Job 6 (BOKCV)

1 Kisha Ayubu akajibu: 2 “Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa,nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani! 3 Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote,kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka. 4 Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu,roho yangu inakunywa sumu yake;vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu. 5 Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani,au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula? 6 Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi,au upo utamu katika ute mweupe wa yai? 7 Ninakataa kuvigusa;vyakula vya aina hii hunichukiza. 8 “Laiti ningepata haja yangu,kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia, 9 kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda,kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali! 10 Ndipo bado ningekuwa na hii faraja,furaha yangu katika maumivu makali:kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu. 11 “Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini?Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu? 12 Je, mimi nina nguvu za jiwe?Je, mwili wangu ni shaba? 13 Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe,wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami? 14 “Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake,hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi. 15 Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa,ni kama vijito vya msimu,ni kama vijito ambavyo hufurika 16 wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo,ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka, 17 lakini hukauka majira ya ukame,na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake. 18 Misafara hugeuka kutoka njia zake;hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia. 19 Misafara ya Tema inatafuta maji,wafanyabiashara wa Sheba wanaosafirihutazama kwa matarajio. 20 Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini;wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia. 21 Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote;mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa. 22 Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu,au mnilipie fidia kutoka mali zenu, 23 au niokoeni mikononi mwa adui,au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’? 24 “Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya;nionyesheni nilikokosea. 25 Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli!Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini? 26 Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema,na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo? 27 Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima,na kubadilishana rafiki yenu na mali. 28 “Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi.Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu? 29 Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu;angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu. 30 Je, pana uovu wowote midomoni mwangu?Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

In Other Versions

Job 6 in the ANGEFD

Job 6 in the ANTPNG2D

Job 6 in the AS21

Job 6 in the BAGH

Job 6 in the BBPNG

Job 6 in the BBT1E

Job 6 in the BDS

Job 6 in the BEV

Job 6 in the BHAD

Job 6 in the BIB

Job 6 in the BLPT

Job 6 in the BNT

Job 6 in the BNTABOOT

Job 6 in the BNTLV

Job 6 in the BOATCB

Job 6 in the BOATCB2

Job 6 in the BOBCV

Job 6 in the BOCNT

Job 6 in the BOECS

Job 6 in the BOGWICC

Job 6 in the BOHCB

Job 6 in the BOHCV

Job 6 in the BOHLNT

Job 6 in the BOHNTLTAL

Job 6 in the BOICB

Job 6 in the BOILNTAP

Job 6 in the BOITCV

Job 6 in the BOKCV2

Job 6 in the BOKHWOG

Job 6 in the BOKSSV

Job 6 in the BOLCB

Job 6 in the BOLCB2

Job 6 in the BOMCV

Job 6 in the BONAV

Job 6 in the BONCB

Job 6 in the BONLT

Job 6 in the BONUT2

Job 6 in the BOPLNT

Job 6 in the BOSCB

Job 6 in the BOSNC

Job 6 in the BOTLNT

Job 6 in the BOVCB

Job 6 in the BOYCB

Job 6 in the BPBB

Job 6 in the BPH

Job 6 in the BSB

Job 6 in the CCB

Job 6 in the CUV

Job 6 in the CUVS

Job 6 in the DBT

Job 6 in the DGDNT

Job 6 in the DHNT

Job 6 in the DNT

Job 6 in the ELBE

Job 6 in the EMTV

Job 6 in the ESV

Job 6 in the FBV

Job 6 in the FEB

Job 6 in the GGMNT

Job 6 in the GNT

Job 6 in the HARY

Job 6 in the HNT

Job 6 in the IRVA

Job 6 in the IRVB

Job 6 in the IRVG

Job 6 in the IRVH

Job 6 in the IRVK

Job 6 in the IRVM

Job 6 in the IRVM2

Job 6 in the IRVO

Job 6 in the IRVP

Job 6 in the IRVT

Job 6 in the IRVT2

Job 6 in the IRVU

Job 6 in the ISVN

Job 6 in the JSNT

Job 6 in the KAPI

Job 6 in the KBT1ETNIK

Job 6 in the KBV

Job 6 in the KJV

Job 6 in the KNFD

Job 6 in the LBA

Job 6 in the LBLA

Job 6 in the LNT

Job 6 in the LSV

Job 6 in the MAAL

Job 6 in the MBV

Job 6 in the MBV2

Job 6 in the MHNT

Job 6 in the MKNFD

Job 6 in the MNG

Job 6 in the MNT

Job 6 in the MNT2

Job 6 in the MRS1T

Job 6 in the NAA

Job 6 in the NASB

Job 6 in the NBLA

Job 6 in the NBS

Job 6 in the NBVTP

Job 6 in the NET2

Job 6 in the NIV11

Job 6 in the NNT

Job 6 in the NNT2

Job 6 in the NNT3

Job 6 in the PDDPT

Job 6 in the PFNT

Job 6 in the RMNT

Job 6 in the SBIAS

Job 6 in the SBIBS

Job 6 in the SBIBS2

Job 6 in the SBICS

Job 6 in the SBIDS

Job 6 in the SBIGS

Job 6 in the SBIHS

Job 6 in the SBIIS

Job 6 in the SBIIS2

Job 6 in the SBIIS3

Job 6 in the SBIKS

Job 6 in the SBIKS2

Job 6 in the SBIMS

Job 6 in the SBIOS

Job 6 in the SBIPS

Job 6 in the SBISS

Job 6 in the SBITS

Job 6 in the SBITS2

Job 6 in the SBITS3

Job 6 in the SBITS4

Job 6 in the SBIUS

Job 6 in the SBIVS

Job 6 in the SBT

Job 6 in the SBT1E

Job 6 in the SCHL

Job 6 in the SNT

Job 6 in the SUSU

Job 6 in the SUSU2

Job 6 in the SYNO

Job 6 in the TBIAOTANT

Job 6 in the TBT1E

Job 6 in the TBT1E2

Job 6 in the TFTIP

Job 6 in the TFTU

Job 6 in the TGNTATF3T

Job 6 in the THAI

Job 6 in the TNFD

Job 6 in the TNT

Job 6 in the TNTIK

Job 6 in the TNTIL

Job 6 in the TNTIN

Job 6 in the TNTIP

Job 6 in the TNTIZ

Job 6 in the TOMA

Job 6 in the TTENT

Job 6 in the UBG

Job 6 in the UGV

Job 6 in the UGV2

Job 6 in the UGV3

Job 6 in the VBL

Job 6 in the VDCC

Job 6 in the YALU

Job 6 in the YAPE

Job 6 in the YBVTP

Job 6 in the ZBP