imewadia,yaani, wakati wako wa kuadhibiwa. 32 Mwenye majivuno atajikwaa na kuanguka,wala hakuna yeyote atakayemuinua;nitawasha moto katika miji yake,utakaowateketeza wote wanaomzunguka.” 33 Hili ndilo asemalo BWANA Mwenye Nguvu Zote:“Watu wa Israeli wameonewa,nao watu wa Yuda pia.Wote waliowateka wamewashikilia sana,wanakataa kuwaachia waende. 34 Lakini Mkombozi wao ana nguvu; BWANA Mwenye Nguvu Zote ndilo jina lake.Atatetea kwa nguvu shauri laoili alete raha katika nchi yao,lakini ataleta msukosukokwa wale waishio Babeli. 35 “Upanga dhidi ya Wakaldayo!”asema BWANA,“dhidi ya wale waishio Babelina dhidi ya maafisa wake na watu wenye busara! 36 Upanga dhidi ya manabii wake wa uongo!Watakuwa wapumbavu.Upanga dhidi ya mashujaa wake!Watajazwa na hofu kuu 37 Upanga dhidi ya farasi na magari yake ya vitapamoja na askari wake wote wa kigeni katika safu zake!Wao watakuwa kama wanawake.Upanga dhidi ya hazina zake!Hizo zitatekwa nyara. 38 Ukame juu ya maji yake!Nayo yatakauka.Kwa kuwa ni nchi ya sanamu,wao wanaenda wazimu kwa ajili ya sanamu. 39 “Kwa hiyo, viumbe vya jangwani na fisi wataishi humo,nao bundi watakaa humo.Kamwe haitakaliwa tenawala watu hawataishi humo kutoka kizazi hadi kizazi. 40 Kama vile Mungu alivyoangamiza Sodoma na Gomorapamoja na miji iliyokuwa jirani nayo,”asema BWANA,“vivyo hivyo hakuna mtu yeyoteatakayeishi humo.Naam, hakuna mtu yeyoteatakayekaa humo. 41 “Tazama! Jeshi linakuja kutoka kaskazini;taifa kubwa na wafalme wengiwanaamshwa kutoka miisho ya dunia. 42 Wamejifunga pinde na mikuki;ni wakatili na wasio na huruma.Wanatoa sauti kama bahari inayongurumawanapoendesha farasi zao;wanakuja kama watu waliojipanga tayari kwa vitaili kukushambulia, ee Binti Babeli. 43 Mfalme wa Babeli amesikia habari kuwahusu,nayo mikono yake imelegea.Uchungu umemshika,maumivu kama ya mwanamke katika utungu wa kuzaa. 44 Kama simba anayepanda kutoka vichaka vya Yordanikuja kwenye nchi ya malisho mengi,ndivyo nitamfukuza Babeli kutoka nchi yake ghafula.Ni nani aliye mteule,nitakayemweka kwa ajili ya jambo hili?Ni nani aliye kama mimi,na ni nani awezaye kunipinga?Tena ni mchungaji yupiawezaye kusimama kinyume nami?” 45 Kwa hiyo, sikia kile BWANA alichokipanga dhidi ya Babeli,kile alichokusudia dhidi ya nchi ya Wakaldayo:Aliye mchanga katika kundi ataburutwa mbali.Yeye ataharibu kabisa malisho yao kwa sababu yao. 46 Kwa sauti ya kutekwa kwa Babeli, dunia itatetemeka;kilio chake kitasikika pote miongoni mwa mataifa.

In Other Versions

Jeremiah 50 in the ANGEFD

Jeremiah 50 in the ANTPNG2D

Jeremiah 50 in the AS21

Jeremiah 50 in the BAGH

Jeremiah 50 in the BBPNG

Jeremiah 50 in the BBT1E

Jeremiah 50 in the BDS

Jeremiah 50 in the BEV

Jeremiah 50 in the BHAD

Jeremiah 50 in the BIB

Jeremiah 50 in the BLPT

Jeremiah 50 in the BNT

Jeremiah 50 in the BNTABOOT

Jeremiah 50 in the BNTLV

Jeremiah 50 in the BOATCB

Jeremiah 50 in the BOATCB2

Jeremiah 50 in the BOBCV

Jeremiah 50 in the BOCNT

Jeremiah 50 in the BOECS

Jeremiah 50 in the BOGWICC

Jeremiah 50 in the BOHCB

Jeremiah 50 in the BOHCV

Jeremiah 50 in the BOHLNT

Jeremiah 50 in the BOHNTLTAL

Jeremiah 50 in the BOICB

Jeremiah 50 in the BOILNTAP

Jeremiah 50 in the BOITCV

Jeremiah 50 in the BOKCV2

Jeremiah 50 in the BOKHWOG

Jeremiah 50 in the BOKSSV

Jeremiah 50 in the BOLCB

Jeremiah 50 in the BOLCB2

Jeremiah 50 in the BOMCV

Jeremiah 50 in the BONAV

Jeremiah 50 in the BONCB

Jeremiah 50 in the BONLT

Jeremiah 50 in the BONUT2

Jeremiah 50 in the BOPLNT

Jeremiah 50 in the BOSCB

Jeremiah 50 in the BOSNC

Jeremiah 50 in the BOTLNT

Jeremiah 50 in the BOVCB

Jeremiah 50 in the BOYCB

Jeremiah 50 in the BPBB

Jeremiah 50 in the BPH

Jeremiah 50 in the BSB

Jeremiah 50 in the CCB

Jeremiah 50 in the CUV

Jeremiah 50 in the CUVS

Jeremiah 50 in the DBT

Jeremiah 50 in the DGDNT

Jeremiah 50 in the DHNT

Jeremiah 50 in the DNT

Jeremiah 50 in the ELBE

Jeremiah 50 in the EMTV

Jeremiah 50 in the ESV

Jeremiah 50 in the FBV

Jeremiah 50 in the FEB

Jeremiah 50 in the GGMNT

Jeremiah 50 in the GNT

Jeremiah 50 in the HARY

Jeremiah 50 in the HNT

Jeremiah 50 in the IRVA

Jeremiah 50 in the IRVB

Jeremiah 50 in the IRVG

Jeremiah 50 in the IRVH

Jeremiah 50 in the IRVK

Jeremiah 50 in the IRVM

Jeremiah 50 in the IRVM2

Jeremiah 50 in the IRVO

Jeremiah 50 in the IRVP

Jeremiah 50 in the IRVT

Jeremiah 50 in the IRVT2

Jeremiah 50 in the IRVU

Jeremiah 50 in the ISVN

Jeremiah 50 in the JSNT

Jeremiah 50 in the KAPI

Jeremiah 50 in the KBT1ETNIK

Jeremiah 50 in the KBV

Jeremiah 50 in the KJV

Jeremiah 50 in the KNFD

Jeremiah 50 in the LBA

Jeremiah 50 in the LBLA

Jeremiah 50 in the LNT

Jeremiah 50 in the LSV

Jeremiah 50 in the MAAL

Jeremiah 50 in the MBV

Jeremiah 50 in the MBV2

Jeremiah 50 in the MHNT

Jeremiah 50 in the MKNFD

Jeremiah 50 in the MNG

Jeremiah 50 in the MNT

Jeremiah 50 in the MNT2

Jeremiah 50 in the MRS1T

Jeremiah 50 in the NAA

Jeremiah 50 in the NASB

Jeremiah 50 in the NBLA

Jeremiah 50 in the NBS

Jeremiah 50 in the NBVTP

Jeremiah 50 in the NET2

Jeremiah 50 in the NIV11

Jeremiah 50 in the NNT

Jeremiah 50 in the NNT2

Jeremiah 50 in the NNT3

Jeremiah 50 in the PDDPT

Jeremiah 50 in the PFNT

Jeremiah 50 in the RMNT

Jeremiah 50 in the SBIAS

Jeremiah 50 in the SBIBS

Jeremiah 50 in the SBIBS2

Jeremiah 50 in the SBICS

Jeremiah 50 in the SBIDS

Jeremiah 50 in the SBIGS

Jeremiah 50 in the SBIHS

Jeremiah 50 in the SBIIS

Jeremiah 50 in the SBIIS2

Jeremiah 50 in the SBIIS3

Jeremiah 50 in the SBIKS

Jeremiah 50 in the SBIKS2

Jeremiah 50 in the SBIMS

Jeremiah 50 in the SBIOS

Jeremiah 50 in the SBIPS

Jeremiah 50 in the SBISS

Jeremiah 50 in the SBITS

Jeremiah 50 in the SBITS2

Jeremiah 50 in the SBITS3

Jeremiah 50 in the SBITS4

Jeremiah 50 in the SBIUS

Jeremiah 50 in the SBIVS

Jeremiah 50 in the SBT

Jeremiah 50 in the SBT1E

Jeremiah 50 in the SCHL

Jeremiah 50 in the SNT

Jeremiah 50 in the SUSU

Jeremiah 50 in the SUSU2

Jeremiah 50 in the SYNO

Jeremiah 50 in the TBIAOTANT

Jeremiah 50 in the TBT1E

Jeremiah 50 in the TBT1E2

Jeremiah 50 in the TFTIP

Jeremiah 50 in the TFTU

Jeremiah 50 in the TGNTATF3T

Jeremiah 50 in the THAI

Jeremiah 50 in the TNFD

Jeremiah 50 in the TNT

Jeremiah 50 in the TNTIK

Jeremiah 50 in the TNTIL

Jeremiah 50 in the TNTIN

Jeremiah 50 in the TNTIP

Jeremiah 50 in the TNTIZ

Jeremiah 50 in the TOMA

Jeremiah 50 in the TTENT

Jeremiah 50 in the UBG

Jeremiah 50 in the UGV

Jeremiah 50 in the UGV2

Jeremiah 50 in the UGV3

Jeremiah 50 in the VBL

Jeremiah 50 in the VDCC

Jeremiah 50 in the YALU

Jeremiah 50 in the YAPE

Jeremiah 50 in the YBVTP

Jeremiah 50 in the ZBP